< Acts 15 >

1 And certain having come down from Judea, were teaching the brothers, “If you are not circumcised after the custom of Moses, you are not able to be saved”;
Basi, watu wengine walifika Antiokia kutoka Yudea wakaanza kuwafundisha wale ndugu wakisema, “Kama hamtatahiriwa kufuatana na mapokeo ya Sheria ya Mose, hamtaweza kuokolewa.”
2 there having been, therefore, not a little dissension and debate to Paul and Barnabas with them, they arranged for Paul and Barnabas, and certain others of them, to go up to the apostles and elders to Jerusalem about this question;
Jambo hili lilisababisha ubishi mkubwa, na baada ya Paulo na Barnaba kujadiliana nao, ikaamuliwa Paulo na Barnaba pamoja na waumini kadhaa wa lile kanisa la Antiokia waende Yerusalemu kuwaona wale mitume na wazee kuhusu jambo hilo.
3 they indeed, then, having been sent forward by the assembly, were passing through Phoenicia and Samaria, declaring the conversion of the nations, and they were causing great joy to all the brothers.
Basi, kanisa liliwaaga, nao walipokuwa wanapitia Foinike na Samaria waliwaeleza watu jinsi mataifa mengine yalivyomgeukia Mungu. Habari hizo zikawafurahisha sana ndugu hao wote.
4 And having come to Jerusalem, they were received by the assembly, and the apostles, and the elders; they also declared as many things as God did with them;
Walipofika Yerusalemu walikaribishwa na kanisa, mitume na wazee; nao wakawapa taarifa juu ya yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.
5 and there rose up certain of those of the sect of the Pharisees who believed, saying, “It is required to circumcise them, to command them also to keep the Law of Moses.”
Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, “Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata Sheria ya Mose.”
6 And there were gathered together the apostles and the elders, to see about this matter,
Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalum wa kuchunguza jambo hilo.
7 and there having been much disputing, Peter having risen up said to them, “Men, brothers, you know that from former days God made choice among us, through my mouth, for the nations to hear the word of the good news, and to believe;
Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama, akasema, “Ndugu zangu, ninyi mnafahamu kwamba hapo awali Mungu alipenda kunichagua mimi miongoni mwenu niihubiri Habari Njema, ili watu wa mataifa wapate kusikia na kuamini.
8 and the heart-knowing God bore them testimony, having given to them the Holy Spirit, even as also to us,
Naye Mungu anayejua mioyo ya watu, alithibitisha kwamba amewakubali kwa kuwapa nao Roho Mtakatifu kama alivyotupa sisi.
9 and also put no difference between us and them, having purified their hearts by faith;
Hakufanya ubaguzi wowote kati yetu na wao; aliitakasa mioyo yao kwa imani.
10 now, therefore, why do you tempt God, to put a yoke on the neck of the disciples, which neither our fathers nor we were able to bear?
Sasa basi, kwa nini kumjaribu Mungu kwa kuwatwika hao waumini mzigo ambao wala babu zetu, wala sisi hatukuweza kuubeba?
11 But through the grace of the Lord Jesus Christ, we believe to be saved, even as also they.”
Isiwe hivyo, ila tunaamini kwamba, sisi kama vile wao, tunaokolewa kwa njia ya neema ya Bwana Yesu.”
12 And all the multitude kept silence and were listening to Barnabas and Paul expounding as many signs and wonders as God did among the nations through them;
Kikundi chote kilikaa kimya, kikawasikiliza Barnaba na Paulo wakieleza miujiza na maajabu ambayo Mungu alitenda kwa mikono yao kati ya watu wa mataifa mengine.
13 and after they were silent, James answered, saying, “Men, brothers, listen to me:
Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: “Ndugu zangu, nisikilizeni!
14 Simeon expounded how at first God looked on [us] to take a people out of [the] nations for His Name,
Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.
15 and to this the words of the Prophets agree, as it has been written:
Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
16 After these things I will return, And I will rebuild the dwelling place of David that has fallen down, And I will rebuild its ruins, And will set it upright—
Baada ya mambo haya nitarudi. Nitaijenga tena ile nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitayatengeneza magofu yake na kuijenga tena.
17 That the remnant of men may seek after the LORD, And all the nations on whom My Name has been called, Says the LORD, who is doing all these things.
Hapo watu wengine wote, watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu, watamtafuta Bwana.
18 Known from the ages to God are all His works. (aiōn g165)
Ndivyo asemavyo Bwana, aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale. (aiōn g165)
19 For this reason I judge: not to trouble those who turn back to God from the nations,
“Kwa hiyo, uamuzi wangu ni huu: tusiwataabishe watu wa mataifa wanomgeukia Mungu.
20 but to write to them to abstain from the defilements of the idols, and the whoredom, and the strangled thing, and the blood;
Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa najisi kwa kutambikiwa sanamu za miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.
21 for Moses has those preaching him from former generations in every city—being read every Sabbath in the synagogues.”
Kwa maana kwa muda mrefu maneno ya Mose yamekuwa yakihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masunagogi yote kila siku ya Sabato.”
22 Then it seemed good to the apostles and the elders, with the whole assembly, to send to Antioch with Paul and Barnabas chosen men out of themselves—Judas surnamed Barsabas, and Silas, leading men among the brothers—
Mitume, wazee na kanisa lote waliamua kuwachagua watu fulani miongoni mwao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Basi, wakamchagua Yuda aitwaye pia Barsaba, na Sila ambao wote walikuwa wanajulikana zaidi kati ya ndugu.
23 having written through their hand thus: “The apostles, and the elders, and the brothers, to those in Antioch, and Syria, and Cilicia, brothers, who [are] of the nations, greeting;
Wakawapa barua hii: “Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, tunawasalimuni ninyi ndugu wa mataifa mengine mlioko huko Antiokia, Siria na Kilikia.
24 seeing we have heard that some having gone forth from us troubled you with words, subverting your souls, saying to be circumcised and to keep the Law, to whom we gave no charge,
Tumesikia kwamba watu wengine kutoka huku kwetu waliwavurugeni kwa maneno yao, wakaitia mioyo yenu katika wasiwasi. Lakini wamefanya hivyo bila ya idhini yoyote kutoka kwetu.
25 it seemed good to us, having come together with one accord, to send to you chosen men, with our beloved Barnabas and Paul—
Hivyo, tumeamua kwa pamoja kuwachagua watu kadhaa na kuwatuma kwenu pamoja na wapenzi wetu Barnaba na Paulo,
26 men who have given up their lives for the Name of our Lord Jesus Christ—
ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
27 we have sent, therefore, Judas and Silas, and they are telling the same things by word.
Kwa hiyo, tunawatuma Yuda na Sila kwenu; hawa watawaambieni wao wenyewe haya tuliyoandika.
28 For it seemed good to the Holy Spirit, and to us, to lay no more burden on you, except these necessary things:
Basi, Roho Mtakatifu na sisi tumekubali tusiwatwike mzigo zaidi ya mambo haya muhimu:
29 to abstain from things offered to idols, and blood, and a strangled thing, and whoredom; keeping yourselves from which, you will do well; be strong!”
Msile vyakula vilivyotambikiwa sanamu; msinywe damu; msile nyama ya mnyama aliyenyongwa; na mjiepushe na uasherati. Mtakuwa mmefanya vema kama mkiepa kufanya mambo hayo. Wasalaam!”
30 They then, indeed, having been let go, went to Antioch, and having brought the multitude together, delivered the letter,
Baada ya kuwaaga, hao wajumbe walielekea Antiokia ambako waliita mkutano wa waumini, wakawapa hiyo barua.
31 and having read [it] they rejoiced for the consolation;
Walipoisoma hiyo barua, maneno yake yaliwatia moyo, wakafurahi sana.
32 Judas also and Silas, also being prophets themselves, through much discourse exhorted the brothers, and confirmed,
Yuda na Sila, ambao nao walikuwa manabii, walizungumza na hao ndugu kwa muda mrefu wakiwatia moyo na kuwaimarisha.
33 and having passed some time, they were let go with peace from the brothers to the apostles;
Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu wa Antiokia waliwaaga wakiwatakia amani, kisha wakarudi kwa wale waliokuwa wamewatuma.
34 [[and it seemed good to Silas to remain there still.]]
Lakini Sila aliamua kubaki.
35 And Paul and Barnabas continued in Antioch, teaching and proclaiming good news—with many others also—the word of the LORD;
Paulo na Barnaba walibaki huko Antiokia kwa muda; wakafundisha na kuhubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.
36 and after certain days, Paul said to Barnabas, “Having turned back again, we may look after our brothers, in every city in which we have preached the word of the LORD—how they are.”
Baada ya siku kadhaa, Paulo alimwambia Barnaba, “Turudi tukawatembelee wale ndugu katika kila mji tulikolihubiri neno la Bwana tukajionee jinsi wanavyoendelea.”
37 And Barnabas resolved to take with [them] John called Mark,
Barnaba alitaka wamchukue pia Yohane aitwaye Marko.
38 and Paul was not thinking it good to take him with them who withdrew from them from Pamphylia, and did not go with them to the work;
Lakini Paulo hakupendelea kumchukua Marko, ambaye awali aliwaacha kule Pamfulia na kukataa kushiriki katika kazi yao.
39 there came, therefore, a sharp contention, so that they were parted from one another, and Barnabas having taken Mark, sailed to Cyprus,
Basi kukatokea ubishi mkali kati yao, na wakaachana. Barnaba akamchukua Marko, wakapanda meli kwenda Kupro.
40 and Paul having chosen Silas, went forth, having been given up to the grace of God by the brothers;
Naye Paulo akamchagua Sila, na baada ya ndugu wa mahali hapo kumweka chini ya ulinzi wa neema ya Bwana, akaondoka.
41 and he went through Syria and Cilicia, confirming the assemblies.
Katika safari hiyo alipitia Siria na Kilikia akiyaimarisha makanisa.

< Acts 15 >