< Joshua 7 >
1 But the children of Israel committed a trespass on the devoted things; for 'Achan, the son of Carmi, the son of Zabdi, the son of Zerach, of the tribe of Judah, took of the devoted things: and the anger of the Lord was kindled against the children of Israel.
Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
2 And Joshua sent men from Jericho to 'Ai, which is beside Beth-aven, on the east side of Beth-el, and said unto them, thus, Go up and spy out the country. And the men went up and spied out 'Ai.
Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
3 And they returned to Joshua, and said unto him, Let not all the people go up; but let about two or three thousand men go up and smite 'Ai: do not fatigue all the people [to go] thither; for they are but few.
Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
4 So there went up thither of the people about three thousand men; and they fled before the men of 'Ai.
Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
5 And the men of 'Ai smote of them about thirty and six men; and they chased them from before the gate unto the stone-quarries, and smote them on the declivity [of the hill]; wherefore the heart of the people melted, and became as water.
Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
6 And Joshua rent his clothes, and fell upon his face to the earth before the ark of the Lord until the evening, he with the elders of Israel, and they put dust upon their head.
Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
7 And Joshua said, Alas, O Lord Eternal, wherefore hast thou caused this people to pass over the Jordan, to deliver us into the hand of the Emorites, to destroy us? and oh! that we had been content, and dwelt on the other side of the Jordan!
Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
8 I pray thee, O Lord, what shall I say, since Israel have turned their back before their enemies!
Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
9 And when the Canaanites and all the inhabitants of the land will hear of it, they will environ us round, and cut off our name from the earth; and what wilt thou do for thy great name?
Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
10 And the Lord said unto Joshua, Get thee up; wherefore liest thou upon thy face.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
11 Israel hath sinned, and they have also transgressed my covenant which I have commanded them; and they have also taken of the devoted things, and have also stolen, and have also dissembled, and they have also put it into their own vessels.
Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
12 Therefore will the children of Israel not be able to stand up before their enemies; their back will they turn before their enemies, because they have become accursed: I will not be any more with you, except ye destroy the accursed from among you.
Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
13 Rise up, sanctify the people, and say, Sanctify yourselves against tomorrow; for thus hath said the Lord the God of Israel, An accursed thing is in the midst of thee, O Israel: thou shalt not be able to stand up before thy enemies, until ye have removed the accursed from among you.
Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
14 And ye shall be brought near in the morning according to your tribes: and it shall be, that the tribe which the Lord will seize shall come near according to its families; and the family which the Lord will seize shall come near by households; and the household which the Lord shall seize will come near by its men.
Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
15 And it shall be, that he that is seized with the accursed thing shall be burnt with fire, he, and all that he hath; because he hath transgressed the covenant of the Lord, and because he hath wrought wickedness in Israel.
Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
16 So Joshua rose up early in the morning, and brought Israel near by their tribes, and the tribe of Judah was seized;
Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
17 And he brought near the family of Judah, and he seized the family of the Zarchites; and he brought near the family of the Zarchites by its men, and Zabdi was seized;
Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
18 And he brought near his household by its men, and 'Achan, the son of Carmi, the son of Zabdi, the son of Zerach, of the tribe of Judah, was seized.
Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
19 And Joshua said unto 'Achan, My son, give, I pray thee, glory to the Lord, the God of Israel, and make confession unto him; and tell me, I pray thee, what thou hast done: hide nothing from me.
Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
20 And 'Achan answered Joshua, and said, Truly! I have indeed sinned against the Lord the God of Israel, and thus and thus have I done:
Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
21 I saw among the spoil a handsome Babylonish mantle, and two hundred shekels of silver, and a wedge of gold of fifty shekels in weight, and I coveted them, and took them; and, behold, they are hidden in the earth in the midst of my tent, with the silver beneath the same.
Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
22 Joshua thereupon sent messengers, and they ran unto the tent; and, behold, it was hidden in his tent, and the silver beneath it.
Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
23 And they took them out of the midst of the tent, and brought them unto Joshua, and unto all the children of Israel, and they laid them out before the Lord.
Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
24 And Joshua took 'Achan the son of Zerach, and the silver, and the mantle, and the wedge of gold, and his sons, and his daughters, and his ox, and his ass, and his sheep, and his tent, and all that he had, and all Israel were with him, and they brought them up unto the valley of 'Achor.
Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
25 And Joshua said, How hast thou troubled us! so shall the Lord trouble thee this day. And all Israel stoned him with stones, and burnt them with fire, after they had stoned them with stones.
Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
26 And they raised over him a great heap of stones [which is] unto this day; and the Lord turned from the fierceness of his anger. Wherefore the name of that place was called, The valley of 'Achor, unto this day.
Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.