< Acts 27 >

1 And when our sailing to Italy was determined, they were delivering up both Paul and certain others, prisoners, to a centurion, by name Julius, of the band of Sebastus,
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 and having embarked in a ship of Adramyttium, we, being about to sail by the coasts of Asia, set sail, there being with us Aristarchus, a Macedonian of Thessalonica,
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 on the next [day] also we touched at Sidon, and Julius, courteously treating Paul, permitted [him], having gone on to friends, to receive [their] care.
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 And there, having set sail, we sailed under Cyprus, because of the winds being contrary,
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 and having sailed over the sea down by Cilicia and Pamphylia, we came to Myria of Lycia,
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 and there the centurion having found a ship of Alexandria, sailing to Italy, put us into it,
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 and having sailed slowly many days, and with difficulty coming down by Cnidus, the wind not permitting us, we sailed under Crete, down by Salmone,
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 and hardly passing it, we came to a certain place called Fair Havens, near to which was the city of Lasaea.
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 And much time being spent, and the sailing now being dangerous—because of the fast also being already past—Paul was admonishing,
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 saying to them, “Men, I perceive that with hurt, and much damage, not only of the load and of the ship, but also of our lives—the voyage is about to be”;
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 but the centurion gave more credence to the pilot and to the shipowner than to the things spoken by Paul;
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 and the haven being not well placed to winter in, the greater part gave counsel to sail from there, if somehow they might be able, having attained to Phoenix, to winter [there], [which is] a haven of Crete, looking to the southwest and northwest,
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 and a south wind blowing softly, having thought they had obtained [their] purpose, having lifted anchor, they sailed close by Crete,
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 and not long after, there came down from it a turbulent wind [that] is called the Euroclydon,
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 and the ship being caught, and not being able to bear up against the wind, having given [her] up, we were carried on,
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 and having run under a certain little island called Clauda, we were hardly able to become masters of the boat,
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 which having taken up, they were using helps, undergirding the ship, and fearing lest they may fall into the [sandbars of] Syrtis, having let down the mast—so were carried on.
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 And we, being exceedingly storm-tossed, the succeeding [day] they were making a clearing,
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 and on the third [day] we cast out the tackling of the ship with our own hands,
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 and neither sun nor stars appearing for more days, and not a little storm lying on us, from then on all hope was taken away of our being saved.
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 And there having been long fasting, then Paul having stood in the midst of them, said, “It was necessary, indeed, O men—having listened to me—not to set sail from Crete, and to save this hurt and damage;
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 and now I exhort you to be of good cheer, for there will be no loss of life among you—but of the ship;
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 for this night there stood by me a messenger of God—whose I am, and whom I serve—
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 saying, Do not be afraid Paul; it is necessary for you to stand before Caesar; and behold, God has granted to you all those sailing with you;
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 for this reason be of good cheer, men! For I believe God, that so it will be, even as it has been spoken to me,
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 and on a certain island it is necessary for us to be cast.”
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 And when the fourteenth night came—we being carried up and down in the Adria—toward the middle of the night the sailors were supposing that some country drew near to them;
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 and having sounded they found twenty fathoms, and having gone a little farther, and again having sounded, they found fifteen fathoms,
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 and fearing lest we may fall on rough places, having cast four anchors out of the stern, they were wishing day to come.
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 And the sailors seeking to flee out of the ship, and having let down the boat to the sea, in pretense as [if] out of the prow they are about to cast anchors,
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 Paul said to the centurion and to the soldiers, “If these do not remain in the ship—you are not able to be saved”;
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 then the soldiers cut off the ropes of the boat, and permitted it to fall off.
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 And until the day was about to be, Paul was calling on all to partake of nourishment, saying, “Fourteen days today, waiting, you continue fasting, having taken nothing,
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 for this reason I call on you to take nourishment, for this is for your safety, for of not one of you will a hair fall from the head”;
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 and having said these things, and having taken bread, he gave thanks to God before all, and having broken [it], he began to eat;
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 and all having become of good cheer, also took food themselves,
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 (and we were—all the souls in the ship—two hundred, seventy-six),
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 and having eaten sufficient nourishment, they were lightening the ship, casting forth the wheat into the sea.
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 And when the day came, they were not discerning the land, but were perceiving a certain bay having a beach, into which they took counsel, if possible, to thrust forward the ship,
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 and having taken up the anchors, they were committing [it] to the sea, at the same time—having loosed the bands of the rudders, and having hoisted up the foresail to the wind—they were making for the shore,
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 and having fallen into a place of two seas, they ran the ship aground, and the prow, indeed, having stuck fast, remained immoveable, but the stern was broken by the violence of the waves.
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 And the soldiers’ counsel was that they should kill the prisoners, lest anyone having swam out should escape,
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 but the centurion, resolving to save Paul, hindered them from the counsel, and commanded those able to swim, having cast themselves out first—to get to the land,
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 and the rest, some indeed on boards, and some on certain things of the ship; and thus it came to pass that all came safe to the land.
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.

< Acts 27 >