< 2 Timothy 3 >

1 And know this, that in the last days there will come perilous times,
Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu.
2 for men will be lovers of themselves, lovers of money, boasters, proud, slanderous, disobedient to parents, unthankful, unkind,
watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu;
3 without natural affection, implacable, false accusers, without control, barbaric, not lovers of those who are good,
watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema;
4 traitors, reckless, lofty, lovers of pleasure more than lovers of God,
watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
5 having a form of piety, but having denied its power; and be turning away from these,
Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.
6 for of these there are those coming into the houses and leading captive the weak women, loaded with sins, led away with manifold desires,
Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina;
7 always learning, and never able to come to a knowledge of truth,
wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli.
8 and even as Jannes and Jambres stood against Moses, so these also stand against the truth, men corrupted in mind, disapproved concerning the faith;
Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose.
9 but they will not advance any further, for their folly will be evident to all, as theirs also became.
Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre.
10 And you have followed after my teaching, manner of life, purpose, faith, long-suffering, love, endurance,
Wewe lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu,
11 the persecutions, the afflictions, that befell me in Antioch, in Iconium, in Lystra; what persecutions I endured! And the LORD delivered me out of all.
udhalimu na mateso yangu. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.
12 And all who will to live piously in Christ Jesus will also be persecuted,
Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe.
13 and evil men and impostors will advance to the worse, leading astray and being led astray.
Watu waovu na wadanyanyifu watazidi kuwa waovu zaidi na zaidi kwa kuwadanganya wengine na kudanganyika wao wenyewe.
14 And you—remain in the things which you learned and were entrusted with, having known from whom you learned,
Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa, ukaukubali kabisa. Unawajua wale waliokuwa walimu wako.
15 and because you have known the Holy Writings from infancy, which are able to make you wise—to salvation, through faith that [is] in Christ Jesus.
Unakumbuka kwamba tangu utoto wako umeyajua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu.
16 Every Writing [is] God-breathed, and profitable for teaching, for conviction, for correction, for instruction that [is] in righteousness,
Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
17 that the man of God may be fitted—having been completed for every good work.
ili mtu anayemtumikia Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila tendo jema.

< 2 Timothy 3 >