< Colossians 4 >

1 The masters: give that which is righteous and equal to the servants, having known that you also have a Master in the heavens.
Mabwana, toeni kwa watumwa mambo yaliyo haki na ya adili. Mnajua pia kwamba mnaye Bwana mbinguni.
2 Continue in the prayer, watching in it in thanksgiving,
Endeleeni kuwa thabiti katika maombi. Kaeni macho katika hilo kwa shukrani.
3 also praying for us at the same time, that God may open to us a door for the word, to speak the secret of the Christ, because of which I have also been bound,
Ombeni pamoja kwa ajili yetu pia, ili kwamba Mungu afungue mlango kwa ajili ya neno, kunena siri ya ukweli ya Kristo. Kwa sababu ya hili nimefungwa minyororo.
4 that I may reveal it, as it is necessary for me to speak.
Na ombeni kwamba niweze kuliweka wazi, kama inavyonipasa kusema.
5 Walk in wisdom toward those outside, redeeming the time,
Enenda kwa hekima kwa wale walioko nje, na muukomboe wakati.
6 your word always being seasoned with salt in grace—to know how it is necessary for you to answer each one.
Maneno yenu na yawe na neema wakati wote, na yakolee chumvi majira yote, ili kwamba mweze kujua jinsi inavyowapasa kumjibu kila mtu.
7 Tychicus will make known to you all the things concerning me—the beloved brother, and faithful servant, and fellow-servant in the LORD—
Kwa mambo yanayonihusu mimi, Tikiko atayafanya yajulikane kwenu. Yeye ni ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, na mtumwa mwenzetu katika Bwana.
8 whom I sent to you for this very thing, that he might know the things concerning you, and might comfort your hearts,
Namtuma kwenu kwa ajili ya hili, kwamba mweze kujua mambo kuhusu sisi na pia kwamba aweze kuwatia moyo.
9 with Onesimus the faithful and beloved brother, who is of you; they will make known to you all things that [are] here.
Namtuma pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa mwaminifu, na mmoja wenu. Watawaambia kila kitu kilichotokea hapa.
10 Aristarchus greets you, my fellow-captive, and Marcus, the nephew of Barnabas (concerning whom you received commands—if he may come to you, receive him),
Aristarko, mfungwa mwenzangu, anawasalimu, pia na Marko binamu yake na Barnaba mliyepokea utaratibu kutoka kwake, “kama akija kwenu, mpokeeni,”
11 and Jesus who is called Justus, who are of circumcision: these [are the] only fellow-workers for the Kingdom of God who become a comfort to me.
Na pia Yesu aitwaye Yusto. Hawa peke yao wa tohara ni watendakazi wenzangu kwa jili ya ufalme wa Mungu. Wamekuwa ni faraja kwangu.
12 Epaphras greets you, who [is] of you, a servant of Christ, always striving for you in the prayers, that you may stand perfect and made full in all the will of God,
Epafra anawasalimu. Yeye ni mmoja wenu na mtumwa wa Kristo Yesu. Yeye hufanya bidii katika maombi kwa ajili, ili kwamba mweze kusimama kwa ukamilifu na kuhakishwa kikamilifu katika mapenzi yote ya Mungu.
13 for I testify to him that he has much zeal for you, and those in Laodicea, and those in Hierapolis.
Kwa kuwa ninamshuhudia, kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa hao walioko Laodekia, na kwa hao walioko Hierapoli.
14 Lucas greets you, the beloved physician, and Demas;
Luka yule tabibu mpendwa, na Dema wanawasalimu.
15 those in Laodicea greet you—brothers, and Nymphas, and the assembly in his house;
Wasalimu ndugu zangu walioko Laodekia, na Nimfa, na kanisa lile lililoko nyumbani kwake.
16 and when the letter may be read with you, cause that it may also be read in the assembly of the Laodiceans, and the [letter] from Laodicea that you also may read;
Barua hii itakapokuwa imesomwa miongoni mwenu, isomwe pia kwa kanisa la walaodekia, nanyi pia hakikisheni mnaisoma ile barua kutoka Laodekia.
17 and say to Archippus, “See to the ministry that you received in the LORD, that you may fulfill it.”
Sema kwa Arkipo, ''Angalia ile huduma ambayo umeipokea katika Bwana, kwamba unapaswa kuitimiza.”
18 The salutation [is] by my hand, Paul. Remember my bonds. The grace [is] with you! Amen.
Salamu hii ni kwa mkono wangu mwenyewe - Paulo. Ikuumbukeni minyororo yangu. Neema na iwe nanyi.

< Colossians 4 >