< 1 Corinthians 12 >

1 And concerning the spiritual things, brothers, I do not wish you to be ignorant;
Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2 you have known that you were nations, being carried away as you were led to the mute idols;
Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3 for this reason, I give you to understand that no one, speaking in the Spirit of God, says Jesus [is] accursed, and no one is able to say Jesus [is] LORD, except in the Holy Spirit.
Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: “Yesu alaaniwe!” Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: “Yesu ni Bwana,” asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4 And there are diversities of gifts, and the same Spirit;
Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5 and there are diversities of ministries, and the same Lord;
Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6 and there are diversities of workings, and it is the same God—who is working all in all.
Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7 And to each has been given the manifestation of the Spirit for profit;
Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8 for to one through the Spirit has been given a word of wisdom, and to another a word of knowledge, according to the same Spirit;
Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9 and to another faith in the same Spirit, and to another gifts of healings in the same Spirit;
Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10 and to another in-workings of mighty deeds; and to another prophecy; and to another discernings of spirits; and to another [various] kinds of tongues; and to another interpretation of tongues:
humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11 and the one and the same Spirit works all these, dividing to each individually as He intends.
Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12 For even as the body is one, and has many members, and all the members of the one body, being many, are one body, so also [is] the Christ,
Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote—ingawaje ni vingi—hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13 for also in one Spirit we were all immersed into one body, whether Jews or Greeks, whether servants or freemen, and all were made to drink one Spirit,
Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14 for also the body is not one member, but many.
Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15 If the foot may say, “Because I am not a hand, I am not of the body,” is it not, because of this, not of the body?
Kama mguu ungejisemea: “Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili”, je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16 And if the ear may say, “Because I am not an eye, I am not of the body,” is it not, because of this, not of the body?
Kama sikio lingejisemea: “Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili”, je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17 If the whole body [were] an eye, where the hearing? If the whole hearing, where the smelling?
Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18 And now, God set the members, each one of them in the body, according as He willed,
Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19 and if all were one member, where [is] the body?
Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 And now, indeed, [are] many members, but one body;
Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21 and an eye is not able to say to the hand, “I have no need of you”; nor again the head to the feet, “I have no need of you.”
Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: “Sikuhitaji wewe”, wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Siwahitaji ninyi.”
22 But much more the members of the body seeming to be weaker are necessary,
Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23 and those that we think to be less honorable of the body, around these we put more abundant honor, and our unseemly things have more abundant seemliness,
Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24 and our seemly things have no need; but God tempered the body together, having given more abundant honor to the lacking part,
ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25 that there may be no division in the body, but that the members may have the same anxiety for one another,
ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26 and whether one member suffers, all the members suffer with [it], or one member is glorified, all the members rejoice with [it];
Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27 and you are the body of Christ, and members in particular.
Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28 And some, indeed, God set in the Assembly: first apostles, secondly prophets, thirdly teachers, afterward powers, afterward gifts of healings, helpings, governings, various kinds of tongues.
Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29 [Are] all apostles? [Are] all prophets? [Are] all teachers? [Are] all powers?
Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30 [Do] all have gifts of healings? Do all speak with tongues? Do all interpret?
Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31 And earnestly desire the better gifts; and yet I show to you a far [more] excelling way:
Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.

< 1 Corinthians 12 >