< Amos 6 >
1 Woe [to] those secure in Zion, And those confident on the mountain of Samaria, The marked of the chief of the nations, And the house of Israel has come to them.
Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
2 Pass over [to] Calneh and see, And go there [to] Hamath the great, And go down [to] Gath of the Philistines, Are [they] better than these kingdoms? [Is] their border greater than your border?
Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
3 Who are putting away the day of evil, And you bring the seat of violence near,
Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
4 Who are lying down on beds of ivory, And are spread out on their couches, And are eating lambs from the flock, And calves from the midst of the stall,
Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
5 Who are taking part according to the stringed instrument, Like David they invented for themselves instruments of music;
Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
6 Who are drinking with bowls of wine, And anoint themselves [with] chief perfumes, And have not been pained for the breach of Joseph.
Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
7 Therefore they now go at the head of the captives, And the mourning-feast of stretched-out ones is turned aside.
Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
8 Lord YHWH has sworn by Himself, A declaration of YHWH, God of Hosts: “I am abominating the excellence of Jacob, And his high places I have hated, And I have delivered up the city and its fullness.”
“Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
9 And if there are left ten persons in one house, It has come to pass—that they have died.
Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
10 And his loved one has lifted him up, even his burner, To bring forth the bones from the house, And he said to him who [is] in the sides of the house, “Is there [any] yet with you?” And he said, “None,” Then he said, “Hush! We must not make mention of the Name of YHWH.”
Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
11 For behold, YHWH is commanding, And He has struck the great house [with] breaches, And the little house [with] clefts.
Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
12 Do horses run on a rock? Does one plow [it] with oxen? For you have turned judgment to gall, And the fruit of righteousness to wormwood.
Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
13 O you who are rejoicing at nothing, Who are saying, “Have we not taken to ourselves horns by our strength?”
Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
14 “Surely, behold, I am raising a nation against you, O house of Israel,” A declaration of YHWH, God of Hosts, “And they have oppressed you from the coming in to Hamath, To the stream of the desert.”
Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”