< 1 Thessalonians 5 >

1 And concerning the times and the seasons, brothers, you have no need of my writing to you,
Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2 for you have thoroughly known that the Day of the LORD so comes as a thief in the night,
Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3 for when they may say, “Peace and security,” then sudden destruction comes [on] them, as the travail [on] her who is with child, and they will not escape;
Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4 but you, brothers, are not in darkness, that the Day may catch you as a thief;
Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5 you are all sons of light, and sons of day; we are not of night, nor of darkness,
Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6 so, then, we may not sleep as also the others, but watch and be sober,
Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7 for those sleeping, sleep by night, and those making themselves drunk, are drunken by night,
Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8 and we, being of the day—let us be sober, putting on a breastplate of faith and love, and a helmet—a hope of salvation,
Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9 because God did not appoint us to anger, but to the acquiring of salvation through our Lord Jesus Christ,
Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10 who died for us, that whether we wake—whether we sleep—we may live together with Him;
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11 for this reason, comfort one another, and build up one another, as also you do.
Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12 And we ask you, brothers, to know those laboring among you and leading you in the LORD and admonishing you,
Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13 and to esteem them very abundantly in love, because of their work; be at peace among yourselves;
Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14 and we exhort you, brothers, admonish the disorderly, comfort the feeble-minded, support the weak, be patient to all;
Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15 see [that] no one may render evil for evil to anyone, but always pursue that which is good, both to one another and to all;
Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16 always rejoice;
Furahini daima,
17 continually pray;
salini kila wakati
18 give thanks in everything, for this [is] the will of God in Christ Jesus in regard to you.
na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19 Do not quench the Spirit;
Msimpinge Roho Mtakatifu;
20 do not despise prophesyings;
msidharau unabii.
21 prove all things; hold fast [to] that which is good;
Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22 abstain from all appearance of evil;
na epukeni kila aina ya uovu.
23 and may the God of peace Himself sanctify you wholly, and may your whole spirit and soul and body be preserved, unblameably at the coming of our Lord Jesus Christ;
Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 He who is calling you is steadfast, who also will do [it].
Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25 Brothers, pray for us.
Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26 Greet all the brothers with a holy kiss.
Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27 I charge you [by] the LORD, that the letter be read to all the holy brothers.
Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28 The grace of our Lord Jesus Christ [is] with you! Amen.
Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< 1 Thessalonians 5 >