< 1 Corinthians 14 >

1 Pursue love, and earnestly seek the spiritual things, and rather that you may prophesy,
Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
2 for he who is speaking in an [unknown] tongue—he does not speak to men, but to God, for no one listens, and he speaks secrets in spirit;
Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
3 and he who is prophesying to men speaks edification, and exhortation, and comfort;
Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
4 he who is speaking in an [unknown] tongue, edifies himself, and he who is prophesying, edifies the Assembly;
Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
5 and I wish you all to speak with tongues, and more that you may prophesy, for greater is he who is prophesying than he who is speaking with tongues, except one may interpret, that the Assembly may receive edification.
Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
6 And now, brothers, if I may come to you speaking tongues, what will I profit you, except I will speak to you either in revelation, or in knowledge, or in prophesying, or in teaching?
Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
7 Yet the things without life giving sound—whether pipe or harp—if they may not give a difference in the sounds, how will be known that which is piped or that which is harped?
Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
8 For also, if a trumpet may give an uncertain sound, who will prepare himself for battle?
Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
9 So also you, if you may not give speech easily understood through the tongue—how will that which is spoken be known? For you will be speaking to air.
Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
10 There are, it may be, so many kinds of voices in the world, and none of them is unmeaning.
Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
11 If, then, I do not know the power of the voice, I will be a foreigner to him who is speaking, and he who is speaking is a foreigner to me;
Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
12 so you also, since you are earnestly desirous of spiritual gifts, seek for the building up of the Assembly that you may abound;
Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
13 for this reason he who is speaking in an [unknown] tongue—let him pray that he may interpret;
Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
14 for if I pray in an [unknown] tongue, my spirit prays, and my understanding is unfruitful.
Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
15 What then is it? I will pray [in] the spirit, and I will also pray [with] understanding; I will sing psalms [in] the spirit, and I will also sing psalms [with] understanding;
Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
16 since, if you may bless in spirit, he who is filling the place of the commoner, how will he say the Amen at your giving of thanks, since he has not known what you say?
Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
17 For you, indeed, give thanks well, but the other is not built up!
Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
18 I give thanks to my God—more than you all with tongues speaking—
Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
19 but I wish to speak five words in an assembly through my understanding, that I also may instruct others, rather than myriads of words in an [unknown] tongue.
Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
20 Brothers, do not become children in the understanding, but in the evil be children, and in the understanding become perfect;
Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
21 in the Law it has been written, that, “With other tongues and with other lips I will speak to this people, and even so they will not hear Me, says the LORD”;
Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
22 so that the tongues are for a sign, not to the believing, but to the unbelieving; and the prophecy [is] not for the unbelieving, but for the believing.
Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
23 If, therefore, the whole assembly may come together to the same place, and all may speak with tongues, and there may come in commoners or unbelievers, will they not say that you are mad?
Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
24 And if all may prophesy, and anyone may come in, an unbeliever or commoner, he is convicted by all, he is discerned by all,
Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
25 and so the secrets of his heart become visible, and so having fallen on [his] face, he will worship God, declaring that God really is among you.
nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
26 What then is it, brothers? Whenever you may come together, each of you has a psalm, has a teaching, has a tongue, has a revelation, has an interpretation. Let all things be for building up;
Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27 if anyone speaks an [unknown] tongue, by two, or at the most, by three, and in turn, and let one interpret;
Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
28 and if there may be no interpreter, let him be silent in an assembly, and let him speak to himself, and to God.
Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
29 And prophets—let two or three speak, and let the others discern,
Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
30 and if [anything] may be revealed to another [who is] sitting, let the first be silent;
Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
31 for you are able, one by one, all to prophesy, that all may learn, and all may be exhorted,
Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
32 and the spiritual gift of prophets are subject to prophets,
Roho za manabii huwatii manabii.
33 for God is not [a God] of tumult, but of peace, as in all the assemblies of the holy ones.
Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
34 Your women, let them be silent in the assemblies, for it has not been permitted to them to speak, but to be subject, as the Law also says;
wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
35 and if they wish to learn anything, let them question their own husbands at home, for it is a shame to women to speak in an assembly.
Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
36 Did the word of God come forth from you? Or did it come to you alone?
Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
37 If anyone thinks to be a prophet, or spiritual, let him acknowledge the things that I write to you—that they are commands of the LORD;
Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
38 and if anyone is ignorant—let him be ignorant;
Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
39 so that, brothers, earnestly desire to prophesy, and do not forbid to speak with tongues;
Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
40 let all things be done decently and in order.
Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.

< 1 Corinthians 14 >