< Psalms 77 >
1 “To the chief musician on Jeduthun, by Assaph a psalm.” [I lift up] my voice unto God, and I cry; [I lilt up] my voice unto God: do then give ear unto me.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 On the day of my distress I sought the Lord; in the night my hand was stretched out, and did not cease: my soul refused to be comforted.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 I think of God, and moan: I reflect, and my spirit is overwhelmed. (Selah)
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 Thou holdest my eyes awake: I am troubled and I cannot speak.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 I think over the days of old, the years of ancient times.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 I call to remembrance my song in the night; with my own heart I reflect: and my spirit maketh diligent search.
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 Will the Lord cast me off for ever? and will he never more give his favor again?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Is his kindness spent for ever? is his promise come to an end for all generations?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Hath God forgotten to be gracious? or hath he shut up in anger his mercies? (Selah)
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 And I said, This shall be my entreaty, [for] the years of the right hand of the Most High.
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 I will remember the deeds of the Lord; for I will remember out of ancient times thy wonders.
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 I will meditate also of all thy work, and on thy deeds will I reflect.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 O God, in holiness is thy way: where is there a god so great as God?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 Thou art the God that dost wonders: thou hast made known among the people thy strength.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 Thou hast redeemed with [a mighty] arm thy people, the sons of Jacob and Joseph. (Selah)
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 The waters saw thee, O God, the waters saw thee; they shook: also the depths trembled.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 The clouds poured out water; the skies sent forth thunder: also thy arrows sped along.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 The voice of thy thunder was in the whirlwind; lightnings gave light to the world; the earth trembled and quaked,
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 Through the sea led thy way, and thy path was through mighty waters, and thy footsteps could not be known.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 Thou didst lead like a flock thy people by means of Moses and Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.