< 1 Samuel 2 >

1 And Hannah prays and says: “My heart has exulted in YHWH, My horn has been high in YHWH, My mouth has been large over my enemies, For I have rejoiced in Your salvation.
Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 There is none holy like YHWH, For there is none except You, And there is no rock like our God.
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3 You do not multiply—you speak haughtily—The old saying goes out from your mouth, For YHWH [is] a God of knowledge, And actions are weighed by Him.
Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
4 Bows of the mighty are broken, And the stumbling have girded on strength.
Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
5 The satiated hired themselves for bread, And the hungry have ceased. While the barren has borne seven, And she abounding with sons has languished.
Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
6 YHWH puts to death, and keeps alive, He brings down to Sheol, and brings up. (Sheol h7585)
BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
7 YHWH dispossesses, and He makes rich, He makes low, indeed, He makes high.
BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
8 He raises the poor from the dust, He lifts up the needy from a dunghill, To cause [them] to sit with nobles, Indeed, He causes them to inherit a throne of glory, For the fixtures of earth [are] of YHWH, And He sets the habitable world on them.
Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
9 He keeps the feet of His saints, And the wicked are silent in darkness, For man does not become mighty by power.
Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
10 YHWH—His adversaries are broken down, He thunders against them in the heavens: YHWH judges the ends of the earth, And gives strength to His king, And exalts the horn of His anointed.”
Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
11 And Elkanah goes to Ramath, to his house, and the youth has been serving YHWH [in] the presence of Eli the priest;
Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
12 and the sons of Eli [are] sons of worthlessness, they have not known YHWH.
Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
13 And the custom of the priests with the people [is that when] any man is sacrificing a sacrifice, then the servant of the priest has come in when the flesh is boiling, and [with] the hook of three teeth in his hand,
Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
14 and has struck [it] into the pan, or kettle, or cauldron, or pot; all that the hook brings up the priest takes for himself; thus they do to all Israel who are coming in there in Shiloh.
Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
15 Also, before they make incense with the fat, then the priest’s servant has come in and said to the man who is sacrificing, “Give flesh to roast for the priest, and he does not take boiled flesh from you, but raw”;
Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
16 and the man says to him, “Let them surely make incense with the fat according to the [custom] today, then take to yourself as your soul desires”; and he has said to him, “Surely you give now; and if not—I have taken by strength.”
Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
17 And the sin of the young men is very great [in] the presence of YHWH, for the men have despised the offering of YHWH.
Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
18 And Samuel is ministering [in] the presence of YHWH, a youth girt [with] an ephod of linen;
Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
19 and his mother makes a small upper coat for him, and she has brought it up to him from time to time, in her coming up with her husband to sacrifice the sacrifice of the time.
Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
20 And Eli blessed Elkanah and his wife, and said, “YHWH appoints seed of this woman for you, for the petition which she asked for YHWH”; and they have gone to their place.
Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
21 When YHWH has looked after Hannah, then she conceives and bears three sons and two daughters; and the youth Samuel grows up with YHWH.
BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
22 And Eli [is] very old, and has heard all that his sons do to all Israel, and how that they lie with the women who are assembling [at] the opening of the Tent of Meeting,
Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
23 and he says to them, “Why do you do things like these? For I am hearing of your evil words from all the people—these!
Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
24 No, my sons; for the report which I am hearing is not good, causing the people of YHWH to transgress.
Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
25 If a man sins against a man, then God has judged him; but if a man sins against YHWH, who prays for him?” And they do not listen to the voice of their father, though YHWH has delighted to put them to death.
“Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
26 And the youth Samuel is going on and growing up, and [is] good with both YHWH, and also with men.
Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
27 And a man of God comes to Eli and says to him, “Thus said YHWH: Was I really revealed to the house of your father in their being in Egypt, before Pharaoh’s house,
Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
28 even to choose him out of all the tribes of Israel for a priest for Myself, to go up on My altar, to make incense, to bear an ephod before Me, and I give to the house of your father all the fire-offerings of the sons of Israel?
Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
29 Why do you kick at My sacrifice and at My offering, which I commanded [in] My habitation, and honor your sons above Me, to make yourselves fat from the first part of every offering of Israel, of My people?
Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
30 Therefore—a declaration of YHWH, God of Israel—I certainly said, Your house and the house of your father walk up and down before Me for all time; and now—a declaration of YHWH—Far be it from Me! For he who is honoring Me, I honor, and those despising Me, are lightly esteemed.
Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
31 Behold, days [are] coming, and I have cut off your arm, and the arm of the house of your father, that an old man is not in your house;
Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
32 and you have beheld an adversary [in My] habitation, in all that He does good with Israel, and there is not an old man in your house all the days.
Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
33 And the man of yours I do not cut off from My altar—[My purpose is] to consume your eyes, and to grieve your soul; and all the increase of men [in] your house die;
Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
34 and this [is] the sign to you that comes to your two sons, to Hophni and Phinehas—in one day both of them die;
Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
35 and I have raised up a steadfast priest for Myself; he does as in My heart and in My soul; and I have built a steadfast house for him, and he has walked up and down before My anointed all the days;
Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
36 and it has been, everyone who is left in your house comes to bow himself to him for a wage of silver and a cake of bread, and has said, Please admit me to one of the priest’s offices, to eat a morsel of bread.”
Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'

< 1 Samuel 2 >