< 1 Timothy 1 >

1 Paul, an apostle of Jesus Christ, according to a command of God our Savior, and of the Lord Jesus Christ our hope,
Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
2 to Timotheus—genuine child in faith: Grace, kindness, peace, from God our Father and Christ Jesus our Lord!
nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
3 According as I exhorted you to remain in Ephesus—I going on to Macedonia—that you might charge certain [ones] not to teach any other thing,
Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
4 nor to give heed to fables and endless genealogies, that cause questions rather than [the] stewardship of God which [is] in faith.
Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
5 And the end of the charge is love out of a pure heart, and of a good conscience, and of unhypocritical faith,
Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
6 from which certain [men], having swerved, turned aside to vain discourse,
Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
7 willing to be teachers of law, not understanding either the things they say, nor concerning what they confidently assert,
Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
8 and we have known that the Law [is] good, if anyone may use it lawfully;
Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
9 having known this, that law is not set for a righteous man, but for lawless and insubordinate persons, ungodly and sinners, impious and profane, murderers of fathers and murderers of mothers, manslayers,
Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
10 whoremongers, homosexuals, enslavers, liars, perjured persons, and if there be any other thing that is adverse to sound doctrine,
sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
11 according to the good news of the glory of the blessed God, with which I was entrusted.
Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
12 And I give thanks to Him who enabled me—Christ Jesus our Lord—that He reckoned me steadfast, having put [me] to the ministry,
Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
13 who before was speaking slander, and persecuting, and insulting, but I found kindness, because, being ignorant, I did [it] in unbelief,
ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
14 and the grace of our Lord exceedingly abounded, with faith and love that [is] in Christ Jesus.
Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
15 The word [is] steadfast, and worthy of all acceptance, that Christ Jesus came into the world to save sinners—of whom I am first;
Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
16 but because of this I found kindness, that Jesus Christ might first show forth all long-suffering in me, for a pattern of those about to believe on Him to continuous life. (aiōnios g166)
lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele. (aiōnios g166)
17 And to the King of the ages, the incorruptible, invisible, only wise God, [is] honor and glory through the ages of the ages! Amen. (aiōn g165)
Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee—kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
18 I commit to you this charge, child Timotheus, according to the prophecies that went before on you, that you may war in them the good warfare,
Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
19 having faith and a good conscience, which some having thrust away, made shipwreck concerning the faith,
na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
20 of whom are Hymenaeus and Alexander, whom I delivered to Satan, that they might be instructed not to speak evil.
Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

< 1 Timothy 1 >