< Psalms 78 >
1 “A Maskil of Assaph.” Give ear, O my people, to my instruction: incline thy ear to the words of my mouth.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I will open with a parable my mouth: I will utter riddles out of ancient times;
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Which we have heard and know, and which our fathers have related unto us.
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 We will not conceal them from their children, relating to the latest generation the praises of the Lord, and his strength, and his wonderful deeds which he hath done.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Yea, he established a testimony in Jacob, and instituted a law in Israel, which he commanded our fathers, that they should make them known to their children:
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 In order that the latest generation might know them, even the children that are to be born; that they may arise and relate them to their children;
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 That they may place in God their hope, and not forget the doings of God, but observe his commandments;
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 And that they may not be like their fathers, a stubborn and rebellious generation; a generation that had not directed their heart firmly, and whose spirit was not faithful to God.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 The children of Ephraim, like well-armed archers, that turn round on the day of battle,
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 Kept not the covenant of God, and in his law they refused to walk;
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 And they forgot his deeds, as also his wonders, which he had permitted them to see.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 In the presence of their fathers did he do wonders, in the land of Egypt, in the fields of Zo'an.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 He divided the sea, and caused them to pass through; and he made the waters stand upright as a wall.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 And he led them with the cloud by day, and all the night with a light of fire.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 He split rocks in the wilderness, and gave them drink as out of the mighty deep.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 And he brought forth running streams out of the rock, and caused water to run down like rivers.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 But they repeated to sin yet more against him, rebelling against the Most High in the desert.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 And they tempted God in their heart, by asking food for their desire.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Yea, they spoke against God: they said, Will God be able to set in order a table in the wilderness?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Behold, he smote the rock, so that waters gushed out, and streams overflowed: shall he also be able to give bread? or can he provide flesh for his people?
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Therefore, when the Lord heard this, he became wroth: and a fire was kindled against Jacob, and anger also ascended against Israel,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 Because they had not believed in God, and had not trusted in his salvation.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Then he ordained the skies from above, and the doors of heaven he opened;
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 And he let rain down upon them manna to eat, and the corn of heaven gave he unto them.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Angels' bread did man eat: he sent them provision to satisfaction.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 He caused an east wind to pass along the heavens; and he led forth by his strength the south wind.
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 And he let rain upon them flesh [as plentiful] as the dust, and winged birds like the sand of the sea;
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 And he let them fall in the midst of their camp, round about their habitations.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 And they ate, and were greatly satisfied, and what they longed for he brought unto them.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 They were not estranged from their longing, yet was their food in their mouth:
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 When the wrath of God ascended against them, and he slew some of the fattest of them, and the young men of Israel did he strike down.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 With all this they sinned again, and believed not in his wonders.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Therefore he caused their days to come to an end in nought, and their years in dread.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 When he slew them, then did they seek him, and they returned and inquired earnestly after God.
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 And they remembered that God was their rock, and the most high God their redeemer.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Nevertheless they prayed insincerely to him with their mouth, and with their tongue they lied unto him.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 For their heart was not firm with him, and they were not faithful in his covenant.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 But he, being merciful, forgave the iniquity, and destroyed [them] not: yea, many a time turned he his anger away, and did not awaken all his fury.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 And he remembered that they are but flesh, a spirit that passeth away, and returneth not again.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 How oft did they rebel against him in the wilderness, grieve him in the desert!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Yea, they once more tempted God, and set limits to the Holy One of Israel.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 They remembered not his hand, the day when he ransomed them from the adversary;
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 When he displayed in Egypt his signs, and his wonderful tokens in the fields of Zo'an.
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 And he changed their rivers into blood; and their running streams, that they could not drink [of them].
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 He sent out among them various wild beasts, which devoured them; and frogs, which destroyed them.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 And he gave unto the cricket their products, and their labor unto the locust.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 He slew with hail their vines, and their sycamore-trees with ice-bolts.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 And he surrendered to the hail their cattle, and their herds to the lightning's flashes.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 He let loose against them the fierceness of his anger, wrath and indignation, and distress, a host of angels of misfortune.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 He leveled a path for his anger; he withheld not from death their soul, and their life he surrendered to the pestilence;
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 And he smote all the first-born in Egypt; the first of their strength in the tents of Ham;
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 But he caused his own people to depart like flocks, and guided them like a drove in the wilderness.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 And he led them in safety, so that they felt no dread; but the sea covered over their enemies.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 And he brought them to his holy territory, even to this mount, which his right hand had acquired.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 And he drove out from before them nations, and divided them by the measuring-line as an inheritance, and he caused to dwell in their tents the tribes of Israel.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Yet they tempted and rebelled against the most high God, and his testimonies they kept not;
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 But swerved aside, and dealt unfaithfully like their fathers; they turned about like a deceitful bow.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 And they provoked him to anger with their high-places, and with their graven images they moved him to jealousy.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 God heard this, and he became wroth, and felt greatly disgusted with Israel;
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 And he cast off the dwelling at Shiloh, the tabernacle where he had dwelt among men;
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 And he gave up his strength unto captivity, and his glory into the adversary's hand.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 And he surrendered his people unto the sword; and with his inheritance was he wroth.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 His young men the fire devoured; and his virgins were not demanded in marriage.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 His priests fell by the sword; and his widows did not weep.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Then awoke the Lord as one that sleepeth, like a mighty man that shouteth by reason of wine.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 And he smote his enemies backward: a perpetual disgrace on them.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Yet was he disgusted with the tent of Joseph, and of the tribe of Ephraim he made not choice;
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 But he chose the tribe of Judah, the mount Zion which he loved.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 And he built like high [mountains] his sanctuary, like the earth which he hath founded for ever.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 And he made choice of David his servant, and took him from the sheep-folds:
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 From following the ewes with young he brought him, to feed Jacob his people, and Israel his inheritance.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 And he fed them according to the integrity of his heart; and by the skilfulness of his hands did he lead them.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.