< Numbers 5 >

1 And the Lord spoke unto Moses, saying,
BWANA alinena na Musa. Akasema,
2 Command the children of Israel, that they send out of the camp every leper, and every one that hath an issue, and whosoever is defiled by the dead:
“Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
3 Both male and female shall ye send out, to without the camp shall ye send them; that they defile not their camps, in the midst whereof I dwell.
Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
4 And the children of Israel did so, and they sent them out to without the camp: as the Lord had spoken unto Moses, so did the children of Israel.
Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
5 And the Lord spoke unto Moses, saying,
Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
6 Speak unto the children of Israel, If any man or woman commit any sin against a fellow-man, thereby doing a trespass against the Lord, and this person thus become guilty:
“Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
7 Then shall they confess their sin which they have committed; and he shall make restitution for his trespass with the principal thereof, and its fifth part shall he add thereto, and give it unto him against whom he hath trespassed.
Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
8 But if the man have no kinsman to whom restitution could be made for the trespass, then shall the trespass which is restored unto the Lord, belong to the priest; besides the ram of the atonement, whereby an atonement shall be made for him.
Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
9 And every offering of all the holy things of the children of Israel, which they bring unto the priest, shall be his.
Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
10 And every man's hallowed things shall be his: whatsoever any man giveth to the priest, shall belong to him.
Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
11 And the Lord spoke unto Moses, saying,
Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
12 Speak unto the children of Israel, and say unto them, If the wife of any man go aside, and commit a trespass against him,
“Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
13 And a man lie with her carnally, and it be hidden from the eyes of her husband, because she hath been secretly defiled; and there be no witness against her, and she have not been detected and in the fact;
Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
14 And the spirit of jealousy come over him, and he be jealous of his wife, and she have been defiled; or the spirit of jealousy come over him, and he be jealous of his wife, and she have not been defiled:
Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
15 Then shall the man bring his wife unto the priest, and he shall bring her offering for her, the tenth part of an ephah of barley-meal; he shall not pour any oil upon it, nor put any frankincense thereupon; for it is a meat-offering of jealousy, a meat-offering of memorial, bringing iniquity to remembrance.
Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
16 And the priest shall bring her near, and place her before the Lord;
Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
17 And the priest shall take holy water in an earthen vessel; and of the dust that is on the floor of the tabernacle the priest shall take, and put it into the water;
Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
18 And the priest shall place the woman before the Lord, and uncover the woman's head, and put upon her hands the meat-offering of memorial, it is the meat-offering of jealousy; and in the hand of the priest shall be the bitter waters that bring the curse.
Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
19 And the priest shall charge her by an oath, and he shall say unto the woman, If no man have lain with thee, and if thou hast not gone aside to uncleanness behind thy husband: then be thou free from these bitter waters that bring the curse.
Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
20 But if thou hast gone aside behind thy husband, and if thou hast been defiled, and some man have lain with thee besides thy husband: —
Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
21 And the priest shall charge the woman with an oath of imprecation, and the priest shall say unto the woman, The Lord then make thee a curse and an oath among thy people, when the Lord doth cause thy thigh to fall away, and thy belly to swell;
ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
22 And these waters that bring the curse shall go into thy bowels, to cause the belly to swell, and the thigh to fall away; and the woman shall say, Amen, amen.
Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
23 And the priest shall write these curses on a roll, and he shall blot them out with the bitter waters.
Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
24 And he shall cause the woman to drink the bitter waters that bring the curse: and the waters that bring the curse shall enter into her for bitterness.
Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
25 And the priest shall take out of the woman's hand the meat-offering of jealousy, and he shall wave the meat-offering before the Lord, and bring it near to the altar:
Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
26 And the priest shall take a handful from the meat-offering, as its memorial, and burn it upon the altar, and after that shall he cause the woman to drink the water.
Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
27 And when he hath made her drink the water, then shall it come to pass, if she have been defiled, and have committed a trespass against her husband, that the waters that bring the curse shall enter into her, for bitterness, and her belly shall swell, and her thigh shall fall away; and the woman shall become a curse among her people.
Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
28 And if the woman have not been defiled, but be clean: then shall she remain unharmed, and she shall conceive seed.
Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
29 This is the law of jealousies, when a woman goeth aside behind her husband, and hath been defiled;
Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
30 Or when the spirit of jealousy cometh over him, and he be jealous of his wife; and he shall place the woman before the Lord, and the priest shall do unto her altogether according to this law.
Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
31 And the man shall be guiltless from iniquity; but this woman shall bear her iniquity.
Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”

< Numbers 5 >