< 2 Samuel 6 >
1 And again David gathered every chosen one in Israel—thirty thousand,
Basi kwa mara nyingine Daudi akawakusanya wateuli wa Israeli, elfu thelathini.
2 and David rises and goes, and all the people who [are] with him, from Ba‘ale-Judah, to bring up the Ark of God from there, whose name has been called—the Name of YHWH of Hosts, inhabiting the cherubim—on it.
Daudi akainuka na akaenda na watu wake wote waliokuwa pamoja naye kutoka Baala ulioko Yuda ili alilete sanduku la Mungu, liitwalo kwa jina la Yahwe wa majeshi, akaaye juu ya makerubi.
3 And they cause the Ark of God to ride on a new cart, and lift it up from the house of Abinadab, which [is] in the height, and Uzzah and Ahio sons of Abinadab are leading the new cart;
Wakaliweka sanduku la Mungu juu ya mkokoteni mpya. Wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wanawe, wakauongoza mkokoteni.
4 and they lift it up from the house of Abinadab, which [is] in the height, with the Ark of God, and Ahio is going before the Ark,
Wakautoa mkokoteni na sanduku la Mungu juu yake nyumbani mwa Abinadabu juu ya kilima. Ahio alikuwa ametangulia mbele ya sanduku.
5 and David and all the house of Israel are playing before YHWH, with all kinds of [instruments] of fir-wood, even with harps, and with psalteries, and with timbrels, and with horns, and with cymbals.
Kisha Daudi na nyumba yote ya Israeli wakaanza kucheza mbele ya Yahwe, wakishangilia kwa vyombo vya mziki, vinubi, vinanda, matari, kayamba na matowazi.
6 And they come to the threshing-floor of Nachon, and Uzzah puts forth [his hand] to the Ark of God, and lays hold on it, for they released the oxen;
Hata walipofika katika shinikizo la Nasoni, wale ng'ombe wakakwama, Uza akanyosha mkono wake na kulikumbatia sanduku la Mungu, naye akalishikilia.
7 and the anger of YHWH burns against Uzzah, and God strikes him there for the error, and he dies there by the Ark of God.
Kisha asira ya Yahweh ikawaka dhidi ya Uza. Mungu akampiga kwa ajili ya dhambi yake. Uza akafa pale pale kando ya sandaku la Mungu.
8 And it is displeasing to David, because that YHWH has broken forth a breach on Uzzah, and [one] calls that place Perez-Uzzah to this day;
Daudi akakasirika kwa kuwa Yahwe alimpiga Uza, naye akapaita mahali pale Peresi Uza. Eneo hilo linaitwa Peres Uza hata leo.
9 and David fears YHWH on that day and says, “How does the Ark of YHWH come to me?”
Daudi akamwogopa Yahweh siku hiyo. Akasema, “Sanduku la Yahwe lawezaje kuja kwangu?”
10 And David has not been willing to turn aside the Ark of YHWH to himself, to the City of David, and David turns it aside to the house of Obed-Edom the Gittite,
Hivyo Daudi hakuwatayari tena kulichukua sanduku la Yahwe katika mji wa Daudi. Badala yake, akaliweka kando katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti.
11 and the Ark of YHWH inhabits the house of Obed-Edom the Gittite [for] three months, and YHWH blesses Obed-Edom and all his house.
Sanduku la Yahwe likakaa katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti kwa miezi mitatu. Kwa hiyo Yahwe akambariki yeye na nyumba yake yote.
12 And it is declared to King David, saying, “YHWH has blessed the house of Obed-Edom, and all that he has, because of the Ark of God”; and David goes and brings up the Ark of God from the house of Obed-Edom to the City of David with joy.
Kisha mfalme Daudi akaambiwa, “Yahwe ameibariki nyumba ya Obedi Edomu na kila kitu alichonacho kwa sababu ya sanduku la Mungu.” Hivyo Daudi akaenda na kulipandisha sanduku la Mungu kutoka katika nyumba ya Obedi Edomu hadi mji wa Daudi kwa furaha.
13 And it comes to pass, when those carrying the Ark of YHWH have stepped six steps, that he sacrifices an ox and a fatling.
Ikawa waliolibeba sanduku la Yahwe walipochukua hatua sita, akatoa sadaka ng'ombe na ndama aliyenona.
14 And David is dancing with all [his] strength before YHWH, and David is girded with a linen ephod,
Daudi akacheza mbele ya Yahwe kwa nguvu zake zote; alikuwa amevaa naivera ya kitani pekee.
15 and David and all the house of Israel are bringing up the Ark of YHWH with shouting, and with the voice of a horn,
Hivyo Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalipandisha sanduku la Yahwe kwa vifijo na sauti za tarumbeta.
16 and it has come to pass, the Ark of YHWH has come into the City of David, and Michal daughter of Saul has looked through the window and sees King David moving and dancing before YHWH, and she despises him in her heart.
Hata ikawa sanduku la Yahwe lilipofika mjini mwa Daudi, Mikali, binti Sauli, alichungulia dirishani. Akamwona mfalme Daudi akiruka na kucheza mbele ya Yahwe. Akamdharau moyoni mwake.
17 And they bring in the Ark of YHWH, and set it up in its place, in the midst of the tent which David has spread out for it, and David causes burnt-offerings and peace-offerings to ascend before YHWH.
Wakaliingiza sanduku la Yahwe na kuliweka mahali pake, katikati ya hema ambayo Daudi alikuwa ameliwekea. Kisha Daudi akatoa sadaka ya kuteketezwa na matoleo ya amani mbele za Yahwe.
18 And David finishes from causing the burnt-offering and the peace-offerings to ascend, and blesses the people in the Name of YHWH of Hosts,
Ikawa Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Yahwe wa majeshi.
19 and he apportions to all the people, to all the multitude of Israel, from man and to woman, to each, one cake of bread, and one eshpar, and one ashisha, and all the people go, each to his house.
Kisha akawagawia watu wote, umati wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kipande cha mkate, nyama na keki ya zabibu. Kisha watu wote wakaondoka; kila mmoja akarudi kwake.
20 And David turns back to bless his house, and Michal daughter of Saul goes out to meet David and says, “How honorable was the king of Israel today, who was uncovered today before the eyes of the handmaids of his servants, as one of the vain ones is openly uncovered!”
Kisha Daudi akarudi ili aibariki familia yake. Mikali, binti Sauli, akatoka ili akutane na Daudi naye akasema, “Jinsi gani mtukufu mfalme wa Israeli alivyokuwa leo, aliyejiacha uchi mbele ya macho ya vijakazi miongoni mwa watumishi wake, kama mmoja wa wapumbavu ambaye bila aibu hujifunua yeye mwenyewe!”
21 And David says to Michal, “Before YHWH, who fixed on me above your father, and above all his house, to appoint me leader over the people of YHWH, and over Israel—indeed, I played before YHWH;
Daudi akamjibu Mikali, “Nilifanya hivyo mbele ya Yahwe, aliyenichagua juu ya baba yako na juu ya familia yake yote, aliyeniweka kuwa kiongozi juu ya watu wa Yahwe, juu ya Israeli. Mbele ya Yahwe nitafurahi!
22 and I have been more vile than this, and have been low in my eyes, and with the handmaids whom you have spoken of, I am honored with them.”
Nitakuwa nisiye na heshima hata zaidi ya hapa, na nitajishusha mbele za macho yangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliowasema, nitaheshimiwa.”
23 As for Michal daughter of Saul, she had no child until the day of her death.
Hivyo Mikali, binti Sauli, hakuwa na watato hata alipokufa.