< 1 Samuel 3 >

1 And the youth Samuel is serving YHWH before Eli, and the word of YHWH has been precious in those days—there is no vision breaking forth.
Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
2 And it comes to pass, at that time, that Eli is lying down in his place, and his eyes have begun [to be] faded—he is not able to see.
Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
3 And the lamp of God is not yet extinguished, and Samuel is lying down in the temple of YHWH, where the Ark of God [is],
Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
4 and YHWH calls to Samuel, and he says, “Here I [am].”
Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
5 And he runs to Eli and says, “Here I [am], for you have called for me”; and he says, “I did not call; turn back, lie down”; and he goes and lies down.
Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
6 And YHWH adds to call Samuel again, and Samuel rises and goes to Eli, and says, “Here I [am], for you have called for me”; and he says, “I have not called, my son, turn back, lie down.”
Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
7 And Samuel has not yet known YHWH, and the word of YHWH is not yet revealed to him.
Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8 And YHWH adds to call Samuel the third time, and he rises and goes to Eli, and says, “Here I [am], for you have called for me”; and Eli understands that YHWH is calling to the youth.
Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
9 And Eli says to Samuel, “Go, lie down, and it has been, if He calls to you, that you have said, Speak, YHWH, for Your servant is hearing”; and Samuel goes and lies down in his place.
Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
10 And YHWH comes, and stations Himself, and calls as time by time, “Samuel, Samuel”; and Samuel says, “Speak, for Your servant is hearing.”
Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
11 And YHWH says to Samuel, “Behold, I am doing a thing in Israel, at which the two ears of everyone hearing it tingle.
Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
12 In that day I establish to Eli all that I have spoken to his house, beginning and completing;
Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
13 and I have declared to him that I am judging his house for all time, for the iniquity which he has known, for his sons are making themselves vile, and he has not restrained them,
Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
14 and therefore I have sworn to the house of Eli: the iniquity of the house of Eli is not atoned for, by sacrifice, and by offering—for all time.”
Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
15 And Samuel lies until the morning, and opens the doors of the house of YHWH, and Samuel is afraid of declaring the vision to Eli.
Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
16 And Eli calls Samuel and says, “Samuel, my son”; and he says, “Here I [am].”
lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
17 And he says, “What [is] the word which He has spoken to you? Please do not hide it from me; so God does to you, and so does He add, if you hide from me a word of all the words that He has spoken to you.”
Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
18 And Samuel declares to him the whole of the words, and has not hid from him; and he says, “It [is] YHWH; that which is good in His eyes He does.”
Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
19 And Samuel grows up, and YHWH has been with him, and has not let any of his words fall to the earth;
Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
20 and all Israel knows, from Dan even to Beer-Sheba, that Samuel is established for a prophet to YHWH.
Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
21 And YHWH adds to appear in Shiloh, for YHWH has been revealed to Samuel, in Shiloh, by the word of YHWH.
Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.

< 1 Samuel 3 >