< 1 Peter 1 >

1 Peter, an apostle of Jesus Christ, to the chosen sojourners of the dispersion of Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia, and Bithynia,
Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
2 according to [the] foreknowledge of God the Father, by [the] sanctification of the Spirit, to [the] obedience and sprinkling of the blood of Jesus Christ: Grace and peace be multiplied to you!
Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
3 Blessed [is] the God and Father of our Lord Jesus Christ, who, according to the abundance of His kindness begot us again to a living hope, through the resurrection of Jesus Christ out of the dead,
Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
4 to an incorruptible inheritance, and undefiled, and unfading, reserved for you in the heavens,
na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
5 who, in the power of God are being guarded, through faith, to salvation, ready to be revealed in the last time,
Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
6 in which you are glad, a little now, if it be necessary, being made to sorrow in various trials,
Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
7 so that the proof of your faith—much more precious than gold that is perishing, and being approved through fire—may be found to [result in] praise, and honor, and glory, at the revelation of Jesus Christ,
Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
8 whom, having not seen, you love, in whom, now believing [although] not seeing, you are glad with unspeakable joy and have been filled with glory,
Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
9 receiving the outcome of the faith—salvation of your souls;
kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
10 concerning which salvation [the] prophets sought out and searched out, who prophesied concerning the grace toward you,
Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
11 searching in regard to what or what manner of time the Spirit of Christ that was in them was signifying, testifying beforehand of the sufferings of Christ and the glory after these,
Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
12 to whom it was revealed, that not to themselves, but to us they were ministering these, which now were told to you (through those who proclaimed good news to you), by the Holy Spirit sent from Heaven, to which things messengers desire to look into intently.
Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
13 For this reason, having girded up the loins of your mind, being sober, hope perfectly on the grace that is being brought to you in the revelation of Jesus Christ,
Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
14 as obedient children, not fashioning yourselves to the former desires in your ignorance,
Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
15 but according as He who called you [is] holy, you also, become holy in all behavior,
Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
16 because it has been written: “Become holy, because I am holy”;
Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
17 and if you call on the Father, who is judging without favoritism according to the work of each, pass the time of your sojourn in fear,
Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
18 having known that, not with corruptible things—silver or gold—were you redeemed from your foolish behavior inherited from our forefathers,
Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
19 but with precious blood, as of a lamb unblemished and unspotted—Christ’s—
bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
20 foreknown, indeed, before the foundation of the world, and revealed in the last times because of you,
Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
21 who through Him believe in God who raised [Him] out of the dead, and gave glory to Him, so that your faith and hope may be in God.
Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
22 Having purified your souls in the obedience of the truth through the Spirit to unhypocritical brotherly love, love one another earnestly out of a pure heart,
Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
23 being begotten again, not out of corruptible seed, but incorruptible, through a word of God—living and remaining—throughout the age; (aiōn g165)
Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn g165)
24 because all flesh [is] as grass, and all glory of man as flower of grass; the grass withered, and the flower of it fell away,
Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
25 but the saying of the LORD remains—throughout the age; and this is the saying of good news that was proclaimed to you. (aiōn g165)
Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn g165)

< 1 Peter 1 >