< Psalms 146 >

1 Hallelujah. Praise, O my soul, the Lord.
Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
2 I will praise the Lord throughout my life: I will sing praises unto my God while I have any being.
Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
3 Put not your trust in princes, in the son of man, in whom there is no salvation.
Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
4 When his spirit goeth forth, he returneth to his [native] earth: on that very day perish his thoughts.
Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
5 [But] happy is he who hath the God of Jacob for his help, whose hope is on the Lord his God;
Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
6 Who hath made heaven, and earth, the sea, and all that is therein; who keepeth truth for ever;
Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
7 Who executeth justice for the oppressed: who giveth bread to the hungry: the Lord looseneth the prisoners;
Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
8 The Lord causeth the blind to see; the Lord raiseth up those who are bowed down; the Lord loveth the righteous:
Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
9 The Lord guardeth the strangers; the fatherless and widow he helpeth up; but the way of the wicked he maketh crooked.
Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
10 The Lord will reign for ever, even thy God, O Zion, unto all generations. Hallelujah.
Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.

< Psalms 146 >