< 2 Samuel 20 >

1 And there happened to be a man of worthlessness there, and his name [is] Sheba, son of Bichri, a Benjamite, and he blows with a horn and says, “We have no portion in David, and we have no inheritance in the son of Jesse; each [goes] to his tents, O Israel.”
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 And every man of Israel goes up from after David, after Sheba son of Bichri, and the men of Judah have cleaved to their king, from the Jordan even to Jerusalem.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 And David comes to his house at Jerusalem. And the king takes the ten women-concubines whom he had left to keep the house, and puts them in a house of ward and sustains them, and he has not gone in to them, and they are shut up to the day of their death, living in widowhood.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 And the king says to Amasa, “Call the men of Judah for me [within] three days, and you, stand here,”
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 and Amasa goes to call Judah, and tarries beyond the appointed time that he had appointed him;
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 and David says to Abishai, “Now Sheba son of Bichri does evil to us more than Absalom; you, take the servants of your lord, and pursue after him, lest he has found fortified cities for himself, and delivered himself [from] our eye.”
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 And the men of Joab go out after him, and the Cherethite, and the Pelethite, and all the mighty men, and they go out from Jerusalem to pursue after Sheba son of Bichri;
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 they [are] near the great stone that [is] in Gibeon, and Amasa has gone before them, and Joab [is] girded; he has put his long robe on him, and on it a girdle—a sword [is] fastened on his loins in its sheath; and he has gone out, and it falls.
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 And Joab says to Amasa, “Are you [in] peace, my brother?” And the right hand of Joab lays hold on the beard of Amasa to give a kiss to him;
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 and Amasa has not been watchful of the sword that [is] in the hand of Joab, and he strikes him with it to the fifth [rib], and sheds out his bowels to the earth, and he has not repeated [it] to him, and he dies; and Joab and his brother Abishai have pursued after Sheba son of Bichri.
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 And a man has stood by him, of the young men of Joab, and says, “He who has delight in Joab, and he who [is] for David—after Joab!”
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 And Amasa is rolling himself in blood, in the midst of the highway, and the man sees that all the people have stood still, and he brings around Amasa out of the highway to the field, and casts a garment over him when he has seen that everyone who has come by him has stood still.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 When he has been removed out of the highway, every man has passed on after Joab, to pursue after Sheba son of Bichri.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 And he passes over through all the tribes of Israel to Abel, and to Beth-Maachah, and to all the Berites, and they are assembled, and also go in after him,
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 and they go in and lay siege against him, in Abel of Beth-Maachah, and cast up a mound against the city, and it stands in a trench, and all the people who are [are] with Joab are destroying, to cause the wall to fall.
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 And a wise woman calls out of the city, “Hear! Hear! Please say to Joab, Come near here, and I speak to you.”
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 And he comes near to her, and the woman says, “Are you Joab?” And he says, “I [am].” And she says to him, “Hear the words of your handmaid”; and he says, “I am hearing.”
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 And she speaks, saying, “They spoke often in former times, saying, Let them diligently inquire at Abel, and so they finished.
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 I [am] of the peaceable, faithful ones of Israel; you are seeking to destroy a city and mother in Israel; why do you swallow up the inheritance of YHWH?”
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 And Joab answers and says, “Far be it—far be it from me; I do not swallow up nor destroy.
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 The matter [is] not so; for a man of the hill-country of Ephraim—Sheba son of Bichri [is] his name—has lifted up his hand against the king, against David; give him up by himself, and I go away from the city.” And the woman says to Joab, “Behold, his head is cast to you over the wall.”
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 And the woman comes to all the people in her wisdom, and they cut off the head of Sheba son of Bichri, and cast [it] to Joab, and he blows with a horn, and they are scattered from the city, each [goes] to his tents, and Joab has turned back to Jerusalem to the king.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 And Joab [is] over all the host of Israel, and Benaiah son of Jehoiada [is] over the Cherethite, and over the Pelethite,
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 and Adoram [is] over the tribute, and Jehoshaphat son of Ahilud [is] the remembrancer,
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 and Sheva [is] scribe, and Zadok and Abiathar [are] priests,
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 and also, Ira the Jairite has been minister to David.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.

< 2 Samuel 20 >