< 1 Chronicles 6 >
1 Sons of Levi: Gershon, Kohath, and Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 And the sons of Kohath: Amram, Izhar, and Hebron, and Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 And sons of Amram: Aaron, and Moses, and [his daughter] Miriam. And sons of Aaron: Nadab, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eleazar begot Phinehas, Phinehas begot Abishua,
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 and Abishua begot Bukki, and Bukki begot Uzzi,
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 and Uzzi begot Zerahiah, and Zerahiah begot Meraioth,
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Meraioth begot Amariah, and Amariah begot Ahitub,
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 and Ahitub begot Zadok, and Zadok begot Ahimaaz,
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 and Ahimaaz begot Azariah, and Azariah begot Johanan,
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 and Johanan begot Azariah—him who acted as priest in the house that Solomon built in Jerusalem.
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 And Azariah begets Amariah, and Amariah begot Ahitub,
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 and Ahitub begot Zadok, and Zadok begot Shallum,
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 and Shallum begot Hilkiah, and Hilkiah begot Azariah,
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 and Azariah begot Seraiah, and Seraiah begot Jehozadak;
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 and Jehozadak has gone in YHWH’s removing Judah and Jerusalem by the hand of Nebuchadnezzar.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Sons of Levi: Gershom, Kohath, and Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 And these [are] names of sons of Gershom: Libni and Shimei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 And sons of Kohath: Amram, and Izhar, and Hebron, and Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Sons of Merari; Mahli and Mushi. And these [are] families of the Levite according to their fathers;
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 of Gershom: Libni his son, Jahath his son, Zimmah his son,
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Joah his son, Iddo his son, Zerah his son, Jeaterai his son.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 Sons of Kohath: Amminadab his son, Korah his son, Assir his son,
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Elkanah his son, and Ebiasaph his son, and Assir his son,
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Tahath his son, Uriel his son, Uzziah his son, and Shaul his son.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 And sons of Elkanah: Amasai and Ahimoth.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Elkanah—sons of Elkanah: Zophai his son, and Nahath his son,
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Eliab his son, Jeroham his son, Elkanah his son.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 And sons of Samuel: the firstborn Vashni, and the second Abijah.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Sons of Merari: Mahli, Libni his son, Shimei his son, Uzzah his son,
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Shimea his son, Haggiah his son, Asaiah his son.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 And these [are] they whom David stationed over the parts of the song of the house of YHWH, from the resting of the Ark,
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 and they are ministering before the Dwelling Place of the Tent of Meeting, in song, until the building by Solomon of the house of YHWH in Jerusalem; and they stand according to their ordinance over their service.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 And these [are] those standing, and their sons, of the sons of the Kohathite: Heman the singer, son of Joel, son of Shemuel,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 son of Elkanah, son of Jeroham, son of Eliel, son of Toah,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 son of Zuph, son of Elkanah, son of Mahath, son of Amasai,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 son of Elkanah, son of Joel, son of Azariah, son of Zephaniah,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 son of Tahath, son of Assir, son of Ebiasaph, son of Korah,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 son of Izhar, son of Kohath, son of Levi, son of Israel.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 And his brother Asaph, who is standing on his right—Asaph, son of Berachiah, son of Shimea,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 son of Michael, son of Baaseiah, son of Malchiah,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 son of Ethni, son of Zerah, son of Adaiah,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 son of Ethan, son of Zimmah, son of Shimei,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 son of Jahath, son of Gershom, son of Levi.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 And sons of Merari, their brothers, on the left: Ethan son of Kishi, son of Abdi, son of Malluch,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 son of Hashabiah, son of Amaziah, son of Hilkiah,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 son of Amzi, son of Bani, son of Shamer,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 son of Mahli, son of Mushi, son of Merari, son of Levi.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 And their brothers the Levites are put to all the service of the Dwelling Place of the house of God.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 And Aaron and his sons are making incense on the altar of the burnt-offering, and on the altar of the incense, for all the work of the Holy of Holies, and to make atonement for Israel, according to all that Moses servant of God commanded.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 And these [are] sons of Aaron: Eleazar his son, Phinehas his son, Abishua his son,
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Bukki his son, Uzzi his son, Zerahiah his son,
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Meraioth his son, Amariah his son, Ahitub his son,
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Zadok his son, Ahimaaz his son.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 And these [are] their dwellings, throughout their towers, in their borders, of the sons of Aaron, of the family of the Kohathite, for the lot was theirs;
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 and they give to them Hebron in the land of Judah and its outskirts around it;
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 and they gave the field of the city and its villages to Caleb son of Jephunneh.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 And they gave the cities of refuge to the sons of Aaron: Hebron, and Libnah and its outskirts, and Jattir, and Eshtemoa and its outskirts,
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 and Hilen and its outskirts, Debir and its outskirts,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 and Ashan and its outskirts, and Beth-Shemesh and its outskirts.
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 And from the tribe of Benjamin: Geba and its outskirts, and Allemeth and its outskirts, and Anathoth and its outskirts. All their cities [are] thirteen cities among their families.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 And to the sons of Kohath, those left of the family of the tribe, from the half of the tribe, the half of Manasseh, by lot, [are] ten cities.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 And to the sons of Gershom, for their families, from the tribe of Issachar, and from the tribe of Asher, and from the tribe of Naphtali, and from the tribe of Manasseh in Bashan, [are] thirteen cities.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 To the sons of Merari, for their families, from the tribe of Reuben, and from the tribe of Gad, and from the tribe of Zebulun, by lot, [are] twelve cities.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 And the sons of Israel give the cities and their outskirts to the Levites.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 And they give by lot from the tribe of the sons of Judah, and from the tribe of the sons of Simeon, and from the tribe of the sons of Benjamin, these cities which they call by name;
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 and some of the families of the sons of Kohath have cities of their border from the tribe of Ephraim;
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 and they give the cities of refuge to them: Shechem and its outskirts in the hill-country of Ephraim, and Gezer and its outskirts,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 and Jokmeam and its outskirts, and Beth-Horan and its outskirts,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 and Aijalon and its outskirts, and Gath-Rimmon and its outskirts;
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 and from the half tribe of Manasseh: Aner and its outskirts, and Bileam and its outskirts, for the family of the sons of Kohath who are left.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 To the sons of Gershom from the family of the half of the tribe of Manasseh: Golan in Bashan and its outskirts, and Ashtaroth and its outskirts;
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 and from the tribe of Issachar: Kedesh and its outskirts, Daberath and its outskirts,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 and Ramoth and its outskirts, and Anem and its outskirts;
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 and from the tribe of Asher: Mashal and its outskirts, and Abdon and its outskirts,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 and Hukok and its outskirts, and Rehob and its outskirts;
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 and from the tribe of Naphtali: Kedesh in Galilee and its outskirts, and Hammon and its outskirts, and Kirjathaim and its outskirts.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 To the sons of Merari who are left, from the tribe of Zebulun: Rimmon and its outskirts, Tabor and its outskirts;
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 and from beyond the Jordan by Jericho, at the east of the Jordan, from the tribe of Reuben: Bezer in the wilderness and its outskirts, and Jahzah and its outskirts,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 and Kedemoth and its outskirts, and Mephaath and its outskirts;
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 and from the tribe of Gad: Ramoth in Gilead and its outskirts, and Mahanaim and its outskirts,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 and Heshbon and its outskirts, and Jazer and its outskirts.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.