< 1 Samuel 13 >

1 Saul [is] a son of [[thirty]] years in his reigning, and he has reigned over Israel [forty]-two years,
Sauli alikwa na umri wa miaka [thelathini] alipoanza kutawala; alipokuwa ametawala Israeli kwa miaka [arobaini],
2 then Saul chooses for himself three thousand [men] out of Israel; and two thousand are with Saul in Michmash, and in the hill-country of Beth-El; and one thousand have been with Jonathan in Gibeah of Benjamin; and he has sent each one of the remnant of the people to his tents.
aliwachagua wanaume elfu tatu wa Israeli. Elfu mbili walikuwa pamoja naye huko Mikmashi na katika nchi ya milima ya Betheli, wakati huo wale elfu moja walikuwa pamoja na Yonathani katika Gibea ya Benyamini. Askari waliobaki aliwarudisha nyumbani, kila mtu hemani kwake.
3 And Jonathan strikes the garrison of the Philistines which [is] in Geba, and the Philistines hear, and Saul has blown with a horn through all the land, saying, “Let the Hebrews hear.”
Yonathani akaishinda ngome ya jeshi la Wafilisti iliyokuwa Geba na Wafilisti wakasikia habari hiyo. Baadaye Sauli alipiga tarumbeta katika nchi yote, akisema, “Sikieni enyi Waebrania.”
4 And all Israel have heard, saying, “Saul has struck the garrison of the Philistines,” and also, “Israel has been abhorred by the Philistines”; and the people are called after Saul to Gilgal.
Israeli yote imesikia kwamba Sauli ameipiga ngome ya Wafilisti, na pia kwamba Israeli imekuwa uvundo kwa Wafilisti. Ndipo askari wakaitwa kwa pamoja kuungana na Sauli huko Gilgali.
5 And the Philistines have been gathered to fight with Israel; thirty thousand chariots, and six thousand horsemen, and a people as the sand which [is] on the seashore for multitude; and they come up and encamp in Michmash, east of Beth-Aven.
Wafilisti walijikusanya pamoja kupigana dhidi ya Waisraeli: magari elfu tatu, watu elfu sita wakuendesha magari, na majeshi mengi kama mchanga ufukoni mwa bahari. Wakapanda na kupiga kambi huko Mikimashi, mashariki mwa Beth aveni.
6 And the men of Israel have seen that they are distressed, that the people have been oppressed, and the people hide themselves in caves, and in thickets, and in rocks, and in high places, and in pits.
Watu wa Israeli walipoona kuwa wapo katika matatizo -kwa maana watu walikata tamaa, wakajificha kwenye mapango, kwenye vichaka, kwenye miamba, kwenye visima na katika mashimo.
7 And Hebrews have passed over the Jordan to the land of Gad and Gilead; and Saul [is] yet in Gilgal, and all the people have trembled after him.
Baadhi ya Waebrania walipanda kwenda Yordani katika nchi ya Gadi na Gileadi. Lakini Sauli alibaki Gilgali, na watu waliomfuata wakitetemeka.
8 And he waits seven days, according to the appointment with Samuel, and Samuel has not come to Gilgal, and the people are scattered from off him.
Alisubiri kwa siku saba, muda uliopangwa na Samweli. Lakini Samweli hakufika huko Gilgali, na watu wakatawanyika mbali na Sauli.
9 And Saul says, “Bring the burnt-offering and the peace-offerings near to me”; and he causes the burnt-offering to ascend.
Sauli akasema, “Nileteeni sadaka ya kuteketezwa na sdaka ya amani.” Kisha akatoa sadaka ya kuteketezwa.
10 And it comes to pass at his completing to cause the burnt-offering to ascend, that behold, Samuel has come, and Saul goes out to meet him, to bless him;
Mara tu alipomaliza kutoa sadaka ya kuteketezwa Samweli akawasili. Sauli akatoka nje wakutane na kumsalimia.
11 and Samuel says, “What have you done?” And Saul says, “Because I saw that the people were scattered from off me, and you had not come at the appointment of the days, and the Philistines are gathered to Michmash,
Basi Samweli akasema, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanaiacha, na kwamba umechelewa hukufika kwa muda uliopangwa, na kwamba Wafilisti wamekwisha jikusanya huko Mikmashi,
12 and I say, Now the Philistines come down to me to Gilgal, and I have not appeased the face of YHWH; and I force myself, and cause the burnt-offering to ascend.”
nikasema, 'Sasa Wafilisti watashuka dhidi yangu huko Gilgali, na sijaomba kibali cha BWANA.' Kwa hiyo nikajilazimisha mwenyewe kutoa sadaka ya kuteketezwa.”.
13 And Samuel says to Saul, “You have been foolish; you have not kept the command of your God YHWH, which He commanded you, for now YHWH had established your kingdom over Israel for all time;
Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Umetenda mambo ya kipumbavu. Hukuheshimu amri ya BWANA Mungu wako aliyokupatia. Kwa maana BWANA angeutengeneza utawala wako juu ya Israeli milele.
14 and now, your kingdom does not stand, YHWH has sought [for] a man for Himself according to His own heart, and YHWH charges him for leader over His people, for you have not kept that which YHWH commanded you.”
Lakini sasa utawala wako hautaendelea. BWANA ametafuta mtu anayekubaliwa na moyo wake, kwa sababu wewe hukutii alichokuamuru.”
15 And Samuel rises, and goes up from Gilgal to Gibeah of Benjamin; and Saul inspects the people who are found with him, about six hundred men,
Ndipo Samweli akasimama akapanda kutoka Gilgali hadi Gibea ya Benyamini. Basi Sauli akawahesabu watu waliokuwapo pamoja naye, idadi yao ilikuwa kama watu mia sita.
16 and Saul, and his son Jonathan, and the people who are found with them, are abiding in Gibeah of Benjamin, and the Philistines have encamped in Michmash.
Sauli, mtoto wake Yonathani, na watu waliokuwa pamoja nao, wakabaki Geba ya Benyamimni. Lakini Wafilisti wakapiga kambi huko Mikmashi.
17 And the destroyer goes out from the camp of the Philistines—three detachments: one detachment turns to the way of Ophrah, to the land of Shual,
Wateka nyara makundi matatu wakaja kutoka kambi ya Wafilisti. Kundi moja likapinda kuelekea Ofra, hadi nchi ya Shuali.
18 and one detachment turns the way of Beth-Horon, and one detachment turns the way of the border which is looking on the Valley of the Zeboim, toward the wilderness.
Kundi jingine likageuka kuelekea Bethholoni, na kundi jingine likaelekea katika mpaka kulikabili bonde la Seboimu kuelekea jangwani.
19 And a craftsman is not found in all the land of Israel, for the Philistines said, “Lest the Hebrews make sword or spear”;
Hakuna hata mhunzi aliyeonekana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walisema, “Waebrania wasije wakajitengenezea mapanga au mikuki.”
20 and all Israel goes down to the Philistines, to each sharpen his plowshare, and his coulter, and his axe, and his mattock;
Lakini Waisraeli wote huwa wakiteremka kwa Wafilisti, kila mtu kunoa jembe lake, sululu yake, shoka lake na mundu wake.
21 and there has been the file for mattocks, and for coulters, and for three-pronged rakes, and for the axes, and to set up the goads.
Gharama za kunoa ncha za majembe, sululu, mashoka na kunyoosha michokoo ilikuwa theluthi moja ya shekeli.
22 And it has been, in the day of battle, that there has not been found a sword and spear in the hand of any of the people who [are] with Saul and with Jonathan—but it is found with Saul and with his son Jonathan.
Hivyo siku ya vita, hakukuwa na mapanga au mikuki iliyoonekana katika mikono yoyote ya askali waliokuwa na Sauli na Yonathani; Ni Sauli na mtoto wake tu ndio walikuwa nazo.
23 And the station of the Philistines goes out to the passage of Michmash.
Vikosi vya Wafilisti wakatokeza katika nija ya Mikmashi.

< 1 Samuel 13 >