< 2 Chronicles 6 >
1 Then Solomon said, “YHWH said [He would] dwell in thick darkness,
Kisha Selemani akasema, “Yahwe alisema kwamba ataishi katika giza nene,
2 and I have built a house of habitation for You, and a fixed place for Your dwelling for all ages.”
lakini nimekujengea makao makuu, sehemu kwa ajili yako ya kuishi milele.”
3 And the king turns around his face, and blesses the whole assembly of Israel, and the whole assembly of Israel is standing,
Kisha mfaalme akageuka nyuma na kuwabariki kusanyiko lote la Israeli, wakati kusanyiko lote la Israeli walikuwa wamesimama.
4 and he says, “Blessed [is] YHWH, God of Israel, who has spoken with His mouth with my father David, and with His hands has fulfilled [it], saying,
Akasema, “Yahwe, Mungu wa Israeli, usifiwe, uliyesema na Daudi baba yangu, na ametimiza kwa mikono yake mwenyewe, akisema.
5 From the day that I brought out My people from the land of Egypt, I have not fixed on a city out of any of the tribes of Israel to build a house for my name being there, and I have not fixed on a man to be leader over My people Israel;
'Tangu siku nilipowaleta watu wanagu nje ya nchi ya Misiri, sikuchaagua mji wowote nje ya makabaila yote ya Israeli ambamo nyumba ingejengwa, ili jina lanagu liwe humo. Wala sikuchagua mtu yeyote kuwa mfalme juu ya watu wangu Israeli.
6 and I fix on Jerusalem for My Name being there, and I fix on David to be over My people Israel.
Aidha, nimechagua Yeruselemu, ili kwamba jina langu liwe humo, na nimemchagua Daudi kuwa juu ya watu wanagu Israeli. '
7 And it is with the heart of my father David to build a house for the Name of YHWH God of Israel,
Sasa ilikuwa ndani ya moyo wa Daudi baba yangu, kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yahwe, Mungu wa Israeli.
8 and YHWH says to my father David, Because that it has been with your heart to build a house for My Name, you have done well that it has been with your heart,
Lakini Yahwe alisema kwa Daudi Baba yanagu. 'Kwmba ilikuwa ndani ya moyo wako kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, ulifanya vizuri kwa hili kuliweka moyono mwako.
9 but you do not build the house, for your son who comes forth out from your loins, he builds the house for My Name.
Aidha, hutaijenga ile nyumba, badala yake, mwanao, mmoja atakayetoka kwenye viuno vyako, ataijenga nyumba kwa ajili ya jina langu.'
10 And YHWH establishes His word that He spoke, and I rise up in the stead of my father David, and sit on the throne of Israel, as YHWH spoke, and I build the house for the Name of YHWH, God of Israel,
Yahwe ameyatimiza maneno aliyokuwa amesema, kwa maana nimeiinua sehemu ya Daudi baba yangu, na ninkaa juu ya kiti cha enzi cha Israeli, kama alivyoahidi Yahwe. Nimeijenga nyumba kwa ajii ya jina la Yahwe, Mungu wa Israeli.
11 and I place the Ark there, where the covenant of YHWH [is] that He made with the sons of Israel.”
Nimeliweka humo sanduku, amabamo kuna agano la Yahwe, alilofanya na watu wa Israeli.”
12 And he stands before the altar of YHWH, in front of all the assembly of Israel, and spreads out his hand—
Selemani akasimama mbele ya madhabahu ya Yahwe mbele za kusanyiko lote la Israeli, na akanyosha mikono yake.
13 for Solomon has made a scaffold of bronze, and puts it in the midst of the court, five cubits its length, and five cubits its breadth, and three cubits its height, and he stands on it, and kneels on his knees in front of all the assembly of Israel, and spreads forth his hands toward the heavens—
Kwa mana alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, lenye urefu wa mikono mitano, upana wa mikono mitano, urefu wake kwenda juu mikono mitatu. Alikuwa ameliweka katika ya uwanja. Akasimama juu yake na kupiga magoti mbele ya kusanyiko la Israeli, kisha akanyosha mikono yake kuzielekea mbingu.
14 and says, “O YHWH God of Israel, there is not like You a god in the heavens and in the earth, keeping the covenant and the kindness for Your servants who are walking before You with all their heart;
Akasema, “Yahwe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe katika mbingu, au juu ya dunia, ambaye anatunza agano na upendo imara na watumishi wako ambao hutembea mbele zako kwa moyo wao wote;
15 who has kept for Your servant, my father David, that which You spoke to him; indeed, You speak with Your mouth, and with Your hand have fulfilled [it], as at this day.
wewe uliyetimtimizia Daudi baba yanagu, uliyokuwa umemwahidi. Ndiyo, ulisema kwa kinywa chako na umetimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
16 And now, O YHWH, God of Israel, keep for Your servant, my father David, that which You spoke to him, saying, A man of yours is never cut off from before My face, sitting on the throne of Israel—only, if your sons watch their way to walk in My law, as you have walked before Me.
Sasa, Yahwe, Mungu wa Israeli, tunza ahadi uliyoahidi kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, uliposema, 'Hautashindwa kupata mtu mbele yangu wa kukaa juu ya kiti cha enzi cha Israeli, ikiwa tu uzao wako ni waangalifu kutembea katika sheria yangu, kama wewe ulivyotembea mbele zangu.
17 And now, O YHWH, God of Israel, let Your word be steadfast that You have spoken to Your servant, to David.
Sasa, Mungu wa Israeli, ninaomba kwamba ahadi uliyofanya kwa mtumishi wako Daudi itakuwa kweli.
18 For is it true [that] God dwells with man on the earth? Behold, the heavens, and the heavens of the heavens, do not contain You, how much less this house that I have built?
Lakini kweli Mungu ataishi na wanadamu juu ya dunia? Angalia, dunia yoye na mbugu yenyewe haviwezi kukubeba -sembuse na hekalu hili nililojenga!
19 And You have turned to the prayer of Your servant, and to his supplication, O YHWH my God, to listen to the cry and to the prayer that Your servant is praying before You,
Nakusihi yaheshimu maombi haya ya mtumishi wako na ombi lake. Yahwe Mungu wangu; sikia kilio na amaombi ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako.
20 for Your eyes being open toward this house by day and by night, toward the place that You have said to put Your Name there, to listen to the prayer that Your servant prays toward this place.
Fumbua macho yako kuelekea hekaalu hili usiku na mchana, sehemu aambaayo uliahidi kuliweka jina lako. Nakuomba usikie maombi atakayoomba mtumishi wako kuelekea sehemu hii.
21 And You have listened to the supplications of Your servant, and of Your people Israel, that they pray toward this place, and You hear from the place of Your dwelling, from the heavens, and have listened, and forgiven.
Hivyo sikia maombi ya mtumishi na ya watu wako Israeli tunapoomba kuelekea sehemu hii. Ndiyo, sikia kutoka mahali unapoishi, kutoka mbinguni; na unaposikia, samehe.
22 If a man sins against his neighbor, and he has lifted up an oath on him to cause him to swear, and the oath has come in before Your altar in this house—
Kama mtu atamtenda dhambi jirani yake na ikampasa kuapa kiapo, na ikiwa atakuja na kuapa kiapo mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii,
23 then You hear from the heavens, and have done, and have judged Your servants, to give back to the wicked, to put his way on his head, and to declare righteous the righteous, to give to him according to his righteousness.
basi sikia kutoka mbinguni na kutend na ukawahukumu watumishi wako, ukamlipizie mwovu, ili kuyaleta matendo yake juu ya kichwa chake. Ukamtangaze mwenye haki kuwa hana hatia, ili kumlipa thawabu kwa ajili ya uaminifu wake.
24 And if Your people Israel is struck before an enemy because they sin against You, and they have turned back and confessed Your Name, and prayed and made supplication before You in this house—
Watu wako watakaposhindwa na adui kwa sababu wamekutenda dhambi, kama watageuka nyuma kwako, wakilikili jina lako, wakisali na kuomba msamaha mbele zako hekaluni—
25 then You hear from the heavens and have forgiven the sin of Your people Israel, and caused them to return to the ground that You have given to them, and to their fathers.
basi tafadhali sikia mbinguni na usamehe dhambi za watu wako Isaraeli; uwarudishe katika nchi uliyoitoa kwa ajili yao na baba zao.
26 In the heavens being restrained and there is no rain because they sin against You, and they have prayed toward this place and confessed Your Name, [and] they turn back from their sin because You afflict them—
Wakati mbingu zimefungwa na hakuna mvua kwa sababu watu wamekutenda dhambi—ikiwa wataomba kuelekea sehemu hii, wakilikili jina lako, na kuziacha dhambi zao utakapokuwa umewaadhibu—
27 then You hear in the heavens, and have forgiven the sin of Your servants, and of Your people Israel, because You direct them to the good way in which they walk, and have given rain on Your land that You have given to Your people for an inheritance.
basi sikia mbinguni na usamehe dhambi za watumishi wako na watu wako Israeli, utakapowaelekeza kwenye njia njema iwapasayo kutembea. Tuma mvua juu ya nchi yako, ambayo umewapa watu wako kama urithi.
28 Famine, when it is in the land, [and] pestilence, when it is [in the land], blasting and mildew, locust and caterpillar, when they are [in the land], when its enemies have distressed it in the land—its gates, any plague and any sickness;
Kama kuna njaa katika nchi, au kama kuna ugonjwa, tauni au ukungu, nzige au viwavijeshi, au kama adui wake wameyavamia malango ya mji katika nchi yao, au kwamba kuna pigo lolote au ugonjwa—
29 any prayer, any supplication that is for any man, and for all Your people Israel, when they each know his own plague, and his own pain, and he has spread out his hands toward this house—
na ikiwa sala na maombi yamefanywa na mtu au watu wako wote Israel—kila mmoja akilijua pigo na huzuni katika moyo wake akinyosha mikono yake kuelekea hekalu hili.
30 then You hear from the heavens, the settled place of Your dwelling, and have forgiven, and have given to each according to all his ways (because You know his heart, for You alone have known the heart of the sons of men),
Basi sikiliza mbinguni, sehemu ambayo unaishi; samehe, na umlipe kila mtu kwa njia zake zote; uhaujua moyo wake, kwa sababu wewe na ni wewe pekee unaijua mioyo ya wanadamu.
31 so that they fear You, to walk in Your ways, all the days that they are living on the face of the ground that You have given to our fathers.
Fanya hivyo ili kwamba wakuogope wewe, ili waweze kutembea katika katika njia zako siku zote ambazo wataishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
32 And also, to the stranger who is not of Your people Israel, and he has come from a far-off land for the sake of Your great Name, and Your strong hand, and Your outstretched arm, and they have come in and prayed toward this house—
Kwa mgeni ambaye siyo sehemu ya watu wako Israeli, lakini ambaye- kwa sababu ya ukuu wa jina lako, mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulionyoshwa- akija na kuomba kuelekea sehemu nyumba hii,
33 then You hear from the heavens, from the settled place of Your dwelling, and have done according to all that the stranger calls to You for, so that all the peoples of the earth know Your Name, so as to fear You, as Your people Israel, and to know that Your Name is called on this house that I have built.
basi sikiliza mbinguni, sehemu ambayo unaishi, na fanya yote ambayo mgeni atakuomba, ili kwamba watu wote wa dunia walijue jina lako na kukuogopa wewe, kama wafanyavyo watu wako Israeli, na kwamba waweze kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga inaitwa kwa jina lako.
34 When Your people go out to battle against its enemies in the way that You send them, and they have prayed to You [in] the way of this city that You have fixed on, and the house that I have built for Your Name—
Ikiwa kwamba watu wako wakaenda nje kupigana dhidi ya adui zao, kwa njia yoyote amabayo unaweza kuwatuma, na ikiwa kwamba wakaomba kwako kuelekea mji huu ambao umeuchagua, na kuelekea nyumba ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako.
35 then You have heard their prayer and their supplication from the heavens, and have maintained their cause.
Basi sikiliza maombi yao mbinguni, ombi lao, na uwasaidie.
36 When they sin against You—for there is not a man who does not sin—and You have been angry with them, and have given them before an enemy, and their captors have taken them captive to a land far off or near;
Kama wametenda dhambi dhidi yako—kwa kuwa hakuna asiye tenda dhambi—na ikiwa una hasira nao na kuwakabidhi kwa adui zao, ili kwamba adui wakawabeba na kuwachukua kama mateka kwa ajili ya nchi zao, iwe mbali au karibu.
37 and they have turned [it] back to their heart in the land to where they have been taken captive, and have turned back and made supplication to You in the land of their captivity, saying, We have sinned, we have done perversely, and have done wickedly;
Kisha wakatambua kuwa wako katika nchi ambako wamewekwa utumwani, na ikiwa watatubu na kutafuta msaada kwako katika utumwa wao. ikiwa watasema, 'Tumetenda kinyume na kutenda dhambi. Tumetenda kwa uovu,'
38 indeed, they have turned back to You with all their heart, and with all their soul, in the land of their captivity, to where they have taken them captive, and they have prayed [in] the way of their land that You have given to their fathers, and of the city that You have chosen, and of the house that I have built for Your Name—
ikiwa watarudi kwako kwa mioyo yao yote na kwa nia yao yote katika nchi ya utumwa wao, ambako walichuliwa kama mateka, na ikiwa wataomba kukabili nchi yao, uliyowapa babu zao, na kukabili mji ambao uliuchagua na kukabili nyumba ambayo niliijenga kwa ajili ya jina lako.
39 then You have heard from the heavens, from the settled place of Your dwelling, their prayer and their supplications, and have maintained their cause, and forgiven Your people who have sinned against You.
Basi sika kutoka mbinguni, mahali unapoishi, sikia kuomba kwao na maombi na wayaombayo, na uwasaidie shida zao. Wasamehe watu wako, ambao wamekutenda dhambi.
40 Now my God, I implore You, let Your eyes be open and Your ears attentive to the prayer of this place.
Sasa, Mungu wangu, ninakusihi, uyafungue macho yako, na masikio yako yasiskie maombi yatakayofanywa katika sehemu hii.
41 And now, rise, O YHWH God, to Your rest, You and the Ark of Your strength; Your priests, O YHWH God, are clothed with salvation, and Your saints rejoice in the goodness.
Sasa basi, amka, Yahwe Mungu, kwenye mahali pako pa kupumzikia, Wewe na sanduku la nguvu zako. Makuhani wako, Yahwe Mungu, wavikwe wokovu, na watakatifu wako wafurahi katika wema.
42 O YHWH God, do not turn back the face of Your anointed, be mindful of the kind acts of Your servant David.”
Yahwe Mungu, usiugeuze nyuma uso wa masihi wako. Yakumbuke matendo yako katika agano lako la ufalme kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako.