< Acts 14 >
1 And it came to pass in Iconium, that they entered together into the synagogue of the Jews, and spoke, so that there believed a great multitude of both Jews and Greeks;
Ikatokea ndani ya Ikonio kwamba Paulo na Barnaba waliingia pamoja ndani ya sinagogi la Wayahudi nakuongea namna ambayo kundi kubwa la watu Wayahudi na Wayunani waliamini.
2 and the unbelieving Jews stirred up and made the souls of the nations evil against the brothers;
Lakini wayahudi wasiotii waliwachochea akili wamataifa na kuwafanya kuwa wabaya dhidi ya ndugu.
3 [for a] long time, indeed, therefore, they abided speaking boldly in the LORD, who is testifying to the word of His grace, and granting signs and wonders to come to pass through their hands.
Kwa hiyo walikaa huko kwa muda mrefu, wakiongea kwa ujasiri kwa nguvu ya Bwana, huku akitoa uthibitisho kuhusu ujumbe wa neema yake. Alifanya hivi kwa kutoa ishara na majaabu vifanywe kwa mikono ya Paulo na Barnaba.
4 And the multitude of the city was divided, and some were with the Jews, and some with the apostles,
Lakini eneo kubwa la mji liligawanyika: baadhi ya watu walikuwa pamoja na Wayahudi, na baadhi pamoja na mitume.
5 and when there was a purpose both of the nations and of the Jews with their rulers to mistreat [them], and to stone them,
Wakati wamataifa na Wayahudi walipojaribu kuwashawishi viongozi wao kuwatendea vibaya na kuwaponda mawe Paulo na Barnaba,
6 they having become aware, fled to the cities of Lycaonia, Lystra, and Derbe, and the surrounding region,
wakalitambua hilo na kukimbilia katika miji ya Likaonia, Listra na Derbe, na maeneo yanayozunguka pale,
7 and there they were proclaiming good news.
na huko waliihubiri injili.
8 And a certain man in Lystra, impotent in the feet, was sitting, being lame from the womb of his mother—who never had walked;
Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja aliyekaa, hakuwa na nguvu miguuni mwake, kilema kutoka tumboni mwa mama yake, hajawahi kutembea.
9 this one was hearing Paul speaking, who, having steadfastly beheld him, and having seen that he has faith to be saved,
Mtu huyu alimsikia Paulo akiongea. Paulo alimkazia macho na akaona kwamba alikuwa na imani ya kuponywa.
10 said with a loud voice, “Stand up on your feet upright”; and he was springing and walking,
Hivyo alisema kwake kwa sauti ya juu, “Simama kwa miguu yako.” Na yule mtu aliruka juu na kuanza kutembea.
11 and the multitudes having seen what Paul did, lifted up their voice in the speech of Lycaonia, saying, “The gods, having become like men, came down to us”;
Umati ulipoona alichokifanya Paulo, waliinua sauti zao, wakisema katika lahaja ya Kilikaonio, “miungu imetushukia kwa namna ya binadamu.”
12 they were also calling Barnabas Zeus, and Paul Hermes, since he was the leader in speaking.
Walimwita Barnaba “Zeu,” na Paulo “Herme” kwa sababu alikuwa msemaji mkuu.
13 And the priest of the Zeus that is before their city, having brought oxen and garlands to the porches, wished to sacrifice with the multitudes,
Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje ya mji, alileta fahari la ng'ombe na mtungo wa maua mpaka kwenye lango la mji, yeye na umati walitaka kutoa sadaka.
14 and having heard, the apostles Barnabas and Paul, having torn their garments, sprung into the multitude, crying
Lakini mitume, Barnaba na Paulo, walipolisikia hili, walirarua mavazi yao na kwa haraka walikwenda nje kwenye umati, wakilia
15 and saying, “Men, why do you do these things? And we are similar-feeling men with you, proclaiming good news to you, to turn to the living God from these vanities, who made the heaven, and the earth, and the sea, and all the things in them;
na kusema, “Enyi watu, kwanini mnafanya mambo haya? Na sisi pia ni binadamu wenye hisia kama za kwenu. Tunawaletea habari njema, kwamba mgeuke kutoka kwenye vitu hivi visivyofaa na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu, dunia na bahari na kila kitu kilichomo.
16 who in the past generations permitted all the nations to go on in their ways,
Katika nyakati zilizopita, aliwaruhusu mataifa kutembea katika njia zao wenyewe.
17 though, indeed, He did not leave Himself without witness, doing good—giving rains to us from Heaven, and fruitful seasons, filling our hearts with food and gladness”;
Lakini bado, hakuondoka pasipo shahidi, katika hilo alifanya vizuri na akawapatia mvua kutoka mbinguni na nyakati za mazao, akiwajaza mioyo yenu kwa vyakula na furaha”
18 and saying these things, they scarcely restrained the multitudes from sacrificing to them.
Hata kwa maneno haya, Paulo na Barnaba kwa shida waliuzuia umati kuwatolea sadaka.
19 And there came there, from Antioch and Iconium, Jews, and they having persuaded the multitudes, and having stoned Paul, drew him outside of the city, having supposed him to be dead;
Lakini baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio walikuja kuushawishi umati. Wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji, wakidhani alikuwa amekufa.
20 and the disciples having surrounded him, having risen he entered into the city, and on the next day he went forth with Barnabas to Derbe.
Hata hivyo wanafunzi walikuwa wamesimama karibu naye, aliamka, wakaingia mjini. Siku ya pili, aliende Derbe na Barnaba.
21 Having also proclaimed good news to that city, and having discipled many, they turned back to Lystra, and Iconium, and Antioch,
Baada ya kufundisha injili katika mji ule na kuwafanya wanafunzi wengi, walirudi Listra, hadi Ikoniamu, na hadi Antiokia.
22 confirming the souls of the disciples, exhorting to remain in the faith, and that it is required of us to enter into the Kingdom of God through many tribulations,
Waliendelea kuimarisha nafsi za wanafunzi na kutiwa moyo kuendelea katika imani, akasema, “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kwa kupitia mateso mengi.”
23 and having appointed to them elders in every assembly by vote, having prayed with fastings, they commended them to the LORD in whom they had believed.
Walipo wateua kwa ajili yao wazee wa kila kusanyiko la waaminio, na wakiwa wameomba na kufunga, waliwakabidhi kwa Bwana, ambaye wao walimwamini.
24 And having passed through Pisidia, they came to Pamphylia,
Kisha walipita katika Pisidia, walifika Pamfilia.
25 and having spoken the word in Perga, they went down to Attalia,
Wakati walipoongea maneno katika Perga, waliteremka kwenda Atalia.
26 and [from] there sailed to Antioch, from where they had been given by the grace of God for the work that they fulfilled;
Kutoka huko walipanda meli hadi Antiokia ambako walikuwa wamejitoa kwa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameikamilisha.
27 and having come and gathered the assembly together, they declared as many things as God did with them, and that He opened a door of faith to the nations;
Walipofika huko Antiokia, na kulikusanya kusanyiko la pamoja, wakatoa taarifa ya mambo ambayo Mungu amefanya kwao, na jinsi alivyowafungulia mlango wa imani kwa watu wa Mataifa.
28 and they abided there with the disciples [for] not a short time.
Walikaa kwa muda mrefu na wanafunzi.