< 2 Corinthians 9 >

1 For indeed, concerning the ministry that [is] for the holy ones, it is superfluous for me to write to you,
Hakuna haja yangu kuwaandikia kuhusu huduma hii itolewayo kwa ajili ya watakatifu.
2 for I have known your readiness of mind, which in your behalf I boast of to Macedonians, that Achaia has been prepared a year ago, and your zeal stirred up the greater part,
Kwa kuwa ninajua mlivyo na shauku ya kusaidia, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili ya jambo hilo kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana na shauku yenu imewachochea wengi wao katika kutoa.
3 and I sent the brothers, that our boasting on your behalf may not be made vain in this respect; that, according as I said, you may be ready,
Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusiwe maneno matupu, bali mpate kuwa tayari kama nilivyosema mngekuwa tayari.
4 lest if Macedonians may come with me, and find you unprepared, we may be put to shame (that we do not say—you) in this same confidence of boasting.
Kwa maana kama nikija na Mmakedonia yeyote na kuwakuta hamjawa tayari, tutaona aibu kusema chochote juu yenu katika matoleo.
5 Therefore I thought [it] necessary to exhort the brothers, that they may go before to you, and may make up before your formerly announced blessing, that this be ready, as a blessing, and not as covetousness.
Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kwenu kabla yangu, wafanye mipango ya hayo matoleo ya ukarimu mliyokuwa mmeahidi, ili yawe tayari kama matoleo ya hiari wala si kama ya kutozwa kwa nguvu.
6 And [remember] this: he who is sowing sparingly, will also reap sparingly; and he who is sowing in blessings, will also reap in blessings;
Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye kwa uchache pia atavuna kwa uchache, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.
7 each one, according as he purposes in heart, not out of sorrow or out of necessity, for God loves a cheerful giver,
Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa uchoyo au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo mkunjufu.
8 and God [is] able to cause all grace to abound to you, that in everything always having all sufficiency, you may abound to every good work,
Naye Mungu aweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili katika mambo yote kila wakati, mwe na kila kitu mnachohitaji, ili mweze kushiriki kwa wingi katika kila kazi njema.
9 according as it has been written: “He dispersed abroad, He gave to the poor, His righteousness remains throughout the age,” (aiōn g165)
Kama ilivyoandikwa: “Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele.” (aiōn g165)
10 and may He who is supplying seed to the sower, and bread for food, supply and multiply your seed sown, and increase the fruits of your righteousness,
Yeye ampaye mpanzi mbegu kwa ajili ya kupanda na mkate kuwa chakula, atawapa na kuzizidisha mbegu zenu za kupanda na kuongeza mavuno ya haki yenu.
11 being enriched to all liberality in everything, which works thanksgiving through us to God,
Mtatajirishwa kwa kila namna ili mpate kuwa wakarimu kila wakati, na kupitia kwetu, ukarimu wenu utamletea Mungu shukrani.
12 because the ministry of this service not only is supplying the wants of the holy ones, but is also abounding through many thanksgivings to God,
Huduma hii mnayofanya si tu kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watakatifu, bali huzidi sana kwa shukrani nyingi apewazo Mungu.
13 through the proof of this ministry glorifying God for the subjection of your confession to the good news of the Christ, and [for] the liberality of the fellowship to them and to all,
Kwa sababu ya huduma ambayo mmejithibitisha wenyewe, watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utiifu ufuatanao na ukiri wenu wa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wenu wa kushiriki pamoja nao na pia wengine wote.
14 and by their supplication in your behalf, longing after you because of the exceeding grace of God on you;
Nao katika maombi yao kwenu mioyo yao itawaonea shauku kwa sababu ya neema ipitayo kiasi mliyopewa na Mungu.
15 thanks also to God for His unspeakable gift!
Ashukuriwe Mungu kwa karama yake isiyoelezeka.

< 2 Corinthians 9 >