< 1 Timothy 4 >
1 And the Spirit expressly says that in latter times some will depart from the faith, giving heed to seducing spirits and teachings of demons,
Sasa Roho anasema waziwazi kwamba katika nyakati zijazo baadhi ya watu wataiacha imani na kuwa makini kusikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya kipepo yatakayofundishwa
2 speaking lies in hypocrisy, being seared in their own conscience,
katika uongo na unafiki. Dhamiri zao zitabadilishwa.
3 forbidding to marry—to abstain from meats that God created to be received with thanksgiving by those believing and acknowledging the truth,
Watawazuia kuoa na kupokea vyakula ambavyo Mungu aliviumba vitumiwe kwa shukrani miongoni mwao waaminio na wenye kuijua kweli.
4 because every creature of God [is] good, and nothing [is] to be rejected, with thanksgiving being received,
Kwa sababu kila kitu ambacho Mungu amekiumba ni chema. Hakuna ambacho tunapokea kwa shukrani kinastahili kukataliwa.
5 for it is sanctified through the word of God and intercession.
Kwa sababu kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kwa njia ya maombi.
6 Placing these things before the brothers, you will be a good servant of Jesus Christ, being nourished by the words of the faith, and of the good teaching, which you followed after,
Kama utayaweka mambo haya mbele ya ndugu, utakuwa mtumishi mzuri wa Yesu Kristo. Kwa sababu umestawishwa kwa maneno ya imani na kwa mafundisho mazuri ambayo umeyafuata.
7 but reject the profane and old women’s fables, and exercise yourself to piety,
Lakini zikatae hadithi za kidunia ambazo zinapendwa na wanawake wazee. Badala yake, jifunze mwenyewe katika utaua.
8 for bodily exercise is to little profit, but piety is profitable to all things, having promise of the life that now is, and of that which is coming;
Kwa maana mazoezi ya mwili yafaa kidogo, bali utauwa wafaa sana kwa mambo yote. Hutunza ahadi kwa maisha ya sasa na yale yajayo.
9 the word [is] steadfast, and worthy of all acceptance;
Ujumbe huu ni wakuaminiwa na unastahili kukubaliwa kabisa.
10 for this we both labor and are reproached, because we hope on the living God, who is Savior of all men—especially of those believing.
Kwa kuwa ni kwa sababu hii tunataabika na kufanya kazi kwa bidii sana. Kwa kuwa tunao ujasiri katika Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, lakini hasa kwa waaminio.
11 Charge these things, and teach;
Uyaseme na kuyafundisha mambo haya.
12 let no one despise your youth, but become a pattern of those believing in word, in behavior, in love, in spirit, in faith, in purity;
Mtu yeyote asiudharau ujana wako. Badala yake, uwe mfano kwa wote waaminio, katika usemi, mwenendo, upendo, uaminifu, na usafi.
13 until I come, give heed to the reading, to the exhortation, to the teaching;
Mpaka nitakapokuja, dumu katika kusoma, katika kuonya, na katika kufundisha.
14 do not be careless of the gift in you, that was given you through prophecy, with laying on of the hands of the eldership;
Usiipuuze karama iliyomo ndani yako, ambayo ulipewa kupitia unabii, kwa kuwekewa mikono na wazee.
15 be careful of these things; be in these things, that your advancement may be evident in all things;
Uyajali mambo haya. Ishi katika hayo ili kukua kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. Zingatia sana mwenendo wako na mafundisho.
16 take heed to yourself and to the teaching; remain in them, for doing this thing, you will save both yourself and those hearing you.
Dumu katika mambo haya. Maana kwa kufanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.