< Numbers 11 >

1 And it came to pass that as the people complained in a manner displeasing in the ears of the Lord, the Lord heard it, and his anger was kindled, and the fire of the Lord burnt among them, and consumed at the uttermost part of the camp.
Sasa watu wakanung'unika juu ya matatizo yao wakati BWANA alipokuwa akiwasikiliza. BWANA akawasikia watu naye akakasirika. Moto kutoka kwa BWANA ukashuka na ukawaka kati yao na kuteketeza baadhi ya kambi kwenye pembe zake.
2 And the people then cried unto Moses; and Moses prayed unto the Lord, and the fire disappeared.
Ndipo watu wakamwita Musa kwa nguvu, Naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukazimika.
3 And he called the name of the place Tab'erah; because the fire of the Lord had burnt among them.
Mahali pale paliitwa Tabera, kwa sababu moto wa BWANA uliwaka kati yao.
4 And the mixed multitude that was among them felt a lustful longing: and the children of Israel also wept again, and said, Who will give us flesh to eat?
Baadhi ya wageni wakaanza kuweka kambi zao pamoja na wana wa wa Israeli. Walitaka kula chakula kizuri. Kisha wana wa Israeli walipoanza kulia wakisema, “Ni nani atakayetupatia nyama za kula?
5 We remember the fish, which we could eat in Egypt for naught; the cucumbers, and the melons, and the leeks, and the onions, and the garlic;
Tunakumbuka samaki tulizokula bure kule Misri, yale matango, na matikiti maji, na mboga na vitunguu na vitunguu saumu.
6 But now our soul is faint: there is nothing at all, only to the manna are our eyes [directed].
Na sasa hatuna hamu ya kula, kwa sababu tunaona mana tu.
7 But the manna was like coriander-seed, and its color as the color of the bdellium.
Mana ilifanana na punje ya mtama. ilionekana kama bedola.
8 The people went about and gathered it, and ground it in a mill, or pounded it in a mortar, and boiled it in a pot, or made cakes of it: and its taste was as the taste of cakes mixed with oil.
watu wakazunguka kisha wakakusanyika. Wakaisaga, wakaitwanga kwa vinu, wakaitokosa nyunguni, na kuitengeneza mikate. radha yake ilikuwa kama mafuta mapya ya mizeituni.
9 And when the dew fell upon the camp in the night, the manna fell upon it.
Na umande ulipoanguka kambini usiku ule, na mana ilianguka pia.
10 And Moses heard the people weep according to their families, every man at the door of his tent: and the anger of the Lord was kindled greatly; and in the eyes of Moses also was it displeasing.
Musa akawasikia watu wakilia katika familia zao, na kila mtu alikuwa kwenye lango la hema yake. BWANA alikasirika sana, na mbele ya macho ya Musa malalamiko yao yalikuwa mabaya.
11 And Moses said unto the Lord, Wherefore hast thou done evil to thy servant? and wherefore have I not found favor in thy eyes, that thou layest the burden of all this people upon me?
Musa akasema na BWANA, “Kwa nini umemtendea mtumishi wako vibaya namna hiyo? kwa nini hujapendezwa na mimi? unanifanya kubeba mizigo ya hawa watu.
12 Was it I who have conceived all this people? or was it I who have begotten them? that thou shouldst say unto me, Carry them in thy bosom, as a nursing father beareth the sucking child, unto the land which thou hast sworn unto their fathers?
Je, mimi ndiye niliyewatungia mimba hawa watu? Mimi ndiye niliyewazaa kiasi kwamba unaniambia, “wabebe kwa ukaribu vifuani mwako kama baba abebavyo mtoto wake? Je, nitawabeba mpaka kwenye nchi ambayo uliwaahidi mababu zao kuwapa?
13 Whence shall I obtain flesh to give unto all this people? for they weep around me, saying, Give us flesh, that we may eat.
Naweza kupata wapi nyama za kuwapa watu wote hawa? Wanalia mbele zangu na wanasema, 'tupe nyama tule.'
14 I am not able by myself alone to bear all this people, because it is too heavy for me.
Mimi peke yangu siwezi kuwabeba watu wote hawa. Ni wengi sana kwangu.
15 And if thou wilt thus deal with me, then slay me, I pray thee, at once, if I have found favor in thy eyes: that I may not see my wretchedness.
Kwa vile unanitendea hivi, basi uniue, na kama wewe ni mpole kwangu, basi niondolee mzigo huu.”
16 And the Lord said unto Moses, Gather unto me seventy men of the elders of Israel, whom thou knowest to be the elders of the people, and its officers; and take them unto the tabernacle of the congregation, and they shall stand there with thee.
BWANA akamwambia Musa, “Niletee wazee sabini miongoni mwa Waisraeli. Hakikisha ni wazee na viongozi wa watu. Uwalete kwenye hema ya kukutania wasimame pamoja na wewe.
17 And I will come down and speak with thee there: and I will take some of the spirit which is upon thee, and I will put it upon them; and they shall bear with thee the burden of the people, and thou shalt not bear it by thyself alone.
Nami nitashuka niseme nawe mahali pale. Nitatoa sehemu ya roho iliyo ndani yako na kuwapatia wao. Nao watabeba mzigo wa watu pamoja nawe. na hautaubeba peke yako.
18 And unto the people shalt thou say, Hold yourselves ready against tomorrow, that ye may eat flesh; for ye have wept in the ears of the Lord, saying, Who shall give us flesh to eat? for it was better with us in Egypt: thus will the Lord give you flesh, and ye shall eat.
Waambie watu, 'Jitakaseni ninyi wenyewe, kwa kuwa kesho mtakuala nyama, kwa kuwa mmelia na BWANA amesikia, “Mlipokuwa mkisema kuwa nani atakayetupa nyama tule? Kule Misri tulikula chakula kizuri!” Kwa hiyo BWANA atawapeni nyama, nanyi mtakula nyama.
19 Not one day shall ye eat, nor two days, nor five days, nor ten days, nor twenty days;
Hamtakula nyama kwa siku moja tu, au siku mbili, au siku tano, au siku kumi, au siku ishirini,
20 But up to a full month, until it come out at your nostrils, and it become loathsome unto you; because that ye have despised the Lord who is in the midst of you, and ye have wept before him, saying, Why did we come forth out of Egypt?
Lakini mtakula nyama kwa mwezi mmoja mpaka zitakapowatokea puani. Mpaka zitawakinai kwa sababu mmemkataa BWANA ambaye yuko kati yenu. Mmelia mbele yake. mmesema, “Kwa nini tulitoka Misri?””
21 And Moses said, Six hundred thousand men on foot is the people, in the midst of whom I am; and yet thou hast said, Flesh will I give them, that they may eat a whole month.
Kisha Musa akasema, “Mimi nina watu 600, 000, na wewe umesema, “Nitawapa nyama mle kwa mwezi mmoja,'
22 Shall flocks and herds be slain for them, that they may suffice for them? or shall all the fish of the sea be gathered together for them, that they may suffice for them?
Je, tutayachinja haya makundi ya ng'ombe na kondoo ili kuwatosheleza?”
23 And the Lord said unto Moses, Should the Lord's hand be too short? now shalt thou see whether my word shall come to pass unto thee or not.
BWANA akasema na Musa, “Je mkono wangu ni mfupi? Sasa utaona kama maneno yangu ni ya kweli ama sivyo.
24 And Moses went out, and spoke to the people the words of the Lord; and he assembled seventy men from the elders of the people, and placed them round about the tabernacle.
Musa alitoka nje kwenda kuwaambia watu maneno ya BWANA. Aliwakusanya wazee sabini wa watu na kuwaweka kuizunguka hema.
25 And the Lord came down in a cloud and spoke unto him; and he took some of the spirit that was upon him, and put it upon the seventy men, the elders: and it came to pass, that, when the spirit rested upon them, they prophesied, but they did not so any more.
BWANA akashuka chini katika wingu akaongea na Musa. BWANA akachukua sehemu ya roho iliyokuwa kwa Musa na kuiweka kwa wale wazee sabini. Roho alipowashukia, wakaanza kutoa unabii, lakini ilitokea kwenye tukio hilo tu na haikujirudia tena.
26 And there remained two men in the camp, the name of the one was Eldad, and the name of the other Medad; and the spirit rested upon them; and they were of those that were written down, but they had not gone out unto the tabernacle: and they prophesied in the camp.
Watu wawili waitwao Elidadi na Medadi walibaki kambini. Lakini Roho aliwashukia pia. Majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye orodha lakini walikuwa hawajaenda hemani. Hata hivyo nao walitoa unabii wakiwa kambini.
27 And there ran a young man, and told to Moses, and said, Eldad and Medad are prophesying in the camp.
Kijana mmoja huko kambini alikimbia akaenda kumwambia Musa, “Elidadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
28 And Joshua the son of Nun, the servant of Moses from his youth, answered and said, My Lord Moses, forbid them.
Joshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Musa, ambaye ni miongoni mwa wale aliowachagua akamwambia Musa, “Bwana wangu Musa, wazuie.”
29 And Moses said unto him, Art thou zealous for my sake? And oh that one might render all the people of the Lord prophets, that the Lord would put his spirit upon them!
Musa akamwambia, “una wivu kwa niaba yangu? Natamani kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kwamba angeweka Roho yake juu yao wote!”
30 And Moses retired back into thy camp, he with the elders of Israel.
Kisha Musa na wale wazee wakarudi kambini.
31 And a wind went forth from the Lord, and drove up quails from the sea, and scattered them over the camp, about a day's journey on this side, and about a day's journey on the other side, round about the camp, and about two cubits high over the face of the earth.
Kisha upepo ukavuma kutoka kwa BWANA ukaja na kware kutokea baharini. Wakaanguka karibu na kambi, kiasi cha umbali wa safari ya siku moja upande huu na umbali wa siku moja upande mwingine. Wale kware wakaizunguka kambi kiasi cha mita moja toka uso wa dunia.
32 And the people arose all that day, and all that night, and all the following day, and they gathered the quails; he that had taken the least, had gathered ten chomers: and they spread them out for themselves round about the camp.
Watu wakawakusanya hao kware kwa bidii mchana huo wote na usiku huo wote, na mchana wote uliofuatia. Hakuna aliyekusanya pungufu ya mita mbili za uajazo. Wakawaanika kweye ardhi yote hapo kambini.
33 The flesh was yet between their teeth, it was not yet chewed: when the wrath of the Lord was kindled against the people, and the Lord smote among the people a very great plague.
Wakati ile nyama ikiwa bado iko kwenye meno yao, wakiwa bado wanatafuna, BWANA akawakasirikia. Akwapiga watu wale kwa gonjwa kubwa sana.
34 And he called the name of that place Kibroth-hattaavah; because there they buried the people that had lustfully craved.
Mahali pale paliitwa Kibroti Hataava, kwa sababu pale walizika watu waliotamani nyama.
35 From Kibroth-hattaavah the people journeyed unto Chazeroth; and they remained at Chazeroth.
Kutoka Kibroti Hataava watu wakasafiri hadi Hazeroti, ambapo walipumzika.

< Numbers 11 >