< Joshua 21 >
1 Then came near the heads of the divisions of the Levites unto Elazar the priest, and unto Joshua the son of Nun, and unto the heads of the divisions of the tribes of the children of Israel;
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 And they spoke unto them at Shiloh, in the land of Canaan, saying, The Lord commanded by the hand of Moses to give unto us cities to dwell in, with the open spaces thereof for our cattle.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 And the children of Israel gave unto the Levites from their inheritance, at the order of the Lord, these cities and their open spaces.
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 And the lot came out for the families of the Kehathites: and the children of Aaron the priest, who were of the Levites, obtained from the tribe of Judah, and from the tribe of Simeon, and from the tribe of Benjamin, by lot, thirteen cities.
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 And the rest of the children of Kehath obtained from the families of the tribe of Ephraim, and from the tribe of Dan, and from the half tribe of Menasseh, by lot, ten cities.
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 And the children of Gershon obtained from the families of the tribe of Issachar, and from the tribe of Asher, and from the tribe of Naphtali, and from the half tribe of Menasseh in Bashan, by lot, thirteen cities.
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 The children of Merari after their families obtained from the tribe of Reuben, and from the tribe of Gad, and from the tribe of Zebulun, twelve cities.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 And the children of Israel gave unto the Levites these cities with their open spaces, as the Lord had commanded by the hand of Moses, by lot.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 And they gave from the tribe of the children of Judah, and from the tribe of the children of Simeon, these cities which are called by name.
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 And the children of Aaron, of the families of the Kehathites, of the children of Levi, obtained them; —for they had the first lot.
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 And they gave unto them Kiryath-arba', [the father of 'Anak, ] which is Hebron, in the mountain of Judah, with the open spaces thereof round about it;
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 But the fields of the city, and its villages, they gave to Caleb the son of Yephunneh for his possession.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 And to the children of Aaron the priest they gave the city of refuge for the manslayer, Hebron with its open spaces, and Libnah with its open spaces,
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 And Yattir with its open spaces, and Eshtemoa' with its open spaces.
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 And Cholon with its open spaces, and Debir with its open spaces,
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 And 'Ayin with its open spaces, and Yuttah with its open spaces, and Beth-shemesh with its open spaces: nine cities from those two tribes.
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 And from the tribe of Benjamin, Gib'on with its open spaces, Geba' with its open spaces,
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 'Anathoth with its open spaces, and 'Almon with its open spaces: four cities.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 All the cities of the children of Aaron, the priests, were thirteen cities with their open spaces.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 And the families of the children of Kehath, the Levites, who remained of the children of Kehath, obtained the cities of their lot from the tribe of Ephraim.
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 And they gave to them the city of refuge for the manslayer, Shechem with its open spaces in the mountain of Ephraim, and Gezer with its open spaces,
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 And Kibzayim with its open spaces, and Beth-choron with its open spaces: four cities.
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 And from the tribe of Dan, Elteke with its open spaces, Gibbethon with its open spaces,
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Ayalon with its open spaces, Gath-rimmon with its open spaces: four cities.
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 And from the half tribe of Menasseh, Ta'nach with its open spaces, and Gath-rimmon with its open spaces: two cities.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 All the cities were ten with their open spaces for the families of the children of Kehath that remained.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 And unto the children of Gershon, of the families of the Levites, [they gave] from the other half tribe of Menasseh the city of refuge for the manslayer, Golan in Bashan with its open spaces, and Be'eshterah with its open spaces: two cities.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 And from the tribe of Issachar, Kishyon with its open spaces, Daberath with its open spaces,
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Yarmuth with its open spaces, 'En-gannim with its open spaces: four cities.
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 And from the tribe of Asher, Mishal with its open spaces, Abdon with its open spaces.
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Chelkath with its open spaces, and Rechob with its open spaces: four cities.
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 And from the tribe of Naphtali, the city of refuge for the manslayer, Kedesh in Galilee with its open spaces, and Chammothdor with its open spaces, and Karthan with its open spaces: three cities.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 All the cities of the Gershunites according to their families were thirteen cities with their open spaces.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 And unto the families of the children of Merari, the remainder of the Levites, [they gave] from the tribe of Zebulun, Yokne'am with its open spaces, and Karthah with its open spaces,
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Dimnah with its open spaces, Nahalal with its open spaces: four cities.
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 And from the tribe of Gad, the city of refuge for the manslayer, Ramoth in Gil'ad with its open spaces, and Machanayim with its open spaces,
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Cheshbon with its open spaces, Ya'zer with its open spaces: four cities in all.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 All the cities for the children of Merari after their families, they who were remaining of the families of the Levites, even their lot was twelve cities.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 All the cities of the Levites in the midst of the possession of the children of Israel were forty and eight cities with their open spaces.
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 These cities were every one with their open spaces round about them: thus it was with all these cities.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 And the Lord gave unto Israel all the land which he had sworn to give unto their fathers; and they possessed it, and dwelt therein.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 And the Lord gave them rest round about, all just as he had sworn unto their fathers: and there stood not up before them a man of all their enemies; all their enemies the Lord delivered into their hand.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 There failed not aught of all the good thing which the Lord had spoken unto the house of Israel: it all came to pass.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.