< Acts 19 >

1 And it came to pass, in Apollos being in Corinth, Paul having gone through the upper parts, came to Ephesus, and having found certain disciples,
Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2 he said to them, “Having believed, did you receive the Holy Spirit?” And they said to him, “But we did not even hear whether there is any Holy Spirit”;
Akauliza, “Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?” Nao wakamjibu, “La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia.”
3 and he said to them, “Into what, then, were you immersed?” And they said, “Into John’s immersion.”
Naye akasema, “Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?” Wakamjibu, “Ubatizo wa Yohane.”
4 And Paul said, “John, indeed, immersed with an immersion of conversion, saying to the people that they should believe in Him who is coming after him—that is, in the Christ—Jesus”;
Naye Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu.”
5 and they, having heard, were immersed into the Name of the Lord Jesus,
Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6 and Paul having laid [his] hands on them, the Holy Spirit came on them, they were also speaking with tongues, and prophesying,
Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7 and all the men were, as it were, twelve.
Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8 And having gone into the synagogue, he was speaking boldly for three months, reasoning and persuading the things concerning the Kingdom of God,
Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9 and when certain were hardened and were disbelieving, speaking evil of The Way before the multitude, having departed from them, he separated the disciples, reasoning every day in the school of a certain Tyrannus.
Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10 And this happened for two years so that all those dwelling in Asia heard the word of the Lord Jesus, both Jews and Greeks,
Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11 also mighty works—not common—God was working through the hands of Paul,
Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12 so that even to the ailing were brought from his body handkerchiefs or aprons, and the diseases departed from them; the evil spirits also went forth from them.
Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13 And certain of the wandering exorcist Jews, took on [them] to name over those having the evil spirits the Name of the Lord Jesus, saying, “We adjure you by Jesus, whom Paul preaches”;
Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: “Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri.”
14 and there were certain—seven sons of Sceva, a Jew, a chief priest—who are doing this thing;
Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15 and the evil spirit, answering, said, “I know Jesus, and I am acquainted with Paul; and you—who are you?”
Lakini pepo mbaya aliwajibu, “Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?”
16 And the man, in whom was the evil spirit, leaping on them, and having overcome them, prevailed against them, so that they fled naked and wounded out of that house,
Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17 and this became known to all, both Jews and Greeks, who are dwelling at Ephesus, and fear fell on them all, and the Name of the Lord Jesus was being magnified;
Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18 many also of those who believed were coming, confessing and declaring their acts,
Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19 and many of those who had practiced the superfluous arts, having brought the scrolls together, were burning [them] before all; and they reckoned together the prices of them, and found [it] fifty thousand pieces of silver,
Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20 so powerfully was the word of God increasing and prevailing.
Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21 And when these things were fulfilled, Paul purposed in the Spirit, having gone through Macedonia and Achaia, to go on to Jerusalem, saying, “After my being there, it is also necessary for me to see Rome”;
Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.”
22 and having sent to Macedonia two of those ministering to him—Timotheus and Erastus—he himself stayed a time in Asia.
Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23 And there came, at that time, not a little stir about The Way,
Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24 for a certain one, Demetrius by name, a worker in silver, making silver sanctuaries of Artemis, was bringing to the craftsmen not a little gain,
Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25 whom, having brought in a crowd together, and those who worked around such things, he said, “Men, you know that by this work we have our wealth;
Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26 and you see and hear, that not only at Ephesus, but almost in all Asia, this Paul, having persuaded, turned away a great multitude, saying that they who are made by hands are not gods;
Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27 and not only is this department in danger for us of coming into disregard, but also, that of the great goddess Artemis, the temple is to be reckoned for nothing, and also her greatness is about to be brought down, whom all Asia and the world worships.”
Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
28 And having heard, and having become full of wrath, they were crying out, saying, “Great [is] the Artemis of the Ephesians!”
Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi, wa Efeso!”
29 And the whole city was filled with confusion; they rushed also with one accord into the theater, having caught Gaius and Aristarchus, Macedonians, Paul’s fellow-travelers.
Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30 And on Paul’s resolving to enter in to the populace, the disciples were not permitting him,
Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31 and also some of the chief men of Asia, being his friends, having sent to him, were pleading [with] him not to venture into the theater himself.
Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32 Some indeed, therefore, were calling out one thing, and some another, for the assembly was confused, and the greater part did not know for what they had come together;
Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33 and out of the multitude they put forward Alexander—the Jews thrusting him forward—and Alexander having beckoned with the hand, wished to make defense to the populace,
Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34 and having known that he is a Jew, one voice came out of all, for about two hours, crying, “Great [is] the Artemis of the Ephesians!”
Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35 And the public clerk having quieted the multitude, says, “Men, Ephesians, why, who is the man that does not know that the city of the Ephesians is temple-keeper of the great goddess Artemis, and of that which fell down from Zeus?
Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36 These things, then, being undeniable, it is necessary for you to be quiet, and to do nothing rashly.
Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37 For you brought these men, who are neither temple-robbers nor slandering of your goddess;
Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38 if indeed, therefore, Demetrius and the craftsmen with him have a matter with anyone, court [days] are held, and there are proconsuls; let them accuse one another.
Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39 And if you seek after anything concerning other matters, it will be determined in the legal assembly;
Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40 for we are also in peril of being accused of insurrection in regard to this day, there being no occasion by which we will be able to give an account of this concourse”;
Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.”
41 and having said these things, he dismissed the assembly.
Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.

< Acts 19 >