< 2 Corinthians 8 >

1 And we make known to you, brothers, the grace of God, that has been given in the assemblies of Macedonia,
Tunawataka ninyi mjue, kaka na dada, kuhusu neema ya Mungu ambayo imetolewa kwa makanisa ya Makedonia.
2 because in much trial of tribulation the abundance of their joy, and their deep poverty, abounded to the riches of their liberality;
Wakati wa jaribu kubwa la mateso, wingi wa furaha yao na ongezeko la umaskini wao umezaa utjiri mkubwa wa ukarimu.
3 because, according to [their] power, I testify, and above [their] power, they were willing of themselves,
Kwa maana nashuhudia kwamba walitoa kwa kadiri ya walivyoweza, na hata zaidi ya walivyoweza.
4 with much plea calling on us to receive the favor and the fellowship of the ministry to the holy ones,
Na kwa hiari yao wenyewe kwa kutusihi kwingi, walituomba kwa ajili ya kushiriki katika huduma hii kwa waumini.
5 and not according as we expected, but they gave themselves first to the LORD, and to us, through the will of God,
Hii haikutokea kama tulivyokuwa tunatarajia. Badala yake, kwanza walijitoa wao wenyewe kwa Bwana. Kisha wakajitoa wao wenyewe kwetu kwa mapenzi ya Mungu.
6 so that we exhorted Titus, that, according as he began before, so also he may also finish this favor to you,
Hivyo tulimsihi Tito, aliyekuwa tayari ameanzisha kazi hii, kuleta katika utimilifu tendo hili la ukarimu juu yenu.
7 but even as in everything you abound, in faith, and word, and knowledge, and all diligence, and in your love to us, that also in this grace you may abound;
Lakini ninyi mna wingi katika kila kitu- katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika bidii, na katika upendo wenu kwa ajili yetu. Hivyo hakikisheni kwamba ninyi mnakuwa na wingi pia katika tendo hili la ukarimu.
8 I do not speak according to command, but because of the diligence of others, and proving the genuineness of your love,
Nasema hili si kama amri. Badala yake, nasema hili ili kupima uhalisi wa upendo wenu kwa kuulinganisha na shauku ya watu wengine.
9 for you know the grace of our Lord Jesus Christ, that because of you He became poor—being rich, that you may become rich by that poverty.
Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo. Hata kama alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikuwa maskini. Ili kwamba kupitia umaskini wake mweze kuwa tajiri.
10 And I give an opinion in this: for this [is] expedient to you, who not only to do, but also to will, began before—a year ago,
Katika jambo hili nitawapa ushauri ambao utawasaidia. Mwaka mmoja uliopita, hamkuanza tuu kufanya jambo. Lakini mlitamani kulifanya.
11 and now also finish doing [it], that even as [there is] the readiness of the will, so also the finishing, out of that which you have,
Sasa likamilisheni. Kama tu kulivyokuwa na shauku na nia ya kulifanya, kisha, je, mngeweza pia kulileta katika ukamilifu, kwa kadri ya mnavyoweza.
12 for if the willing mind is present, it is well-accepted according to that which anyone may have, not according to that which he does not have;
Kwa kuwa mnashauku ya kufanya tendo hili, ni jambo zuri na linakubalika. Lazima lisimame juu ya kile alichonacho mtu, siyo juu ya asichokuwa nacho mtu.
13 for I do not speak that for others [to be] released, and you pressured,
Kwa kuwa kazi hii siyo kwa ajili kwamba wengine waweze kupata nafuu na ninyi mweze kulemewa. Badala yake, kuwe na usawa.
14 but by equality, at the present time your abundance—for their want, that also their abundance may be for your want, that there may be equality,
Wingi wenu wa wakati wa sasa utasaidia kwa kile wanachohitaji. Hii ni hivyo pia ili kwamba wingi wao uweze kusaidia mahitaji yenu, na kwamba kuwe na usawa.
15 according as it has been written: “He who [gathered] much, had nothing over; and he who [gathered] little, had no lack.”
Hii ni kama ilivyoandikwa; “Yeye aliye na vingi hakuwa na kitu chochote kilichobaki na yeye aliyekuwa na kidogo hakuwa na uhitaji wowote.”
16 And thanks to God, who is putting the same diligence for you in the heart of Titus,
Lakini ashukuriwe Mungu, aliyeweka ndani ya moyo wa Tito moyo uleule wa bidii ya kujali ambyo ninayo kwa ajili yenu.
17 because he indeed accepted the exhortation, and being more diligent, he went forth to you of his own accord,
Kwa kuwa si tu alipokea maombi yetu, bali pia alikuwa na bidii kuhusiana na maombi hayo. Alikuja kwenu kwa hiari yake mwenyewe.
18 and we sent with him the brother, whose praise in the good news [is] through all the assemblies,
Tumemtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa miongoni mwa makanisa kwa ajili ya kazi yake katika kutangaza injili.
19 and not only so, but who was also appointed by vote by the assemblies, our fellow-traveler, with this favor that is ministered by us, to the glory of the same Lord, and your willing mind;
Si hivi tu, lakini pia alichaguliwa na makanisa kusafiri nasisi katika kulibeba sehemu mbalimbali tendo hili la ukarimu. Hii ni kwa utukufu wa Bwana mwenyewe na kwa shauku yetu ya kusaidia.
20 avoiding this, lest anyone may blame us in this abundance that is ministered by us,
Tunaepuka uwezekano kwamba yeyote napaswa kulalamika kuhusiana na sisi kuhusiana na ukarimu huu ambao tunaubeba.
21 providing right things, not only before the LORD, but also before men;
Tunachukua uangalifu kufanya kilicho cha heshima, sio tu mbele za Bwana, lakini pia mbele za watu.
22 and we sent our brother with them, whom we proved being diligent many times in many things, and now much more diligent, by the great confidence that is toward you,
Pia tunamtuma ndugu mwingine pamoja nao. Tumempima mara nyingi, na tumemwona ni mwenye shauku for ajili ya kazi nyingi. Hata sasa ana bidii zaidi kwa sababu ya ujasiri mkubwa alionao ndani yenu.
23 whether—about Titus—my partner and fellow-worker toward you, whether—our brothers, apostles of assemblies—glory of Christ;
Kwa habari ya Tito, yeye ni mshirika mwenza wangu na mtendakazi mwenzangu kwa ajili yenu. Kama kwa ndugu zetu, wanatumwa na makanisa. Ni waheshima kwa Kristo.
24 the showing therefore of your love, and of our boasting on your behalf, show to them, even in the face of the assemblies.
Hivyo, waonesheni upendo wenu, na muoneshe kwa makanisa sababu ya majivuno yetu kwa ajili yenu.

< 2 Corinthians 8 >