< Psalms 80 >
1 “To the chief musician upon Shoshannim; an 'Eduth by Assaph; a psalm.” O Shepherd of Israel, give ear, thou that leadest Joseph like a flock; thou that dwellest between the cherubims, shine forth.
Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
2 Before Ephraim and Benjamin and Menasseh awaken thy might, and come to our help.
Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
3 O God, cause us to return, and let thy countenance shine, that we may be saved.
Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
4 O Lord of hosts, how long shall thy anger smoke against the prayer of thy people?
Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
5 Thou feedest them with the bread of tears, and givest them tears to drink in great measure.
Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
6 Thou renderest us a contest unto our neighbors: and our enemies hold derision among themselves.
Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
7 O God of hosts, cause us to return, and let thy countenance shine, that we may be saved.
Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
8 A vine didst thou remove out of Egypt: thou drovest out nations, and plantedst it.
Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
9 Thou didst clear out a place before it, and it struck its root deeply, and it filled the land.
Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
10 Mountains were covered with its shadow, and with its boughs the cedars of God.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 It sent out its tendrils as far as the sea, and unto the river its suckers.
Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
12 Wherefore hast thou now broken down its fences, so that all who pass by the way pluck the fruit from it?
Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
13 The boar out of the forest doth gnaw at it, and what moveth on the field feedeth on it.
Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
14 O God of hosts, return; I pray thee, look down from heaven, and behold, and think of this vine;
Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
15 And of the sprout which thy right hand hath planted, and of the branch that thou hast made strong for thyself.
Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
16 It is burnt with fire, it is hewn down; because of the rebuke of thy countenance do they perish.
Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
17 Let thy hand be over the man of thy right hand, over the son of man whom thou hast made strong for thyself.
Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
18 Then will we not swerve from thee: revive us again, and we will call on thy name.
Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
19 O Lord God of hosts, cause us to return: let thy countenance shine, that we may be saved.
Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.