< Psalms 135 >

1 Hallelujah. Praise ye the name of the Lord; praise him, O ye servants of the Lord;
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 Ye that stand in the house of the Lord, in the courts of the house of our God.
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Hallelujah; for the Lord is good: sing praises unto his name; for it is lovely.
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 For Jacob hath the Lord chosen unto himself, Israel, as his peculiar treasure.
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 For I well know that the Lord is great, and that our Lord is above all gods.
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 Whatsoever the Lord willeth, hath he done in the heavens, and on the earth, in the seas, and in all the deeps.
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 He causeth clouds to ascend from the ends of the earth; he maketh lightnings with the rain; he bringeth forth the wind out of his treasuries.
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 [He it is] who smote the first-born of Egypt, both of man and of cattle;
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 Who sent signs and wonderful tokens into the midst of thee, O Egypt, against Pharaoh, and against all his servants;
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Who smote many nations, and slew mighty kings;
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 Sichon the king of the Emorites, and 'Og the king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 And gave their land as an inheritance, an inheritance unto Israel his people.
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 O Lord, thy name [endureth] for ever: O Lord, thy memorial is throughout all generations.
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 For the Lord will espouse the cause of his people, and concerning his servants will he bethink himself.
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 The idols of the nations are silver and gold, the work of the hands of men.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 Mouths they have, but they speak not; eyes they have, but they see not;
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 Ears they have, but they hear not; neither is there any breath in their mouth.
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 Like them are those that make them, every one that trusteth in them.
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 O house of Israel, bless ye the Lord; O house of Aaron, bless ye the Lord.
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 O house of Levi, bless ye the Lord; ye that fear the Lord, bless the Lord.
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 Blessed be the Lord out of Zion, even he that resideth at Jerusalem. Hallelujah.
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Psalms 135 >