< 1 Samuel 23 >

1 And they declare to David, saying, “Behold, the Philistines are fighting against Keilah, and they are spoiling the threshing-floors.”
Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
2 And David inquires of YHWH, saying, “Do I go? And have I struck among these Philistines?” And YHWH says to David, “Go, and you have struck among the Philistines, and saved Keilah.”
akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
3 And David’s men say to him, “Behold, we here in Judah are afraid; and how much more when we go to Keilah, to the ranks of the Philistines?”
Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
4 And David adds again to inquire of YHWH, and YHWH answers him and says, “Rise, go down to Keilah, for I am giving the Philistines into your hand.”
Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
5 And David goes, and his men, to Keilah, and fights with the Philistines, and leads away their livestock, and strikes among them [with] a great striking, and David saves the inhabitants of Keilah.
Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
6 And it comes to pass, in the fleeing of Abiathar son of Ahimelech to David, to Keilah, an ephod came down in his hand.
(Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
7 And it is declared to Saul that David has come to Keilah, and Saul says, “God has made him known for my hand, for he has been shut in, to enter into a city of doors and bar.”
Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
8 And Saul summons all the people to the battle, to go down to Keilah, to lay siege to David and to his men.
Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
9 And David knows that Saul is devising the evil against him and says to Abiathar the priest, “Bring the ephod near.”
Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
10 And David says, “YHWH, God of Israel, Your servant has certainly heard that Saul is seeking to come to Keilah, to destroy the city on my account.
Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
11 Do the possessors of Keilah shut me up into his hand? Does Saul come down as Your servant has heard? YHWH, God of Israel, please declare [it] to Your servant.” And YHWH says, “He comes down.”
Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
12 And David says, “Do the possessors of Keilah shut up me and my men into the hand of Saul?” And YHWH says, “They shut [you] up.”
Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
13 And David rises—and his men—about six hundred men, and they go out from Keilah, and go up and down where they go up and down; and it has been declared to Saul that David has escaped from Keilah, and he ceases to go out.
Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
14 And David abides in the wilderness, in fortresses, and abides in the hill-country, in the wilderness of Ziph; and Saul seeks him [for] all the days, and God has not given him into his hand.
Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
15 And David sees that Saul has come out to seek his life, and David [is] in the wilderness of Ziph, in a forest.
Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
16 And Jonathan son of Saul rises, and goes to David [in the] forest, and strengthens his hand in God,
Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
17 and says to him, “Do not fear, for the hand of my father Saul does not find you, and you reign over Israel, and I am to you for second, and also so knows my father Saul.”
Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
18 And both of them make a covenant before YHWH; and David abides in the forest, and Jonathan has gone to his house.
Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
19 And the Ziphites go up to Saul at Gibeah, saying, “Is David not hiding himself with us in fortresses, in the forest, in the height of Hachilah, which [is] on the south of the desolate place?
Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
20 And now, by all the desire of your soul, O king, to come down, come down, and ours [is] to shut him up into the hand of the king.”
Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
21 And Saul says, “Blessed [are] you of YHWH, for you have pity on me;
Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
22 now go prepare yet, and know and see his place where his foot is; who has seen him there? For [one] has said to me, He is very cunning.
Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
23 And see and know of all the hiding places where he hides himself, and you have turned back prepared to me, and I have gone with you, and it has been, if he is in the land, that I have searched him out through all the thousands of Judah.”
Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
24 And they rise and go to Ziph before Saul, and David and his men [are] in the wilderness of Maon, in the plain, at the south of the desolate place.
Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
25 And Saul and his men go to seek, and they declare [it] to David, and he goes down the rock, and abides in the wilderness of Maon; and Saul hears, and pursues after David [to] the wilderness of Maon.
Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
26 And Saul goes on this side of the mountain, and David and his men on that side of the mountain, and David is hurried to go from the face of Saul, and Saul and his men are surrounding David and his men, to catch them.
Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
27 And a messenger has come to Saul, saying, “Hurry, and come, for the Philistines have pushed against the land.”
mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
28 And Saul turns back from pursuing after David, and goes to meet the Philistines, therefore they have called that place “The Rock of Divisions.”
Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
29 And David goes up there, and abides in fortresses [at] En-gedi.
Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.

< 1 Samuel 23 >