< Amos 9 >
1 I have seen the Lord standing by the altar, and He says, “Strike the knob, and the thresholds shake, And cut them off by the head—all of them, And I slay their posterity with a sword, None that flee of them flee away, Nor a fugitive of them escape.
Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
2 If they dig through into Sheol, From there My hand takes them, And if they go up [to] the heavens, From there I cause them to come down. (Sheol )
Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol )
3 And if they are hid in the top of Carmel, From there I search out, and have taken them, And if they are hid from My eyes in the bottom of the sea, From there I command the serpent, And it has bitten them.
Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
4 And if they go into captivity before their enemies, From there I command the sword, And it has slain them, And I have set My eye on them for evil, And not for good.”
Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
5 And [it is] the Lord, YHWH of Hosts, Who is striking against the land, and it melts, And mourned have all the inhabitants in it, And all of it has come up as a flood, And it has sunk—like the flood of Egypt.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
6 Who is building His upper chambers in the heavens; As for His troop, On earth He has founded it, Who is calling for the waters of the sea, And pours them out on the face of the land, YHWH [is] His Name.
yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
7 “Are you not as sons of Cushim to Me, O sons of Israel?” A declaration of YHWH. “Did I not bring Israel up out of the land of Egypt? And the Philistines from Caphtor, and Aram from Kir?
“Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
8 Behold, [the] eyes of Lord YHWH [are] on the sinful kingdom, And I have destroyed it from off the face of the ground, Only, I do not utterly destroy the house of Jacob,” A declaration of YHWH.
“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
9 “For behold, I am commanding, And I have shaken among all the nations the house of Israel, As [one] shakes with a sieve, And there does not fall a grain [to] the earth.
“Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
10 By sword all sinners of My people die, Who are saying, Evil does not overtake, or go before, For our sakes.
Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
11 In that day I raise the dwelling place of David that is fallen, And I have repaired their breaches, And I raise up its ruins, And I have built it up as in days of old,
“Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
12 So that they possess the remnant of Edom, And all the nations on whom My Name is called,” A declaration of YHWH—the doer of this.
ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
13 “Behold, days are coming,” A declaration of YHWH, “And the plowman has come near to the reaper, And the treader of grapes to the scatterer of seed, And the mountains have dropped juice, And all the hills melt.
“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
14 And I have turned back [to] the captivity of My people Israel, And they have built desolate cities, and inhabited, And have planted vineyards, and drunk their wine, And made gardens, and eaten their fruit.
Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
15 And I have planted them on their own ground, And they are not plucked up anymore from off their own ground, That I have given to them,” said your God YHWH!
Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.