< 2 Chronicles 8 >
1 And it comes to pass at the end of twenty years that Solomon has built the house of YHWH and his own house.
Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
2 As for the cities that Huram has given to Solomon, Solomon has built them, and he causes the sons of Israel to dwell there.
Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
3 And Solomon goes to Hamath-Zobah, and lays hold on it;
Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
4 and he builds Tadmor in the wilderness, and all the cities of store that he has built in Hamath.
Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
5 And he builds Beth-Horon the upper, and Beth-Horon the lower—cities of defense, with walls, double gates, and bar—
Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
6 and Ba‘alath, and all the cities of store that Solomon had, and all the cities of the chariot, and the cities of the horsemen, and all the desire of Solomon that he desired to build in Jerusalem, and in Lebanon, and in all the land of his dominion.
Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
7 All the people who are left of the Hittite, and the Amorite, and the Perizzite, and the Hivite, and the Jebusite, who are not of Israel—
Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
8 of their sons who have been left after them in the land, whom the sons of Israel did not consume—Solomon lifts up a tribute to this day.
yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
9 And Solomon has made none of the sons of Israel servants for his work, but they [are] men of war, and heads of his captains, and heads of his charioteers, and of his horsemen;
Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
10 and these [are] heads of the officers whom King Solomon has, two hundred and fifty who are rulers among the people.
Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
11 And Solomon has brought up the daughter of Pharaoh from the City of David to the house that he built for her, for he said, “My wife does not dwell in the house of David king of Israel, for they are holy to whom the Ark of YHWH has come.”
Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
12 Then Solomon has caused burnt-offerings to ascend to YHWH on the altar of YHWH that he built before the porch,
Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
13 even by the matter of a day in its day, to cause to ascend according to the command of Moses, on Sabbaths, and on new moons, and on appointed times, three times in a year—in the Celebration of Unleavened Things, and in the Celebration of Weeks, and in the Celebration of Shelters.
kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
14 And he establishes, according to the ordinance of his father David, the divisions of the priests over their service, and of the Levites over their charges, to praise and to minister before the priests, according to the matter of a day in its day, and the gatekeepers in their divisions at every gate, for so [is] the command of David the man of God.
Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
15 And they have not turned aside [from] the command of the king concerning the priests and the Levites, in reference to any matter, and to the treasures.
Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
16 And all the work of Solomon is prepared until the day of the foundation of the house of YHWH, and until its completion; the house of YHWH is perfect.
Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
17 Then Solomon has gone to Ezion-Geber, and to Elath, on the border of the sea, in the land of Edom;
Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
18 and Huram sends to him, by the hand of his servants, ships and servants knowing the sea, and they go with servants of Solomon to Ophir, and take four hundred and fifty talents of gold from there, and bring it to King Solomon.
Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.