< Psalms 63 >
1 “A psalm of David, when he was in the wilderness of Judah.” O God, thou art my God; early will I seek thee: my soul thirsteth for thee, my flesh longeth for thee in a dry land, and it is faint without water.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 As I have beheld thee in the sanctuary, seeing thy strength and thy glory;
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Because thy kindness is better than life, my lips shall praise thee:
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Thus will I bless thee while I live; in thy name will I lift up my hands.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 As with fat and marrow will my soul be satisfied; and with tuneful lips shall my mouth praise thee.
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 When I remember thee upon my couch, I meditate on thee in the night-watches.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Because thou hast been a help unto me; and in the shadow of thy wings will I sing rejoicingly.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 My soul cleaveth unto following thee: me thy right hand upholdeth.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 But those that seek my soul, to destroy it, shall go down into the lowest deeps of the earth.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 They shall be delivered up to the power of the sword: they shall become a prey for jackals.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 But the king shall rejoice in God: every one that sweareth by him shall glorify himself; for the mouth of those that speak falsehood shall be stopped.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.