< Psalms 113 >

1 Hallelujah. Praise, O ye servants of the Lord, praise ye the name of the Lord.
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
2 Let the name of the Lord be blessed from this time forth and for evermore.
Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun unto his going down the name of the Lord is praised.
Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
4 High above all nations is the Lord, above the heavens is his glory.
Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
5 Who is like the Lord our God, who dwelleth on high?
Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
6 Who condescendeth to view what is done in the heavens, and on the earth?
atazamaye chini angani na duniani?
7 He raiseth up out of the dust the poor, from the dunghill he lifteth up the needy:
Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
8 That he may set him with princes, even with the princes of his people.
ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 He causeth the barren woman to dwell in the midst of [her] household, the joyful mother of children. Hallelujah.
Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!

< Psalms 113 >