< Psalms 42 >

1 BOOK SECOND: “To the chief musician, a Maskil, for the sons of Korach.” As a hart panteth after brooks of water, so panteth my soul after thee, O God.
Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
2 My soul thirsteth for God, for the living God: when shall I go [again] and be seen in the presence of God?
Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
3 My tears have been my food day and night; because men say unto me all the day, Where is thy God?
Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
4 These things will I remember, and pour out my soul in me: how I was wont to pass along amidst the multitude, journeying with them as a pilgrim to the house of God, with the voice of joyful song and thanksgiving, among the festive throng.
Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
5 Why art thou cast down, O my soul, and disquieted in me? Hope thou in God; for I shall yet thank him, because of the salvation of his countenance.
Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
6 O my God, my soul is cast down within me: therefore will I remember thee from the land of the Jordan, and from the peaks of Chermon, from the low mount.
Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
7 Deep calleth unto deep at the noise of thy waterfalls: all thy waves and thy billows have passed over me.
Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
8 In the daytime the Lord will command his kindness, and in the night his song shall be with me, as a prayer unto the God of my life.
Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
9 I will say unto God, my rock, why hast thou forgotten me? why must I walk grieved, under the oppression of the enemy?
Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
10 It is as death in my bones, when my assailants reproach me; when they say unto me all the day, Where is thy God?
Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
11 Why art thou cast down, O my soul? and why art thou disquieted within met? Hope thou in God; for I shall yet thank him, the salvation of my countenance, and my God.
Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.

< Psalms 42 >