< Leviticus 15 >
1 And the Lord spoke unto Moses and to Aaron, saying,
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
2 Speak unto the children of Israel, and say unto them, When any man have a running issue out of his flesh: because of his issue is he unclean.
“Waambie watu wa Israeli, na sema kwao, 'Wakati mtu yeyote kisonono kimemwathiri mwili wake unatoa ugiligili, anakuwa najisi.
3 And this shall be his uncleanness in his issue: whether his flesh run with his issue, or his flesh be stopped from his issue, it is his uncleanness.
Unajisi wake unatokana na athari ya kisonono. Iwe mwili wake unatoa ugiligili au umekoma, huo ni unajisi.”
4 Every bed, whereon he may lie that hath the issue, shall be unclean: and every vessel, whereon he may sit, shall be unclean.
Kitanda chochote anachokilalia kitakuwa najisi, na kila kitu ambacho anakaa juu yake kitakuwa najisi.
5 And any man that toucheth his bed shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na awe amenajisika mpaka jioni.
6 And he that sitteth on any vessel whereon he that hath the issue may sit, shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Yeyote anayekaa katika kitu chochote ambacho mtu ambaye ameathiriwa na kisonono alikaa, mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
7 And he that toucheth the flesh of him that hath the issue shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Na yeyote anayegusa mwili wa ambaye ameathirika na kisonono lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na awe najisi hadi jioni.
8 And if he that hath the issue spit upon him that is clean: then shall this one wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Kama mtu ambaye anaona majimaji kama hayo kwa mtu fulani ambaye ametakasika, ndipo mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na atakuwa najisi hata jioni.
9 And what saddle soever he that hath the issue may ride upon shall be unclean.
Tandiko lolote ambalo ambaye anamajimaji ya kisonono atalikalia litakuwa najisi.
10 And whatsoever toucheth any thing, that may be under him, shall be unclean until the evening: and he that beareth any of these things shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Yeyote anayegusa kitu chochote kilichokuwa chini ya mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji; atanajisika mpaka jioni.
11 And whomsoever he that hath the issue may touch, and he have not rinsed his hands in water, shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Ambaye anamajimaji kama hayo akimgusa kabla kwanza ya kuosha kwa maji safi mikono yake, mtu aliyeguswa lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
12 And an earthen vessel that he who hath the issue may touch, shall be broken; and every vessel of wood shall be rinsed in water.
Chungu chochote cha udongo ambacho ambaye anamajimaji kama hayo akigusa lazima kivunjwe, na kila chombo cha mti lazima kioshwe na maji safi.
13 And when he that hath an issue becometh clean of his issue: then shall he number to himself seven days for his cleansing, and wash his clothes, and bathe his flesh in running water, and then shall he be clean.
Wakati mwenye kisonono anapotakaswa katika kisonono chake, ndipo lazima ahesabu kwaajili yake siku saba kwaajili ya kutakasika kwake; ndipo afue nguo na aoshe mwili wake kwenye maji yatiririkayo. Ndipo atakuwa safi.
14 And on the eighth day shall he take unto himself two turtle-doves, or two young pigeons, and come before the Lord, unto the door of the tabernacle of the congregation, and give them unto the priest:
Katika siku ya nane lazima achukue njiwa wawili au kinda mbili za njiwa na aje mbele za Yahwe pakuingilia kwenye hema ya mkutano; pale lazima atoe hao ndege kwa kuhani.
15 And the priest shall offer them, the one for a sin-offering, and the other for a burnt-offering; and the priest shall make an atonement for him before the Lord for his issue.
Lazima kuhani awatoe, moja kama sadaka ya dhambi na nyingine kama ya kuteketezwa, na kuhani lazima afanye upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe kwaajili ya kisonono chake.
16 And if any man's seed of copulation go out from him, then shall he bathe all his flesh in water, and be unclean until the evening.
Kama mtu yeyote ametokwa na shahawa, ndipo lazima aoge mwili wake wote katika maji; atanajisika mpaka jioni.
17 And any garment, and any skin, whereon the seed of copulation may be, shall be washed with water, and be unclean until the evening.
Kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa lazama paoshwe kwa maji; itakuwa najisi mpaka jioni.
18 And if a man should lie with a woman with seed of copulation, then shall they bathe themselves in water, and be unclean until the evening.
Na kama mwanamke na mwanaume watalala pamoja na kunakutokwa kwa shahawa kwenda kwa mwanamke, lazima wote wawili waoge katika maji; watakuwa najisi mpaka jioni.
19 And if a woman have an issue, so that blood flow from her flesh: then shall she be in her state of separation seven days; and whosoever toucheth her shall be unclean until the evening.
Mwanamke anapokuwa kwenye hedhi, ataendelea kunajisika kwa siku saba, na yeyote anayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 And every thing that she may lie upon in her separation shall be unclean: and whatever she may sit upon shall be unclean.
Chochote anacholala juu yake wakati wa hedhi kitakuwa najisi; kila kitu ambacho anakalia kitakuwa pia najisi.
21 And whosoever toucheth her bed shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
22 And whosoever toucheth any vessel, that she may sit upon, shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Yeyote anayegusa chochote ambacho amekikalia lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo anakuwa najisi mpaka jioni.
23 And if something be on the bed, or on any thing whereon she may sit, when he toucheth it, he shall be unclean until the evening.
Iwe juu ya kitanda au kitu chochote juu ya popote atakapokaa, kama akikigusa, mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
24 And if any man should lie with her, and the uncleanness of her separation come upon him, he shall be unclean seven days; and every bed whereon he may lie shall be unclean.
Kama mwanaume yeyote akilala naye, na unajisi wa mwanamke ukamgusa, atakuwa amenajisika siku saba. Kila kitanda ambacho anakilalia mwanaume huyo kitanajisika.
25 And if a woman have an issue of her blood many days out of the time of her separation, or if it run beyond the time of her separation: all the days of the issue of her uncleanness shall she be as in the days of her separation; she shall be unclean.
Kama mwanamke ametokwa damu kwa siku nyingi ambayo siyo kipindi cha hedhi yake, au ikitoka zaidi ya kipindi chake cha hedhi, wakati wote wa siku za kunajisika, atakuwa kama alikuwa kwenye siku zake za hedhi. Yeye ni najisi.
26 Every bed whereon she may lie all the days of her issue shall be unto her as the bed of her separation; and whatever vessel she may sit upon shall be unclean, as the uncleanness of her separation.
Kila kitanda anachokilalia wakati wote wa kutokwa damu itakuwa kwake sawa tu kama kitanda anacholalia wakati wa hedhi, na kila kitu ambacho anakalia kitakuwa najisi, kama tu unajisi wa hedhi yake.
27 And whosoever toucheth these things shall be unclean; and he shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the evening.
Na yeyote anayegusa kitu kati ya vitu hivyo atakuwa najisi; lazima yeye afue nguo zake na aoge mwenyewe kwenye maji, na atakuwa amenajisika mpaka jioni.
28 And when she becometh clean of her issue, then shall she number to herself seven days, and after that shall she be clean.
Lakini kama mwanamke ametakasika katika kutokwa na damu, ndipo atahesabu kwaajili yake siku saba, baada ya hizo atakuwa safi.
29 And on the eighth day shall she take unto herself two turtle-doves, or two young pigeons, and bring them unto the priest, to the door of the tabernacle of the congregation.
Katika siku ya nane atachukua kwake njiwa wawili au kinda wawili wa njiwa na atawaleta kwa kuhani pakuingilia hema ya mkutano.
30 And the priest shall offer the one for a sin-offering, and the other for a burnt-offering; and the priest shall make an atonement for her before the Lord for the issue of her uncleanness.
Huyo kuhani atatoa ndege mmoja kama sadaka ya dhambi na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa, na atafanya upatanisho kwaajili ya huyo mbele ya Yahwe kwaajili unajisi wa mwanamke atokwaye damu.
31 And ye shall separate the children of Israel from their uncleanness; that they may not die in their uncleanness, when they defile my tabernacle that is in their midst.
Hivi ndivyo lazima uwatenge watu wa Israeli katika unajisi wao, hivyo hawatakufa tokana na unajisi wao, kwa kuchafua hema langu, ambapo naishi kati yao.
32 This is the law of him that hath an issue, and of him whose seed goeth from him, and is defiled therewith;
Huu ndio utaratibu kwa kila ambaye anakisonono, kwaajili kila mwanaume ambaye shahawa yake inatoka na inamfanya kuwa najisi,
33 And of her that is suffering in her separation, and of him that hath an issue, of the man, and of the woman, and of him that lieth with her that is unclean.
kwaajili ya mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha hedhi, kwaajili ya yeyote aliye na kisonono, awe mwanaume au mwanamke, na kwaajili ya yeyote anayelala na mwanamke najisi.