< Psalms 50 >

1 “A psalm of Assaph.” The God of gods, the Lord, speaketh, and calleth the earth, from the rising of the sun unto his setting.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 Out of Zion, the perfection of beauty, God shineth forth.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Our God is coming, and will not keep silence: a fire devoureth before him, and round him there rageth a mighty storm.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 He will call to the heavens above, and to the earth, to judge his people.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 “Gather together unto me my pious servants, who make a covenant with me by sacrifice.”
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 And the heavens tell of his righteousness; for God is judge himself. (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 “Hear, O my people, and I will speak; O Israel, and I will testify against thee: God, thy God, am I.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Not because of thy sacrifices will I reprove thee; and thy burnt-offerings are continually before me.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 I will not take a bullock out of thy house, nor he-goats out of thy folds.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 For mine are all the beasts of the forest, the cattle upon a thousand mountains.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 I know all the fowls of the mountains: whatever moveth on the fields is with me.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 If I were hungry, I would not say it to thee; for mine is the world, and what filleth it.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Do I eat the flesh of fatted bulls, or drink the blood of he-goats?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Offer unto God thanksgiving; and pay unto the Most High thy vows;
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 And call on me on the day of distress: I will deliver thee, — and so wilt thou glorify me.”
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 But unto the wicked God saith, “What hast thou to do to relate my statutes, and why bearest thou my covenant upon thy mouth?
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 And yet thou hatest instruction, and castest my words behind thee.
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 When thou seest a thief, then art thou pleased with him, and with adulterers hast thou thy portion.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 Thou lettest loose thy mouth with evil, and thy tongue frameth deceit.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 Thou sittest and speakest against thy brother; against thy own mother's son thou utterest slander.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 These things hast thou done, and I kept silence: thou didst ween that I am like thyself; [but] I will reprove thee, and set it in order before thy eyes.”
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Do but reflect on this, ye that forget God, lest I tear [you] in pieces, with none to deliver.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 Whoso offereth thanksgiving glorifieth me: and to him that ordereth his course aright, will I show the salvation of God.
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psalms 50 >