< 1 Timothy 5 >

1 You may not rebuke an elder, but exhort [him] as a father, younger persons as brothers,
Usimkemee mwanamume mzee. Bali mtiye moyo kama baba yako. Uwatiye moyo vijana wa kiume kana kwamba ni ndugu zako.
2 aged women as mothers, younger ones as sisters—in all purity;
Uwatiye moyo wanawake wazee kama mama zako, na wanawake vijana kama dada zako kwa usafi wote.
3 honor widows who are really widows;
Waheshimu wajane, wale walio wajane kweli kweli.
4 and if any widow has children or grandchildren, let them first learn to show piety to their own house, and to give back a repayment to the parents, for this is right and acceptable before God.
Lakini kama mjane ana watoto au wajukuu, waache kwanza wajifunze kuonesha heshima kwa watu wa nyumbani mwao wenyewe. Waache wawalipe wazazi wao mema, kwa kuwa hii inapendeza mbele za Mungu.
5 And she who is really a widow and desolate, has hoped on God, and remains in the supplications and in the prayers night and day,
Lakini mjane kweli kweli ni yule aliyeachwa peke yake. Naye huweka tegemeo lake kwa Mungu. Siku zote hudumu katika sala na maombi usiku na mchana.
6 but she given to luxury [while] living has died;
Hata hivyo, mwanamke yule aishiye kwa anasa amekufa, ingawaje yu hai.
7 and charge these things, that they may be blameless;
Na uyahubiri haya mambo ili kwamba wasiwe na lawama.
8 and if anyone does not provide for his own, and especially for those of the household, he has denied the faith, and he is worse than an unbeliever.
Ila kama mtu asipowatunza ndugu zake, hususani wale walioko nyumbani mwake, ameikana imani na ni mmbaya kuliko mtu asiye amini.
9 A widow—do not let her be enrolled under sixty years of age, having been a wife of one husband,
Basi mwanamke aandikishwe kwenye orodha kama mjane akiwa na umri usiopungua miaka sitini, na ni mke wa mume mmoja.
10 being testified to in good works: if she brought up children, if she entertained strangers, if she washed holy ones’ feet, if she relieved those in tribulation, if she followed after every good work;
Lazima awe amejulikana kwa matendo mema, ikiwa ni kwamba amewajali watoto, au ameshakuwa mkarimu kwa wageni, au ameosha miguu ya waaminio, au alimesaidia ambao wamekuwa wakiteswa, au alijitoa kwa kazi yeyote njema.
11 and be refusing younger widows, for when they may revel against the Christ, they wish to marry,
Lakini kwa wale wajane vijana, kataa kuwaandikisha kwenye orodha ya wajane. Kwa kuwa wakiingia kwenye matamanio ya kimwili dhidi ya Kristo, wanataka kuolewa.
12 having judgment, because they cast away the first faith,
Kwa njia hii huingia kwenye hatia kwa kuwa huvunja kujitoa kwao kwa awali.
13 and also at the same time, they learn [to be] idle, going around the houses; and not only idle, but also tattlers and busybodies, speaking things they should not;
Na pia huingia kwenye mazoea ya uvivu. Wao huzunguka nyumba kwa nyumba. Si tu kwamba ni wavivu, bali pia huwa wasengenyaji na na wenye kuingilia mambo ya wengine. Wao husema mambo wasiyopaswa kuyasema.
14 I intend, therefore, younger ones to marry, to bear children, to be mistress of the house, to give no occasion to the opposer of reviling;
Kwa hiyo mimi nataka wanawake vijana waolewe, wazae watoto, wasimamie nyumba zao, ili kutokumpa adui nafasi ya kutushitaki kwa kufanya dhambi.
15 for some already turned aside after Satan.
Kwa sababu baadhi yao wameshamgeukia Shetani.
16 If any believing man or believing woman has widows, let them relieve them, and do not let the assembly be burdened, that it may relieve those [who are] really widows.
Kama mwanamke yeyote aaminiye ana wajane, basi na awasaidie, ili kanisa lisilemewe, ili liweze kuwasaidia wale walio wajane kweli kweli.
17 Let them, the well-leading elders, be counted worthy of double honor, especially those laboring in word and teaching,
Basi wazee wale watawalao vyema wahesabiwe kuwa wamestahili heshima maradufu, hasa wale wanaojishughulisha na kufundisha neno la Mungu.
18 for the Writing says, “You will not muzzle an ox treading out,” and, “Worthy [is] the workman of his reward.”
Kwa kuwa maandiko yanasema, “Usimfumbe ng'ombe kinywa apulapo nafaka,” na “Mfanya kazi anastahili mshahara wake.”
19 Do not receive an accusation against an elder, except on two or three witnesses.
Usipokee mashitaka dhidi ya mzee isipokuwa kuna mashahidi wawili au watatu.
20 Reprove those sinning before all, that the others may also have fear;
Waonye wakosaji mbele ya watu wote ili wengine waliobaki labda wataogopa.
21 I fully testify, before God and the Lord Jesus Christ, and the chosen messengers, that you may keep these things, without prejudging, doing nothing by partiality.
Nakuagiza kwa dhati mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu, na malaika wateule, kwamba uzitunze maagizo haya bila ubaguzi wowote, na kwamba usifanye jambo lolote kwa upendeleo.
22 Be quickly laying hands on no one, nor be having fellowship with [the] sins of others; be keeping yourself pure;
Usimwekee mtu yeyote mikono haraka. Usishiriki dhambi ya mtu mwingine. Yakupasa kujitunza mwenyewe uwe usafi.
23 no longer be drinking water, but be using a little wine, because of your stomach and of your frequent sicknesses;
Hakupasi kunywa maji pekee. Badala yake, unywe mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo na magonjwa yako ya mara kwa mara.
24 the sins of certain men are evident beforehand, leading before to judgment, but some also they follow after;
Dhambi za baadhi ya watu hujulikana kwa uwazi, na huwatangulia hukumuni. Lakini baadhi ya dhambi hufuata baadaye.
25 in like manner the right works are also evident beforehand, and those that are otherwise are not able to be hid.
Vivyo hivyo, baadhi ya kazi njema hujulikana kwa uwazi, lakini hata zingine hazitafichika.

< 1 Timothy 5 >