< Deuteronomy 16 >

1 “Observe the month of Abib, and you have made a Passover to your God YHWH, for in the month of Abib your God YHWH has brought you out of Egypt by night;
Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
2 and you have sacrificed a Passover to your God YHWH, of the flock and of the herd, in the place which YHWH chooses to cause His Name to dwell there.
Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
3 You do not eat any fermented thing with it; [for] seven days you eat unleavened things with it, bread of affliction (for you have come out of the land of Egypt in haste), so that you remember the day of your coming out of the land of Egypt all [the] days of your life;
Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
4 and leaven is not seen with you in all your border [for] seven days, and there does not remain [any] of the flesh which you sacrifice at evening on the first day until morning.
Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
5 You are not able to sacrifice the Passover within any of your gates which your God YHWH is giving to you,
Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
6 except at the place which your God YHWH chooses to cause His Name to dwell—there you sacrifice the Passover in the evening, at the going in of the sun, the season of your coming out of Egypt;
isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
7 and you have cooked and eaten in the place on which your God YHWH fixes, and have turned in the morning and gone to your tents;
Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
8 [for] six days you eat unleavened things, and on the seventh day [is] a restraint to your God YHWH; you do no work.
Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
9 You number seven weeks for yourself; you begin to number seven weeks from the beginning of the sickle among the standing grain,
Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
10 and you have observed the Celebration of Weeks to your God YHWH, a tribute of a free-will offering of your hand, which you give as your God YHWH blesses you.
Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
11 And you have rejoiced before your God YHWH, you, and your son, and your daughter, and your manservant, and your handmaid, and the Levite who [is] within your gates, and the sojourner, and the fatherless, and the widow, who [are] in your midst, in the place which your God YHWH chooses to cause His Name to dwell there,
Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
12 and you have remembered that you have been a servant in Egypt, and have observed and done these statutes.
Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
13 You observe the Celebration of Shelters for yourself [for] seven days, in your ingathering of your threshing-floor and of your wine-vat;
Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
14 and you have rejoiced in your celebration, you, and your son, and your daughter, and your manservant, and your handmaid, and the Levite, and the sojourner, and the fatherless, and the widow, who [are] within your gates.
Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
15 [For] seven days you celebrate before your God YHWH in the place which YHWH chooses, for your God YHWH blesses you in all your increase and in every work of your hands, and you have been only rejoicing.
Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
16 Three times in a year all of your males appear before your God YHWH in the place which He chooses: in the Celebration of Unleavened Things, and in the Celebration of Weeks, and in the Celebration of Shelters; and they do not appear before YHWH empty;
Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
17 each [gives] according to the gift of his hand, according to the blessing of your God YHWH, which He has given to you.
Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
18 You set for yourself judges and authorities within all your gates which your God YHWH is giving to you, for your tribes; and they have judged the people [with] a righteous judgment.
Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
19 You do not turn aside judgment; you do not discern faces, nor take a bribe, for the bribe blinds the eyes of the wise and perverts the words of the righteous.
Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
20 Righteousness—you pursue righteousness, so that you live and have possessed the land which your God YHWH is giving to you.
Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
21 You do not plant an Asherah of any trees for yourself near the altar of your God YHWH, which you make for yourself,
Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
22 and you do not raise up any standing image for yourself which your God YHWH is hating.”
wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.

< Deuteronomy 16 >