< Nehemiah 9 >

1 And on the twenty and fourth day of this month were the children of Israel assembled with fasting, and in sackclothes, and with earth upon them.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
2 And the seed of Israel separated themselves from all children of the strangers: and they stood forward and made confession for their sins, and the iniquities of their fathers.
Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
3 And they stood up in their standing-place, and read in the book of the law of the Lord their God the fourth part of the day; and another fourth part they made confession, and prostrated themselves before the Lord their God.
Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
4 Then stood up upon the stairs of the Levites, Jeshua' and Bani, Kadmiel, Shebanyah, Bunni, Sherebyah, Bani, and Kenani, and they cried with a loud voice unto the Lord their God.
Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
5 Then said the Levites, Jeshua', and Kadmiel, Bani, Chashabneyah, Sherebyah, Hodiyah, Shebanyah, and Pethachyah, Arise! bless ye the Lord your God from eternity to eternity. And let men bless thy glorious name, which is exalted above all blessing and praise.
Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
6 Thou indeed art the Eternal One alone: It is thou that hast made the heavens with all their host, the earth, and all that is upon her, the seas, and all that is in them, and thou givest life to them all; and the host of the heavens bow down before thee.
Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
7 Thou art indeed the Lord the [true] God, who didst choose Abram, and bring him forth out of Ur of the Chaldeans, and change his name to Abraham;
“Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
8 And thou didst find his heart faithful before thee: and thou madest with him the covenant to give the land of the Canaanites, the Hittites, the Emorites, and the Perizittes, and the Jebusites, and the Girgashite—to give it to his seed: and thou hast performed thy words; for thou art righteous.
Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 And thou didst see the affliction of our fathers in Egypt, and their cry didst thou hear by the Red Sea;
“Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
10 And thou didst display signs and wonders on Pharaoh, and on all his servants, and on all the people of his land: for thou knewest that they had dealt presumptuously against them; and thou didst [thus] make thyself a name, as it is this day.
Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
11 And the sea didst thou divide before them, so that they passed through the midst of the sea on dry land; and their pursuers didst thou throw into the deeps, like a stone in mighty waters.
Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
12 And by a pillar of cloud didst thou lead them in the day, and by a pillar of fire in the night, to give light unto them on the way whereon they should go.
Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
13 Also on mount Sinai camest thou down, and spokest with them from heaven; and thou gavest them upright ordinances, and truthful laws, good statutes and commandments;
“Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
14 And thy holy sabbath madest thou known unto them, and commandments, statutes, and a law didst thou enjoin on them, by the hand of Moses thy servant.
Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
15 And bread from heaven didst thou give them for their hunger, and water out of the rock broughtest thou forth for them for their thirst; and thou didst order them to go in to take possession of the land concerning which thou hadst lifted up thy hand to give it unto them.
Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
16 And they and our fathers acted presumptuously, and hardened their neck, and hearkened not to thy commandments.
“Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
17 And they refused to obey, and remembered not thy marvelous deeds which thou hadst done with them; but they hardened their neck, and [spoke of] appointing a chief to return to their bondage, in their rebellion; but thou art a God ready to pardon, gracious and merciful, long-suffering, and abundant in kindness, and forsookest them not.
Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
18 Yea, although they had made for themselves a molten calf, and said, 'This is thy god that hath brought thee up out of Egypt,' and had practised great provocations:
hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
19 Yet in thy abundant mercies didst thou not forsake them in the wilderness: the pillar of cloud departed not from them by day, to lead them on the way; nor the pillar of fire by night, to give them light on the way whereon they should go.
“Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
20 And thy good spirit thou gavest to make them intelligent, and thy manna thou withheldest not from their mouth, and water thou gavest them for their thirst.
Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
21 And forty years didst thou provide for them in the wilderness; they lacked nothing; their clothes did not wear out; and their feet swelled not.
Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
22 Thou gavest them also kingdoms and nations, which thou didst divide into various corners: and they took possession of the land of Sichon, even the land of the king of Cheshbon, and the land of 'Og the king of Bashan.
“Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
23 And their children didst thou multiply like the stars of heaven, and then broughtest them into the land, concerning which thou hadst ordered their fathers to enter in to take possession of it.
Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
24 And the children entered in and took possession of the land; and thou didst humble before them the inhabitants of the land, the Cana'anites, and gavest them up into their hands, with their kings, and the nations of the land, that they might do with them according to their pleasure.
Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
25 And they captured fortified cities, and a fat soil; and they took possession of houses full of all good things, hewn-out wells, vineyards, and olive-yards, and fruit trees in abundance; and they ate, and were satisfied, and became fat, and delighted themselves in thy great goodness.
Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
26 Then became they disobedient, and rebelled against thee, and cast thy law behind their back, and they slew thy prophets who had warned them to bring them back unto thee, and they practised great provocations.
“Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
27 Thereupon thou gavest them up into the hand of their adversaries, who oppressed them: and in the time of their distress they used to cry unto thee, and thou ever heardest them from heaven; and according to thy abundant mercies thou wast wont to give them helpers, who helped them out of the hand of their adversaries.
Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
28 But when [once more] they had rest, they did again evil before thee: wherefore thou didst leave them in the hand of their enemies, so that they had dominion over them; and when they returned, and cried unto thee, thou wast wont to hear them from heaven, and thou didst ever deliver them according to thy mercies many times.
“Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
29 And thou gavest them warning to bring them back unto thy law: yet they acted presumptuously, and hearkened not unto thy commandments, and sinned against thy ordinances, which a man is to do that he may live through them: and they rendered their shoulder rebellious, and hardened their neck, and would not hear.
“Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
30 Yet thou gavest them indulgence many years, and didst warn them through thy spirit by means of thy prophets; but they gave no ear: therefore didst thou give them up into the hand of the nations of the lands.
Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
31 Yet in thy abundant mercies hast thou not made an entire end of them, and thou hast not forsaken them; for a gracious and merciful God art thou.
Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
32 And now, our God, the great, the mighty, and the terrible God, who keepest the covenant and kindness, let not be esteemed as little before thee all the hardship that hath befallen us, on our kings, on our princes, and on our priests, and on our prophets, and on our fathers, and on all thy people, from the days of the kings of Assyria until this day.
“Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
33 Nevertheless thou art righteous in all that is come over us; for thou hast acted [according to] truth, but we have done wickedly.
Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
34 Also our kings, our priests, and our fathers have not executed thy law, and have not listened unto thy commandments and thy testimonies, wherewith thou didst warn them.
Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
35 But they in their kingdom, and in thy abundant goodness which thou hadst given unto them, and in the ample and fat land which thou hadst given up before them, did indeed not serve thee, and they turned not away from their wicked deeds.
Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
36 Behold, we are this day servants: and as regardeth the land that thou gavest unto our fathers to eat its fruit and its good things, behold, we are servants in it;
“Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
37 And it yieldeth its products in abundance for the kings whom thou hast set over us because of our sins; also over our bodies have they dominion, and over our cattle [also] at their pleasure, and we are in great distress.
Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
38 And because of all this, we make a faithful covenant, and write it down; and on the sealed document are our princes, our Levites, and our priests.
“Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”

< Nehemiah 9 >