< Acts 13 >
1 And there were certain in Antioch, in the assembly there, prophets and teachers: both Barnabas, and Simeon who is called Niger, and Lucius the Cyrenian, Manaen also—Herod the tetrarch’s foster-brother—and Saul;
Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
2 and in their ministering to the LORD and fasting, the Holy Spirit said, “Separate to Me both Barnabas and Saul to the work to which I have called them,”
Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: “Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia.”
3 then having fasted, and having prayed, and having laid the hands on them, they sent [them] away.
Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
4 These, indeed, then, having been sent forth by the Holy Spirit, went down to Seleucia, and from there they sailed to Cyprus,
Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
5 and having come to Salamis, they declared the word of God in the synagogues of the Jews, and they also had John [as] a servant;
Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
6 and having gone through the island to Paphos, they found a certain magus, a false prophet, a Jew, whose name [is] Bar-Jesus;
Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
7 who was with the proconsul Sergius Paulus, an intelligent man; this one having called for Barnabas and Saul, desired to hear the word of God,
Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
8 and there withstood them Elymas the magus—for so is his name interpreted—seeking to pervert the proconsul from the faith.
Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
9 And Saul—who also [is] Paul—having been filled with the Holy Spirit, and having looked steadfastly on him,
Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
10 said, “O full of all guile, and all recklessness, son of a devil, enemy of all righteousness, will you not cease perverting the right ways of the LORD?
akasema, “Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
11 And now, behold, a hand of the LORD [is] on you, and you will be blind, not seeing the sun for a season”; and instantly there fell on him a mist and darkness, and he, going around, was seeking some to lead [him] by the hand;
Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo.” Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
12 then the proconsul having seen what has come to pass, believed, being astonished at the teaching of the LORD.
Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
13 And those around Paul having set sail from Paphos, came to Perga of Pamphylia, and John having departed from them, turned back to Jerusalem,
Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
14 and they having gone through from Perga, came to Antioch of Pisidia, and having gone into the synagogue on the day of the Sabbaths, they sat down,
Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
15 and after the reading of the Law and of the Prophets, the chief men of the synagogue sent to them, saying, “Men, brothers, if there be a word in you of exhortation to the people—say on.”
Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: “Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni.”
16 And Paul having risen, and having beckoned with the hand, said, “Men, Israelites, and those fearing God, listen:
Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: “Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
17 the God of this people Israel chose our fathers, and He exalted the people in their sojourning in the land of Egypt, and He brought them out of it with a high arm;
Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
18 and about a period of forty years He endured their conduct in the wilderness,
Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
19 and having destroyed seven nations in the land of Canaan, He divided their land to them by lot.
Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
20 And after these things, about four hundred and fifty years, He gave judges—until Samuel the prophet;
Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
21 and thereafter they asked for a king, and God gave to them Saul, son of Kish, a man of the tribe of Benjamin, for forty years;
Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
22 and having removed him, He raised up to them David for king, to whom also having testified, He said, I found David, the [son] of Jesse, a man according to My heart, who will do all My will.
Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
23 Of this one’s seed, God, according to promise, raised to Israel a Savior—Jesus,
Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
24 John having first preached, before His coming, an immersion of conversion to all the people of Israel;
Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
25 and as John was fulfilling the course, he said, Whom do you suppose I am? I am not [He], but behold, He comes after me, of whom I am not worthy to loose the sandal of [His] feet.
Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
26 Men, brothers, sons of the race of Abraham, and those among you fearing God, to you was the word of this salvation sent,
“Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27 for those dwelling in Jerusalem, and their chiefs, having not known this One, also the voices of the Prophets, which are being read every Sabbath—having judged [Him]—fulfilled,
Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
28 and having found no cause of death, they asked of Pilate that He should be slain,
Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
29 and when they fulfilled all the things written about Him, having taken [Him] down from the tree, they laid Him in a tomb;
Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
30 and God raised Him out of the dead,
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 and He was seen for many days of those who came up with Him from Galilee to Jerusalem, who are His witnesses to the people.
Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
32 And we proclaim good news to you—that the promise made to the fathers,
Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
33 God has completed this in full to us their children, having raised up Jesus, as also in the second Psalm it has been written: You are My Son—I have begotten You today.
Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
34 And that He raised Him up out of the dead, to no longer return to corruption, He has said this: I will give to You the holy [blessings] of David [that are] faithful;
Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
35 for what reason He also says in another [place]: You will not give Your Holy One to see corruption;
Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
36 for David, indeed, having served his own generation by the will of God, fell asleep, and was added to his fathers, and saw corruption,
Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37 but He whom God raised up, did not see corruption.
Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38 Let it therefore be known to you, men, brothers, that the forgiveness of sins is declared to you through this One,
Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
39 and from all things in the Law of Moses from which you were not able to be declared righteous, everyone who is believing in this One is declared righteous;
na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
40 see, therefore, it may not come on you that has been spoken in the Prophets:
Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41 See, you despisers, and wonder, and perish, because I work a work in your days, a work in which you may not believe, though anyone may declare [it] to you.”
Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.”
42 And having gone forth out of the synagogue of the Jews, the nations were calling on [them] that on the next Sabbath these sayings may be spoken to them,
Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
43 and the synagogue having been dismissed, many of the Jews and of the devout proselytes followed Paul and Barnabas, who, speaking to them, were persuading them to remain in the grace of God.
Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
44 And on the coming Sabbath, almost all the city was gathered together to hear the word of God,
Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
45 and the Jews having seen the multitudes, were filled with zeal, and contradicted the things spoken by Paul—contradicting and slandering.
Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
46 And speaking boldly, Paul and Barnabas said, “It was necessary that the word of God be first spoken to you, and seeing you thrust it away, and do not judge yourselves worthy of the continuous life, behold, we turn to the nations; (aiōnios )
Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios )
47 for so the LORD has commanded us: I have set you for a light of nations—for your being for salvation to the end of the earth.”
Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.”
48 And the nations hearing were glad, and were glorifying the word of the LORD, and believed—as many as were appointed to continuous life; (aiōnios )
Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios )
49 and the word of the LORD was spread abroad through all the region.
Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
50 And the Jews stirred up the devout and honorable women, and the first men of the city, and raised persecution against Paul and Barnabas, and put them out from their borders;
Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
51 and having shaken off the dust of their feet against them, they came to Iconium,
Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
52 and the disciples were filled with joy and the Holy Spirit.
Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.