< Acts 14 >
1 And it came to pass in Iconium, that they entered together into the synagogue of the Jews, and spoke, so that there believed a great multitude of both Jews and Greeks;
Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2 and the unbelieving Jews stirred up and made the souls of the nations evil against the brothers;
Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3 [for a] long time, indeed, therefore, they abided speaking boldly in the LORD, who is testifying to the word of His grace, and granting signs and wonders to come to pass through their hands.
Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4 And the multitude of the city was divided, and some were with the Jews, and some with the apostles,
Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5 and when there was a purpose both of the nations and of the Jews with their rulers to mistreat [them], and to stone them,
Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6 they having become aware, fled to the cities of Lycaonia, Lystra, and Derbe, and the surrounding region,
Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7 and there they were proclaiming good news.
wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8 And a certain man in Lystra, impotent in the feet, was sitting, being lame from the womb of his mother—who never had walked;
Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9 this one was hearing Paul speaking, who, having steadfastly beheld him, and having seen that he has faith to be saved,
Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10 said with a loud voice, “Stand up on your feet upright”; and he was springing and walking,
akasema kwa sauti kubwa, “Simama wima kwa miguu yako!” Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11 and the multitudes having seen what Paul did, lifted up their voice in the speech of Lycaonia, saying, “The gods, having become like men, came down to us”;
Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: “Miungu imetujia katika sura za binadamu!”
12 they were also calling Barnabas Zeus, and Paul Hermes, since he was the leader in speaking.
Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13 And the priest of the Zeus that is before their city, having brought oxen and garlands to the porches, wished to sacrifice with the multitudes,
Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14 and having heard, the apostles Barnabas and Paul, having torn their garments, sprung into the multitude, crying
Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15 and saying, “Men, why do you do these things? And we are similar-feeling men with you, proclaiming good news to you, to turn to the living God from these vanities, who made the heaven, and the earth, and the sea, and all the things in them;
“Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16 who in the past generations permitted all the nations to go on in their ways,
Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17 though, indeed, He did not leave Himself without witness, doing good—giving rains to us from Heaven, and fruitful seasons, filling our hearts with food and gladness”;
Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”
18 and saying these things, they scarcely restrained the multitudes from sacrificing to them.
Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19 And there came there, from Antioch and Iconium, Jews, and they having persuaded the multitudes, and having stoned Paul, drew him outside of the city, having supposed him to be dead;
Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20 and the disciples having surrounded him, having risen he entered into the city, and on the next day he went forth with Barnabas to Derbe.
Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21 Having also proclaimed good news to that city, and having discipled many, they turned back to Lystra, and Iconium, and Antioch,
Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22 confirming the souls of the disciples, exhorting to remain in the faith, and that it is required of us to enter into the Kingdom of God through many tribulations,
Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, “Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu.”
23 and having appointed to them elders in every assembly by vote, having prayed with fastings, they commended them to the LORD in whom they had believed.
Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24 And having passed through Pisidia, they came to Pamphylia,
Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25 and having spoken the word in Perga, they went down to Attalia,
Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26 and [from] there sailed to Antioch, from where they had been given by the grace of God for the work that they fulfilled;
Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27 and having come and gathered the assembly together, they declared as many things as God did with them, and that He opened a door of faith to the nations;
Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28 and they abided there with the disciples [for] not a short time.
Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.