< Joshua 24 >

1 And Joshua assembled all the tribes of Israel to Shechem; and he called for the elders of Israel, and for their heads, and for their judges, and for their officers, and they presented themselves before God.
Kisha Yoshua aliyakusanya pamoja makabila yote ya Israeli huko Shekemu na aliwaita wazee wa Israeli, viongozi, waamuzi na maafisa wao, nao wakajihudhurisha mbele za Mungu.
2 And Joshua said unto all the people, Thus hath said the Lord the God of Israel, On the other side of the river did your fathers dwell in old time, even Terach, the father of Abraham, and the father of Nachor; and they served other gods.
Yoshua akawaambia watu wote, “Hiki ndicho Yahweh, Mungu wa Israeli anachokisema, 'Mababu zenu kwa miaka mingi iliyopita waliishi ng'ambo ya mto Frati - Tera, baba wa Ibrahimu na baba wa Nahori - nao waliabudu miungu mingine.
3 And I took your father Abraham from the other side of the river, and I led him throughout all the land of Canaan; and I multiplied his seed, and gave him Isaac.
Lakini nilimchukua baba yenu kutoka ng'ambo ya Frati na nikamwongoza mpaka katika nchi ya Kanaani, na nilimpa watoto wengi kupitia kwa Isaka mwanaye.
4 And I gave unto Isaac, Jacob and Esau: and I gave unto Esau mount Seir, to possess it; but Jacob and his children went down into Egypt.
Na Isaka nikampa Yakobo na Esau. Nilimpa Esau nchi ya milima ya Seiri ili aimiliki, lakini Yakobo na watoto wake walishuka kwenda Misri.
5 And I sent Moses and Aaron, and I plagued Egypt in the manner as I have done among them; and after that I brought you out.
Nilimtuma Musa na Haruni, na niliwapiga Wamisri kwa mapigo. Baada ya hapo, niliwatoa ninyi.
6 And I brought your fathers out of Egypt; and ye came unto the sea; and the Egyptians pursued after your fathers with chariots and horsemen unto the Red Sea.
Niliwatoa baba zenu nje ya nchi ya Misri, nanyi mkafika hata katika bahari. Wamisri waliwafuata kwa magari na wapanda farasi hata katika bahari ya matete.
7 And they cried unto the Lord, and he put darkness between you and the Egyptians, and he brought the sea over them, and covered them; and your eyes saw what I had done on Egypt; and ye dwelt in the wilderness many days.
Na baba zenu walipomwita Yahweh, aliweka giza kati yenu na Wamisri. Aliileta bahari ije juu yao na kuwafunika. Mliona yale niliyoyakifanya huko Misri. Kisha mliishi jangwaani kwa muda mrefu.
8 And I brought you into the land of the Emorites, that dwelt on the other side of the Jordan; and they fought with you: and I gave them into your hand, and ye took possession of their land; and I destroyed them from before you.
Niliwaleta katika nchi wa Waamori, ambao waliishi katika upande mwingine mwa Yordani. Walipigana nanyi, nami niliwatia katika mkono wenu. Mliimiliki nchi yao, nami niliwaangamiza mbele yenu.
9 Then Balak the son of Zippor, the king of Moab, arose and warred against Israel; and he sent and called Bil'am the son of Beor to curse you;
Kisha Balaki mwana wa Zipori, mfalme wa Moabu, aliinuka na kuishambulia Israeli. Alimwita na kumtuma Baalamu mwana wa Beori, ili kuwalaani ninyi.
10 And I would not hearken unto Bil'am; but he had to bless you instead: and I delivered you out of his hand.
Lakini sikumsikiliza Balaamu. Kwa hakika, aliwabarikia ninyi. Basi, niliwaokoa na mkono wake.
11 And ye passed over the Jordan, and came unto Jericho; and then fought the men of Jericho against you, the Emorites, and the Perizzites, and the Canaanites, and the Hittites, and the Girgashites, the Hivites, and the Jebusites: and I gave them up into your hand.
Mlivuka Yordani na mkafika Yeriko. Viongozi wa Yeriko waliinuka wapigane nanyi, pamoja na Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi na Wayebusi. Niliwapa ninyi ushindi dhidi yao na niliwaweka chini ya mamlaka yenu.
12 And I sent before you the hornet which drove them out from before you, even the two kings of the Emorites: not with thy sword, and not with thy bow.
Nilituma manyingu mbele yenu, ambayo yaliwafukuzia mbali na wafalme wawili wa Waamori watoke mbele yenu. Haikutokea kwa sababu ya upanga wenu wala kwa upinde wenu.
13 And I gave you a land for which ye had not toiled, and cities which ye had not built, and ye dwell in them; of vineyards and oliveyards which ye planted not do ye eat.
Niliwapeni ninyi nchi ambayo hamkuifanyia kazi na miji ambayo hamkuijenga, na sasa mnaishi ndani yake. Mnakula matunda ya mizabibu na na mashamba ya mizeituni ambayo hamkuyapanda'.
14 Now therefore fear the Lord, and serve him in sincerity and truth; and put away the gods which your fathers served on the other side of the river and in Egypt, and serve the Lord.
Basi sasa mcheni Yahweh na kumwabudu yeye kwa uadilifu na uaminifu wote; jitengeni na miungu ambayo baba zenu waliiabudu ng'ambo ya Frati na katika Misri, na mkamwabudu Yahweh.
15 And if it be displeasing in your eyes to serve the Lord, choose for yourselves this day whom ye will serve: whether the gods which your fathers that were on the other side of the river served, or the gods of the Emorites, in whose land ye dwell; but as for me and my house, we will serve the Lord.
Na kama inaonekana kuwa ni vibaya machoni penu kumwabudu Yahweh, chagueni ninyi katika siku hii ya leo ni nani mtakayemtumikia, kama ni miungu ambayo baba zenu waliiabudu ng'ambo ya Frati, au miungu ya Waamori, ambao ninyi mnakaa ndani ya nchi yao. Lakini kwangu mimi na nyumba yangu, tutumwabudu Yahweh.”
16 And the people answered and said, Far be it from us to forsake the Lord, to serve other gods;
Watu walijibu na kusema, “Hatutaweza kumwacha Yahweh na kuitumikia miungu mingine,
17 For the Lord our God it is that hath brought us and our fathers up out of the land of Egypt, from the house of slavery, and who hath done those great signs before our eyes, and preserved us upon all the way whereon we have gone, and among all the people through the midst of whom we have passed:
kwa kuwa ni Yahweh Mungu wetu ambaye alitutoa sisi na baba zetu kutoka katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa, na ambaye alifanya hizo ishara kubwa mbele yetu, na ambaye alituhifadhi sisi katika njia zote ambazo sisi tuliziendea, na miongoni mwa mataifa yote ambayo tulipita kati kati yake,
18 And the Lord hath driven out all the nations, and the Emorites who dwelt in the land, from before us; therefore also will we serve the Lord; for he is our God.
Na Yahweh aliwaondoa mbele yetu watu wote, na Waamori walioishi katika nchi hii. Hivyo, tutamwabudu Yahweh pia, kwa kuwa ni Mungu wetu”
19 And Joshua said unto the people, Ye will not be able to serve the Lord; for he is a holy God; he is a watchful God; he will not have any indulgence for your transgressions and for your sins;
Lakini Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikia Yahweh, kwa kuwa ni Mungu mtakatifu; ni Mungu mwenye wivu; hatawasamehe makosa na dhambi zenu.
20 If ye forsake the Lord, and serve strange gods, then will he again do ye evil, and consume ye, after that he hath done you good.
Kama mtamwacha Yahweh na kuabudu miungu ya kigeni, basi atageuka na kuwaharibu. Atawaangamizeni baada ya kuwa amewatendea mema.”
21 And the people said unto Joshua, No; nevertheless the Lord will we serve.
Lakini watu walimwambia Yoshua, “Hapana, tutamwabudu Yahweh.”
22 And Joshua said unto the people, Ye are witnesses against yourselves that ye yourselves have chosen for you the Lord, to serve him. And they said, We are witnesses.
Kisha Yoshua akawaambia watu, “Ninyi ni mashahidi dhidi yenu wenyewe kuwa mmemchagua Yahweh ninyi wenyewe, ili mmwabudu yeye.” Watu walijibu, “Sisi ni mashahidi.”
23 And now put away the strange gods which are in the midst of you, and incline your heart unto the Lord the God of Israel.
“Sasa wekeni mbali miungu ya kigeni iliyoko kwenu, na geuzeni moyo wenu umwelekee Yahweh, Mungu wa Israeli.”
24 And the people said unto Joshua, The Lord our God will we serve, and his voice will we obey.
Watu wakamwambia Yoshua, “Tutamwabudu Yahweh Mungu wetu. Tutaisikiliza sauti yake.
25 And Joshua made a covenant with the people on that day, and set them a statute and an ordinance in Shechem.
Yoshua alifanya agano na watu siku hiyo. Aliziweka maagizo na sheria huko Shekemu.
26 And Joshua wrote these words in the book of the law of God; and he took a great stone, and set it up there under the oak, that was by the sanctuary of the Lord.
Yoshua aliyaandika maneno haya katika kitabu cha sheria za Mungu. Alichukua jiwe kubwa na kulisimamisha hapo chini ya mti wa mwaloni uliokuwa karibu na mahali pa takatifu pa Yahweh.
27 And Joshua said unto all the people, Behold, this stone shall be among us as a witness; for it hath heard all the words of the Lord which he spoke unto us: it shall be therefore as a witness against you, that ye may not deny your God.
Yoshua akawaambia watu, “Tazama, jiwe hili litakuwa ushuhuda dhidi yenu. Limeyasikia maneno yote ambayo Yahweh alitwambia. Hivyo, litakuwa ni shahidi dhidi yenu, hamtakiwi kumkana Mungu wenu.”
28 And Joshua let the people depart, every man unto his inheritance.
Basi Yoshua aliwaacha watu waende zao, kila mmoja alienda kwenye urithi wake.
29 And it came to pass after these things, that Joshua the son of Nun, the servant of the Lord, died, one hundred and ten years old.
Baada ya mambo haya, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Yahweh, alikufa akiwa na miaka 110.
30 And they buried him on the border of his inheritance at Timnath-serach, which is on the mountain of Ephraim, on the north side of mount Ga'ash.
Walimzika katika mpaka wa urithi wake mwenyewe huko Timnathi Sera, ambayo iko kwenye nchi ya milima ya Efraimu, upande wa Mlima Gaashi.
31 And Israel served the Lord all the days of Joshua, and all the days of the elders who lived many days after Joshua, and who had known all the deeds of the Lord, that he had done for Israel.
Israeli ilimwabudu Yahweh siku zote za maisha ya Yoshua, na siku zote za wazee ambao walidumu pamoja na Yoshua, wale ambao waliona kila kitu ambacho Yahweh alikuwa ameifanyia Israeli.
32 And the bones of Joseph, which the children of Israel had brought up out of Egypt, they buried in Shechem, in a parcel of the field which Jacob had bought of the sons of Chamor the father of Shechem for one hundred kessitah: and it remained the inheritance of the children of Joseph.
Mifupa ya Yusufu ambayo watu wa Israeli waliileta kutoka Misri, waliizika huko shekemu, katika sehemu ya nchi ambayo Yakobo alikuwa ameinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu. Aliinunua kwa vipande mia moja vya fedha, na ulikuwa urithi kwa wazawa wa Yusufu.
33 And Elazar the son of Aaron died; and they buried him on the hill of Phinehas his son, which was given him in the mountain of Ephraim.
Eliazeri mwana wa Haruni alikufa pia. Walimzika huko Gibea, katika mji wa ambao alikuwa amepewa Finehasi mwanaye, na ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu.

< Joshua 24 >