< Psalms 83 >

1 “A song or psalm of Assaph.” O God, take no rest for thyself: be not silent and keep not still, O God!
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 For, lo, thy enemies make a tumult, and they that hate thee have lifted up their head.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 Against thy people they take crafty secret device, and they consult against those whom thou protectest.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 They have said, Come, and let us cut them off from being a nation; and the name of Israel shall be remembered no more.
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 For they have consulted cordially together; against thee they make a covenant:
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 The tents of Edom, and the Ishmaelites: Moab, and the Hagarenes;
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, and 'Ammon, and 'Amalek; the Philistines with the inhabitants of Tyre;
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Also Asshur is joined with them; they have become an arm unto the children of Lot. (Selah)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Do unto them as [unto] Midian; as to Sissera, as to Jabin, at the brook Kishon:
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 Who were annihilated at 'En-dor; they became as dung for the ground.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Render them, their nobles, like 'Oreb, and like Zeeb; yea, like Zebach and like Zalmunna' all their princes;
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Who said, Let us conquer for ourselves the dwellings of God,
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 O my God, render them like the thistle-down, like stubble before the wind.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 As the fire burneth up a forest, and as the flame setteth the mountains on fire:
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 So pursue them with thy storm, and with thy whirlwind do thou terrify them.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Fill their faces with shame, that they may seek thy name, O Lord!
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Let them be made ashamed and terrified for ever and aye; yea, let them be put to the blush and perish:
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 That they may know that thou, whose name is the Eternal, art by thyself alone, the Most High over all the earth.
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.

< Psalms 83 >