< Numbers 23 >

1 And Bil'am said unto Balak, Build me here seven altars, and prepare me here seven bullocks and seven rams.
Balaamu akamwabia Balaki, “Jenga madhabahu saba kwa ajili yangu na uandae mafahari saba na kondoo dume saba.”
2 And Balak did as Bil'am had spoken; and Balak and Bil'am offered a bullock and a ram on every altar.
Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyoomba. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume mmoja kwa kila madhabahu.
3 And Bil'am said unto Balak, Place thyself by thy burnt-offering; and I will go, peradventure the Lord will come to meet me, and whatsoever he may show me I will tell thee: and he went thoughtfully alone.
Ndipo Balaamu alipomwamiba Balaki, “Simama kwenye sadaka yako ya kuteketezwa na mimi nitaenda. Labda BWANA atakuja kukutana na mimi. Chochote atakachoniambia nitakuambia.” Kwa hiyo akaenda juu ya mlima usiokuwa na miti.
4 And God met Bil'am: and he said unto him, The seven altars have I made ready, and I have offered a bullock and a ram upon every altar.
Wakati bado akiwa juu ya mlima. Mungu akakutana naye, na Balaamu akamwambia, “Nimejenga madhabahu saba, na nimetoa sadaka ya fahari na kondoo dume kwa kila madhabahu.”
5 And the Lord put a word in Bil'am's mouth, and said, Return unto Balak, and thus shalt thou speak.
BWANA akaweka ujumbe kwenye kinywa cha Baalamu akasema, “Rudi kwa Balaki ukamwambie.”
6 And he returned unto him, and, lo, he was standing by his burnt-offering, he, and all the princes of Moab.
Kwa hiyo Balaamu akarudi kwa Balaki aliyekuwa amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, na viongozi wote wa Moabu walikuwa pamoja naye.
7 And he took up his parable, and said, From Aram did Balak send for me, the king of Moab, out of the mountains of the east, Come, curse me Jacob, and come, defy Israel.
Ndipo Balaamu alipoanza kunena unabii wake akisema, “Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka katika milima ya mashariki, 'Njoo, nilaanie Yakobo kwa ajili yangu,' alisema, 'Njoo umtie unajisi Israeli,'
8 How shall I denounce, whom God hath not denounced? and how shall I defy, whom the Lord hath not defied?
Nawezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani? Nawezaje kuwapinga wale ambao Mungu hawapingi?
9 For from the top of rocks I see him, and from hills I behold him: lo, it is a people that shall dwell alone, and among the nations it shall not be reckoned.
Kwa kuwa kutoka juu ya miamba Ninamwona; kutoka kwenye milima ninamtazama. Kuna watu wanaoishi pekee yao na hawajioni wenyewe kama ni taifa la kawaida.
10 Who can count the dust of Jacob, and number the fourth part of Israel? May my soul die the death of the righteous, and may my last end be like his!
Nani awezaye kuyahesabu mavumbi ya Yakobo au kuhesabu hata robo ya Israeli? Naomba nife kifo cha mtu mwenye haki, na mwisho wa maisha yangu uwe kama wake!”
11 And Balak said unto Bil'am, What hast thou done unto me? to denounce my enemies did I take thee, and, behold, thou hast even blessed them.
Balaki akamwambia Balaamu, “Umenifanyia nini? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini ona, umewabariki,”
12 And he answered and said, Must I not take heed to speak that only which the Lord may put in my mouth?
Balaamu akajibu akasema, “Kwa nini nisiwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA anaweka kinywani mwangu?”
13 And Balak said unto him, Come, I pray thee, with me unto another place, from where thou canst see them; nevertheless a portion of them only wilt thou see, but the whole of them thou wilt not see: and denounce them for me from there.
Basi Balaki akamwambia, “Hebu uje nami kwenye eneo jingine ili uwaone. Utakaowaona ni wale wa karibu tu, huwezi kuwaona wote. Huko sasa unaweza kunilaania hawa watu.”
14 And he brought him to the field of the watchmen, on the top of Pisgah, and he built seven altars, and offered a bullock and a ram on every altar.
Kwa hiyo akampeleka Balaamu kwenye shamba la Zofimu, lililo juu ya Mlima Pisiga, na kule akajenga madhabau zingine saba. Akatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume kwa kila madhabahu.
15 And he said unto Balak, Place thyself here by thy burnt-offering, while I will repair to yonder place.
Kisha Balaamu akamwambia Balaki, “Simama hapa karibu na sadaka zako, wakati mimi naenda kukutana na BWANA kule.”
16 And the Lord met Bil'am, and put a word in his mouth, and said, Return unto Balak, and thus shalt thou speak.
Kwa hiyo BWANA akakutana na Balaamu na kumwekea ujumbe kinywani mwake. Alimwambia, “Rudi kwa Balaki ukamwambie huu ujumbe toka kwangu.”
17 And he came to him, and, behold, he was standing by his burnt-offering, and the princes of Moab with him; and Balak said unto him: What hath the Lord spoken?
Balaamu akamrudia, na tazama, alikuwa amesimama karibu na sadaka zake za kuteketezwa, na vionigozi wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamwuliza, “BWANA amekwambiaje?”
18 And he took up his parable, and said, Rise up, Balak, and hear; bend hither thy ear unto me, son of Zippor!
Balaamu akaanza kutoa unabii. Akasema, “Inuka, Balaki na usikilize. Nisikilize mimi wewe mwana wa Zippori.
19 God is not a man, that he should lie; nor a son of man, that he should repent: hath he said, and shall he not do it? and hath he spoken, and shall he not fulfill it?
Mungu siyo mtu, kwamba umdanganye, au mwanadamu awezaye kubadili mawazo. Je, alishawahi kuahidi kitu pasipo kukitekeleza? Je, alishawahi kusema kuwa atafanya kitu bila kufanya kama alivyosema?
20 Behold, to bless I have received [the word]; and he hath blessed, and I cannot reverse it.
Tazama, Mimi nimeamriwa kuwabariki. Mungu ametoa baraka, nami siwezi kuibadilisha.
21 He hath not beheld any wrong in Jacob, nor hath he seen perverseness in Israel: the Lord his God is with him, and the glory of the king dwelleth among him.
Hajawahi kuona magumu katika Yakobo au tabu katika Israeli. BWANA Mungu wao yuko pamoja nao, na kelele za wafalme wao ziko pamoja nao.
22 God, who brought them out of Egypt, is to them like the heights of the reem.
Mungu aliwatoa Misri kwa nguvu kama za nyati.
23 For there is no enchantment in Jacob, nor is there any divination in Israel: at the proper time shall it be said to Jacob and to Israel, what God doth work.
Hakuna uganga utakaofanikiwa dhidi ya Yakobo, na hakuna uchawi utakaomwumiza Israeli. Badala yake, itasemwa juu ya Yakobo na Israeli, 'Tazama kile ambacho Mungu amefanya!'
24 Behold, it is a people, that shall rise up as a lioness, and as a lion shall it raise itself: it will not lie down until it have eaten the prey, and have drunk the blood of the slain.
Tazama, watu wanainuka kama simba jike, kama vile simba ainukavyo na kuvamia. Halali chini mpaka ale windo lake na kunywa damu ya windo lake,”
25 And Balak said unto Bil'am, Neither shalt thou denounce them, nor shalt thou any wise bless them.
Kisha Balaki akamwambia Balaamu, “Kamwe usiwalaani wala kuwabariki.”
26 But Bil'am answered and said unto Balak, Have I not spoken unto thee, saying, all that the Lord will speak, that must I do.
Lakini Balaamu akamjibu Balaki, “Sijakuambia kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema?
27 And Balak said unto Bil'am, Come, I pray thee, I will take thee unto another place, peradventure it may be pleasing in the eyes of God that thou mayest denounce them for me from there.
Balaki akamwambia Balaamu, “Njoo sasa, Nami nitakupeleka mahali pengine. Labda kule itampendeza Mungu kunilaania hawa hawa watu.”
28 And Balak took Bil'am unto the top of Peor, that looketh toward the desert.
Kwa hiyo Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, ambao unalitazama chini lile jangwa,
29 And Bil'am said unto Balak, Build me here seven altars, and prepare me here seven bullocks and seven rams.
Balaamu akamwambia Balaki, “Nijengee madhabahu saba hapa na uniandalie mafahari saba na kondoo duume saba.
30 And Balak did as Bil'am had said, and he offered a bullock and a ram on every altar.
“Kwa hiyo Balaki akafanya kama alivyoambiwa; akatoa sadaka ya fahari na kondoo mume kwenye kila madhabahu.

< Numbers 23 >