< Proverbs 21 >

1 Like brooks of water is a king's heart in the hand of the Lord: whithersoever it pleaseth him doth he turn it.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Every way of a man is straight in his own eyes; but the Lord weigheth the hearts.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 To exercise righteousness and justice is more acceptable to the Lord than sacrifice.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 Haughtiness of the eyes, and an immoderate heart, are the sinful field of the wicked.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 The plans of the diligent tend only to plenty; but every hasty man is [destined] only to want.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 The getting of treasures by a tongue of falsehood is like the fleeting breath of those that seek death.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 The robbery of the wicked will drag them away; because they refuse to execute justice.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 Perverse is the way of the man that is estranged [from goodness]; but as for the pure, his work is upright.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 It is better to dwell in a corner of a roof, than with a quarrelsome woman in a roomy house.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 The soul of the wicked longeth for evil: his neighbor findeth no grace in his eyes.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 When the scorner is punished, the simple is made wise: and when the wise is taught intelligence, he receiveth knowledge.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 The righteous regardeth attentively the house of the wicked; [but God] overturneth the wicked into unhappiness.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 Whoso stoppeth his ears against the cry of the poor, he also will cry himself, but shall not be answered.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 A gift in secret pacifieth anger, and a bribe in the bosom, strong fury.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 It is joy to the righteous to execute justice; but it is a terror to wrong-doers.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 The man that wandereth astray out of the way of intelligence shall rest in the assembly of the departed.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 He that loveth pleasure will be a man of want: he that loveth wine and oil will not become rich.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 The wicked shall be a ransom for the righteous, and the treacherous shall be put in the stead of the upright.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 It is better to dwell in a desert land, than with a quarrelsome and vexatious woman.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 There are a desirable treasure and oil in the dwelling of the wise; but a foolish man will swallow it up.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 He that pursueth righteousness and kindness will find life, righteousness, and honor.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 A wise man scaleth the city of the mighty, and casteth down the strength in which they trusted.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 Whoso guardeth his mouth and his tongue guardeth his soul against distresses.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 The presumptuous and proud, scorner is his name, dealeth in the wrath of presumption.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 The longing of the slothful will kill him; for his hands refuse to labor.
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 All the day he feeleth a great longing; but the righteous giveth and withholdeth not.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 The sacrifice of the wicked is an abomination: how much more, when he bringeth it with a sinful purpose?
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 A lying witness shall perish; but the man that is obedient [to the law] can speak for ever.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 A wicked man showeth impudence in his face; but as for the upright, he will consider well his way.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 There is no wisdom nor understanding nor counsel against the Lord.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 The horse is prepared for the day of battle; but with the Lord is the victory.
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Proverbs 21 >