< Leviticus 5 >

1 And if any person sin, because he heareth the voice of adjuration, and he is a witness, since he hath either seen or knoweth something; if he do not tell it, and thus bear his iniquity;
Kama mtu atatenda dhambi kwa sababu hakusema ukweli wakati alipotakiwa kutoa ushahidi fulani kuhusu kile alichotakiwa, ameona au kufahamu habari zake, yeye anastahili adhabu.
2 Or if there be a person who toucheth any unclean thing, whether it be the carcass of an unclean beast, or the carcass of unclean cattle, or the carcass of an unclean creeping thing, and it escape his recollection; but [he becometh aware that] he is unclean, and hath [thus] incurred guilt;
Au mtu akigusa kitu chochote ambacho Mungu amekitaja kuwa ni najisi hata kama ni mzoga wa wanyama wa porini au ni mzoga wa wanyama wa kufugwa au wataambaao hata kama mtu huyo hakukusudia kumgusa, yeye ni najisi na mwenye hatia.
3 Or if he touch the uncleanness of man, whatsoever uncleanness of the kind it be by which he can be defiled, and it escape his recollection; but he becometh aware of it, and [that] he hath [thus] incurred guilt;
Au amegusa kitu chochote kilicho kichafu, kwa vyovyote kama hakujua, ndipo atakuwa na hatia akijua vile.
4 Or if any person swear, by pronouncing with his lips to do evil, or to do good [to himself], in whatsoever it be that a man pronounceth with an oath, and it escape his recollection; but he becometh aware of it that he hath incurred guilt by any one of these:
Au kama yeyote akiapa bila kufikiri kwa midomo yake kufanya ubaya, au kufanya vyema kwa vyovyote vile mtu ameapa kwa haraka atakapotambua atakuwa na hatia kwa vitu hivyo.
5 And it shall be, if he have incurred guilt by any one of these [things, ] that he shall confess that concerning which he hath sinned;
Mtu yeyote akiwa na hatia kwa vitu hivi, lazima akiri kwa yoyote dhambi aliyotenda.
6 And he shall bring his trespass-offering unto the Lord for his sin which he hath committed, a female from the flocks, a sheep or a goat, for a sin-offering; and the priest shall make an atonement for him concerning his sin.
Ndipo atakapoleta sadaka yake ya hatia mbele za Bwana kwa dhambi aliyokwisha tenda. Ataleta kondoo jike au mbuzi kutoka katika kundi lake kuwa matoleo ya dhambi, kuhani atafanya upatanisho kuhusu dhambi yake.
7 And if his means be not sufficient for a sheep, then shall he bring as his offering [for the trespass] which he hath committed, two turtle-doves, or two young pigeons, unto the Lord; one for a sin-offering, and the other for a burnt-offering.
Kama hataweza kununua mwana kondoo ataleta kama sadaka ya hatia, hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana, mmoja kwa sadaka ya dhambi na mwingine ni sadaka ya kutekeketezwa.
8 And he shall bring them unto the priest, and he shall offer that which is for the sin-offering first, and pinch off its head by the back of its neck, but shall not divide it asunder:
Atawaleta kwa kuhani, wa kwanza atatoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo yake lakini ataacha kichwa chake kinaning'inia wala hataiondoa kabisa shingo yake katika mwili.
9 And he shall sprinkle some of the blood of the sin-offering upon the wall of the altar: and the rest of the blood shall be wrung out at the bottom of the altar; it is a sin-offering.
Ndipo atanyunyizia damu yake katika sehemu za madhabahu, na damu inayobaki ataimwaga chini ya madhabahu. Hii ni dhabihu ya dhambi.
10 And the second shall he prepare as a burnt-offering, according to the prescribed order; and the priest shall make an atonement for him for his sin which he hath committed, and it shall be forgiven unto him.
Ndipo ataoa ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kama ilivyoelekezwa, na kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi alizokwisha kufanya, na huyo mtu atakuwa amesamehewa.
11 But if his means be not sufficient for two turtle-doves, or two young pigeons, then shall he bring as his offering for that which he hath sinned, the tenth part of an ephah of fine flour for a sin-offering; he shall not put upon it any oil, nor shall he put thereupon any frankincense; for it is a sin-offering.
Lakini kama hataweza kununua hua wawili au makinda ya njiwa mawili, ndipo ataleta kama dhabihu ya dhambi zake sehemu ya kumi ya unga laini kama sadaka ya dhambi. Asiweke mafuta wala ubani juu yake, kwa kuwa ni sadaka ya dhambi.
12 And he shall bring it to the priest; and the priest shall take from it his handful, as its memorial, and burn it on the altar, upon the fire-offerings of the Lord: it is a sin-offering.
Atauleta kwa kuhani, na kuhani atachukua konzi moja ya unga kama ukumbusho wa wema wa Bwana na atauweka juu ya madhabahu na kuteketeza juu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
13 And the priest shall make an atonement for him concerning his sin that he hath committed in one of these, and it shall be forgiven unto him; and it shall belong to the priest, as the meat-offering.
Kuhani atafanya upatanisho kwa dhambi yoyote aliyofanya mtu yeyote, mtu huyo atasamehewa. Na sadaka inayobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyo sadaka ya nafaka.'”
14 And the Lord spoke unto Moses, saying,
Bwana akamwambia Musa, akasema,
15 If any person commit a trespass, and sin through ignorance, against the holy things of the Lord: then shall he bring as his trespass-offering unto the Lord a ram without blemish out of the flocks, in value of two shekels of silver, after the shekel of the sanctuary, for a trespass-offering.
“Kama mtu akikiuka amri na kufanya dhambi kinyume na mambo matakatifu ya Bwana, lakini akifanya bila kukusudia ataleta sadaka ya hatia kwa Bwana. Sadaka hii itakuwa ni kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi; thamani yake halisi kifedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kama sadaka ya hatia.
16 And that, in which he hath sinned against the holy thing, shall he pay, and shall add its fifth part thereto, and give it unto the priest; and the priest shall make an atonement for him with the ram of the trespass-offering, and it shall be forgiven unto him.
Lazima atalipa kwa Bwana kwa kile alichokosa kulingana na kitakatifu, na ataongezea moja ya tano na kumpa kuhani. Ndipo kuhani ataweka upatanisho kwa ajili yake pamoja na kondoo wa sadaka ya hatia, na mtu atakuwa amesamehewa.
17 And if any person sin, and commit any one of the prohibitions of the Lord which ought not to be done; and he know not whether he have incurred guilt, and so bear his iniquity:
Kama mtu akitenda dhambi kwa kufanya kile ambacho Bwana aliagiza kisifanyike, hata kama hakujuwa, atakuwa na hatia na ataibeba hatia yake.
18 Then shall he bring a ram without blemish out of the flocks, of the usual value, for a trespass-offering, unto the priest: and the priest shall make an atonement for him concerning his sin of ignorance, wherein he hath erred and knoweth it not, and it shall be forgiven unto him.
Lazima ataleta kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi, anayestahili thamani ya fedha, kama sadaka ya hatia kwa kuhani. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kulingana na dhambi aliyotenda, ambayo hakujua atakuwa amesamehewa.
19 It is a trespass-offering: he hath in trespassing trespassed against the Lord.
Ni sadaka ya hatia, na amekuwa na hatia mbele za Bwana.”

< Leviticus 5 >