< Numbers 21 >

1 And when the Canaanite, the king of 'Arad, who dwelt in the south, heard that Israel was coming by the way of the spies: he made an attack on Israel, and took from them some prisoners.
Aradi mfalme wa Wakanaani, aliyekuwa akiishi Negebu, aliposikia kuwa Israeli alikuwa akisafiri kwa kupitia barabara kuelekea Atharimu, akapigana dhidi ya Israeli na kujitwalia baadhi ya mateka.
2 And Israel made a vow unto the Lord, and said, If thou wilt but deliver this people into my hand, then will I devote their cities.
Israeli akaapa mbele ya BWANA akasema, “Kama utatupa ushindi dhidi ya hawa watu, ndipo tutakapoingamiza kabisa miji yao,”
3 And the Lord hearkened to the voice of Israel, and he delivered up the Canaanites; and they devoted them and their cities: and they called the name of the place Chormah.
BWANA akaisikia sautiya Israeli na kuwapa ushindi dhidi ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa pamoja na miji yao. Mahali pale paliitwa Horima.
4 And they set forward from mount Hor by the way to the Red Sea, to go round the land of Edom: and the spirit of the people became impatient because of the way.
Wakasafiri kutoka Mlima Hori kwa barabara kuelekea bahari ya shamu wakiizunguka nchi ya Edomu. Watu walikufa moyo kwa njia hiyo.
5 And the people spoke against God, and against Moses, Wherefore have ye brought us up out of Egypt to die in the wilderness? for there is no bread, and there is no water; and our soul loatheth this miserable bread.
Watu wakamnung'unikia Mungu na Musa: “Kwa nini umetutoa Misiri ili tufa katika jangwa hili? Hapa hakuna mikate, wala maji, na chakula hiki dhaifu kimetukinai.”
6 And the Lord let loose against the people poisonous serpents, and they bit the people; and there died much people of Israel.
Basi Mungu akatuma nyoka wa sumu kati yao. Wale nyoka wakawauma wale watu; watu wengi walikufa.
7 And the people then came to Moses, and they said, We have sinned, for we have spoken against the Lord, and against thee; pray unto the Lord, that he take away from us the serpents. And Moses prayed for the people.
Watu wakaenda kwa Musa wakamwambia, “Tumetenda dhambi kwa sababu tumemnung'unikia Mungu na wewe. Mwombe Mungu atuondolee hawa nyoka.” Kwa hiyo Musa akawaombea watu.
8 And the Lord said unto Moses, Make thyself a serpent, and set it upon a pole: and it shall come to pass, that whoever is bitten shall look at it, and he shall live.
BWANA akamwambia Musa, “Tengeneza nyoka na umweke kwenye nguzo. Na itakuwa kila anayeumwa, akimwangalia huyo nyoka atapona,”
9 And Moses made a serpent of copper, and put it upon a pole; and it came to pass, that, when a serpent had bitten any man, and he looked up to the serpent of copper, he remained alive.
Kwa hiyo Musa akatengeneza nyoka wa shaba naye akamweka juu ya nguzo. Na kila mtu alipoumwa na nyoka na kumwangalia huyo nyoka alipona.
10 And the children of Israel set forward, and encamped in Oboth.
Kisha watu wa Israeli wakasafiri na kisha kuweka kambi Obothi.
11 And they journeyed from Oboth, and encamped at 'Iye-ha'abarim, in the wilderness, which is before Moab, toward the rising of the sun.
Kisha wakasafiri kutoka pale na kuweka kambi Iye Abarimu katika jangwa linalokabili Moabu kuelekea upande wa mashariki.
12 From there they set forward and encamped in the valley of Zered.
Kutoka pale wakasafiri na kuweka kambi katika bonde la Zeredi.
13 From there they set forward, and encamped on the other side of Arnon, which is in the wilderness, and which cometh out of the boundary of the Emorites; for Arnon is the border of Moab, between Moab and between the Emorites.
Kutoka pale walisafiri na kuweka kambi kwenye upande mwingine wa mto Amoni, ambao ukubwa wake unaanzia kwenye mpaka wa Waamori. Mto wa Amoni ndio unaootengeneza mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
14 Therefore mention is made in the book of the wars of the Lord, of Vaheb in Supha, and of the brooks of Arnon,
Ndiyo maana imeandikwa katika gombo la Kitabu cha BWANA, “Wahebu katika Sufa, na bonde la Amoni,
15 And the descent of the brooks, that turneth toward Shebeth-'Ar, and leaneth upon the border of Moab;
mtelemko wa bonde linaloelekea katika mji wa Ari na kuelekea kwenye mpaka wa Moabu,”
16 And from there to the well; this is the well where the Lord said unto Moses, Assemble the people and I will give them water.
Kutoka pale wakasafiri mpaka Beeri, hapo ndipo palipo na kisima ambacho Bwana alimwambia Musa, “Wakusanye watu kwa ajili yangu ili uwape maji,”
17 Then did Israel sing this song, Come up, O well; sing ye unto it:
Ndipo Israeli waipoimba wimbo huu: “enyi visima, yajazeni maji. Imbeni juu ya kisima hiki.
18 Well, which the princes have dug, which the nobles of the people have hollowed out with the sceptre, with their staves; — and from the wilderness to Mattanah;
Kisima ambacho viongozi wetu walichimba, kisima ambacho wenye hekima walichimba kwa fimbo ya kifalme na kwa fimbo ya kutembelea.” Kisha kutoka jangwani walitembea mpaka Matanaha.
19 And from Mattanah to Nachaliel; and from Nachaliel to Bamoth;
Kutoka Matanaha walisafiri mpaka Nathalieli, na kutoka Nathalieli mpaka Bamothi,
20 And from Bamoth to the valley, which is in the fields of Moab, to the top of Pisgah, which looketh toward the desert.
na kutoka Bamothi hadi kwenye bonde la Moabu. Hapo ndipo kilele cha Mlima Piska kinapoonekana jangwani.
21 And Israel sent messengers unto Sichon the king of the Emorites, saying,
Kisha Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori akisema,
22 Let me pass through thy land; we will not turn aside into field, or into vineyard; we will not drink the water of a well: by the king's highway will we go along, until we have passed thy border.
Tunaomba tupite katika nchi yako. hatutapita katika shamba au kwenye shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya visima vyako. Tutapita katika njia kuu ya mfalme mpaka tutakapopita mpaka wako.”
23 But Sichon would not suffer Israel to pass through his border; and Sichon assembled all his people together; and went out against Israel into the wilderness; and he came to Yahaz, and fought against Israel.
Lakini mfalme Sihoni hakumruhusu Israeli kupita kwenye mpaka wao. Badala yake, Sihoni akakusanya jeshi lake lote na kumvamia Isreli huko jangwani. Akaja kwa Jahazi, ambapo alipigana dhidi ya Israeli.
24 And Israel smote him with the edge of the sword, and took possession of his land from Arnon unto Yabbok, even unto the children of 'Ammon; for the border of the children of 'Ammon was strong.
Israeli akalivamia jeshi la Sihoni na nchi ya upanga na kuchukua nchi yao kutoka Amon mpaka mto Jabboki, hadi kufikia nchi ya watu wa Amoni. Sasa mpaka wa watu wa Amoni ulikuwa umefungwa.
25 And Israel took all these cities; and Israel dwelt in all the cities of the Emorites, in Cheshbon, and in all the villages thereof.
Israeli akachukua miji yote ya Waamori na akaishi ndani yake, pamoja na Heshiboni na vijiji vyake wote.
26 For Cheshbon was the city of Sichon the king of the Emorites; and he had fought against the former king of Moab, and taken all his land out of his hand, up to the Arnon.
Heshiboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye hapo awali alipigana dhidi ya mfalme wa kwanza wa Moabu. Sihoni alikuwa ameteka ardhi yake yote toka mipaka yake mpaka mto wa Amoni.
27 Therefore said the poets, Come into Cheshbon, let the city of Sichon be built and established.
Hiyo ndiyo sababu wala ambao huongea kwa Mitahali husema, “Njoni Heshboni. Mji wa Sihoni ujengwe na kuimarishwa tena.
28 For a fire is gone out of Cheshbon, a flame from the city of Sichon: it hath consumed 'Ar-Moab, the men of the high places of the Arnon.
Moto uliwaka toka Heshiboni, moto kutoka mji wa Sihoni ambao uliiteketeza Ari ya Moabu, na wenyeji wa miji ya juu ya Amoni.
29 Woe to thee, Moab! thou art lost, O people of Kemosh: he hath suffered his sons to become fugitives, and his daughters to go into captivity, unto the king of the Emorites, Sichon.
Ole wako, Moabu! umepotea, enyi watu wa Chemoshi. Amewafanya watu wake kuwa wakimbizi na binti zake kuwa wafungwa wa Sihoni mfalme wa Waamori.
30 We have thrown them down; lost is Cheshbon even unto Dibon, and we have laid waste [all] up to Nophach, which reacheth unto Medeba.
Lakini tumempiga Sihoni. Tumeiangsmiza Heshibon mpaka Diboni. Tumewaharibu wote mpaka Nofa, ambayo inafika mpaka Madeba.”
31 Thus Israel dwelt in the land of the Emorites.
Kwa hiyo Israeli akaanza kuishi katika nchi ya Waamori,
32 And Moses sent to spy out Ya'zer, and they captured the villages thereof, and drove out the Emorites that were there.
Kisha Musa akatuma watu kwenda kuingalia Yaziri. Waliviteka vijiji vyake na kuwafukuza Waamori waliokuwa wakiishi humo.
33 And they turned and went up by the way to Bashan; and 'Og, the king of Bashan, went out against them, he, and all his people, to the battle at Edrei.
Kisha wakageuka na kuelekea njia inayoelekea Bashani. Ogu mfalme wa Bashani akatofautiana nao, yeye na Jeshi lake lote, ili apigane nao kule Ederei.
34 And the Lord said unto Moses, Fear him not; for into thy hand have I delivered him, and all his people, and his land; and thou shalt do unto him as thou hast done unto Sichon, the king of the Emorites, who dwelt at Cheshbon.
Kisha BWANA akasema na Musa, “Msimwogope, kwa sababu nimewapeni ushindi dhidi yake, Jeshi lake lote na nchi yake. Mfanyeni kama mlivyomfanya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akiishi Heshiboni.”
35 And they smote him and his sons, and all his people, until there was none left unto him that escaped; and they took possession of his land.
Kwa hiyo wakamuua, na wanawe, na jeshi lake lote, mpaka wote wakaishi na hakubaki hata mmoja aliyebaki hai. Kisha wakaichukua nchi yake.

< Numbers 21 >